Jibu la kuwapa watu wanaokuja kukopa kwako


Rafiki yangu nadhani moja ya shida Kubwa ambazo zinawakumba watu wengi ni kushindwa kuwa na nidhamu ya fedha. Hivyo, kwa sababu hawana nidhamu ya na fedha. Wanatumia fedha zao hovyo na bado wanakuja kwako wakitaka uwakope.

Ninachotaka kukwambia leo ni kuwa  kama hawana nidhamu na fedha zao, usitegeemee  kwamba ukiwakopa watakuwa na nidhamu Na fedha yako. Na Wala siyo kwamba unakuwa unawasaidia kama unavyodhani, badala yake unakuwa unazalisha tatizo.

Hawakuwa na nidhamu Na fedha yao, hawatakuwa na nidhamu yako. Wataitumia hovyohovyo. Itaisha na watashindwa kukulipa.

Wewe utakuwa umejipa jukumu la kudai. na kama unavyojua, kukopa ni sherehe ila kulipa ni matanga.

Sasa ili kuondokana na Hali hiyo, hakikisha kuwa haukopi kabisa. Ipende pesa yako, vizuri sana kuliko unavyopenda kitu kingine rafiki yangu.

MTU akikwambia naomba unikopeshe kiasi fulani Cha fedha, mjibu hivi.

Nashukuru sana kwa KUNIAMINI sana na kuniona mimi kuwa mtu ambaye naweza kukusaidia

Nilitamani sana nikusaidie siku ya leo, Ila umechelewa kidogo kuniambia. Laiti ungekuja asubuhi ningeweza kukusaidia vizuri Sana.

Maana muda si mrefu nimetoka kufanya muamala mkubwa. Hivyo sitaweza kukupa hela maana muamala niliyofanya umechukua hela nyingi na bado hapa natafuta nyingine za kuongezea.

Kwa Leo nakushauri ujitahidi uangalie sehemu nyingine.

Asante sana kwa KUNIAMINI.

Kalili hii kauli, na itumie hii mara zote. Ukishamwambia mtu hivyo, anakuwa hana cha kusema zaidi ya hapo.

Itakusaidia sana


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X