Deprecated: strlen(): Passing null to parameter #1 ($string) of type string is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-includes/html-api/class-wp-html-tag-processor.php on line 876

Deprecated: strlen(): Passing null to parameter #1 ($string) of type string is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-includes/html-api/class-wp-html-tag-processor.php on line 876
Fanya hiki kitu unapokuwa na watu mara zote - SONGA MBELE

Fanya hiki kitu unapokuwa na watu mara zote


Utagundua kwamba wiki hii nimekuletea makala za namna ya kuhusiana na watu, kuanzia juzi, jana na hata leo. Lengo ni moja tu. Uweze kujifunza saikolojia ya binadamu kwa undani na ikusaidie kuwa mtu mwenye ushawishi zaidi kuliko mtu mwingine ambaye amekuzunguka.

Nakumbuka wakati nipo chuoni, nilipata kusoma kitabu cha Dale Carnergie kinachoitwa How to Win Friends And Influence People.

Hiki ni kitabu, kama jina lake linavyosema, kipo hivyo hivyo kwelikweli. Nilikisoma kwa umakini mkubwa sana, nikatumia mbinu zilizokuwe kwenye hiki kitab. Muda si mrefu, nikaanza kuwa mtu mwenye ushawihi miongoni mwa watu niliokutana nao.

Kwenye hili la kuwajali wengine kuna mengi ambayo unaweza kufanya.

  1. Unaweza kuwajali kwa kukumbuka majina yao
  2. Unaweza kuwajali wengine kwa kukumbuka tarehe zao za kuzaliwa
  3. Unaweza kuwajali na kufuatilia vitu wanavyopendelea
  4. Kuwasifia n.k.

Rafiki yangu, kuanzia leo hii, hatakama ulikuwa hujali sana kuhusu maisha ya watu. anza kuonesha kwamba unawajali hao watu. Onesha hilo kwa vitendo, hata kama unaongea na hao watu kwa simu,

Na ubora vitu unavyohitaji kuonesha kwa watu kuwa unawajali siyo vitu vya gharama. Ni vitu vya ambavyo unaweza kufanya tena bure kabisa.

Kwa hiyo basi, kuanzia leo hii, jenga utaratibu wa kuonesha kuwa unajali wengine. Hiki kitu kitakuweka mbele kuliko watu wengine wote ambao umewahi kukutana nao kwenye maisha yako.

Na kujali kunaanzia hapahapa. Kama umeipenda hii makala au ambazo umesoma siku za nyuma, washirikishe wengine unaowajali ili waisome. Watumie link hapa chini

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE

Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X