Njia Nane Zitakazokuwezesha Wewe Kulipwa Mara Mbili Mpaka Mara Kumi Zaidi


Moja ya tamanio la watu wengi ni kulipwa kiwango kikubwa kuliko ambavyo wanalipwa sasa hivi au  kupata kipato kikubwa zaidi ya wanavyopata sasa. Nina hakika hata wewe ungependa kulipwa zaidi ya unavyolipwa sasa, pengine ungependa kupata kipato mara mbili mpaka mara tatu zaidi ya unavyopata sasa hivi, si ndio? sasa kwenye andiko la siku ya leo tunaenda kuona mbinu ambazo zitakusaidia wewe kulipwa mara mbii mpaka mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa hivi. Mbinu hizi ambazo tunaenda kuona hapa, ni mbinu ambazo zimethibitishwa kufanya kazi na haziwezi kukuangusha endapo utazitumia kama zilivyoelezwa kwenye andiko la leo.

NJIA YA KWANZA NI KUFANYA KAZI YA UNAVYOLIPWA

Huu najua ni utamaduni ambao haujazoeleka kwa watu wengi. Kuna vijana wengi ambao siku hizi wanalia ajira mitaani ila wakishapata hizo ajira, wanarelax  na hivyo kushindwa kuchapa kazi kama inavyotakiwa. Moja ya kitu ambacho mimi mwenyewe kimekuwa kikinishangaza ni kuona kwamba vijana wengi wanaandika kwenye CV zao kwamba ni wachapakazi na wanaweza kufanya kazi kwenye hali yoyote, ila pale wanapopata kazi, wanakuwa wazembe kiasi kwamba wanashindwa kufanya kazi na kuleta matokeo ambayo wanaahidi wakati wa kuomba kazi.

Sasa siku ya leo nataka nikwambie kwamba achana na uzembe wako, kama unataka kulipwa zaidi.  Fanya kazi kwa kujituma zaidi ya unavyolipwa, uhakika ni kwamba hiki kitu baadaye kitakufanya ulipwe zaidi ya unavyolipwa sasa.

Usije ukachukukulia kuwa juhudi zako ambazo unaweka kwa sasa hivi, zinapotea bure. Unaweza kusema kwamba bosi wako hazioni ila ukweli ni kwamba anaziona hata kama hatakuwa hasemi. Na pengine kuna kitu cha kipekee ambacho atakuwa anakiandaa kwa ajli yako. Au hata kama bosi wako hazioni wala kujali juhudi zako ambazo unaweka. Fahamu kuwa kuna watu wengine ambao wanajali na wanapenda sana juhudi zako, hivyo, kuna siku katika mazingira na namna ambayo wewe mwenyewe hutegemei watu hao watakutafuta ili uende kufanya nao kazi.

Hamna juhudi zako zinapotea bure. Kiufupi ni kwamba asili, ilivyo ni kwamba, hakuna kitu chochote ambacho huwa unafanya unafanya ambacho huwa kinapotea bure. Ndiyo maana wahenga wetu walituasa vizuri waliposema kwamba unavuna ulichopanda. Ukipanda mbegu nzuri, utapata mavuno mazuri, lakini wakati huohuo ukipanda mbegu mbaya utavuna mavuno mabaya.

Ukipanda mbegu ya uchapakazi, utpata mavuno yake.

Ukipanda mbegu ya uzembe, maavuno yake utayapata pia.

Kwa hiyo, kwenye maisha unapaswa kuchagua, unapaswa kuchagua mbegu nzuri ya uchapakazi dhidi ya mbegu ya uzembe. Maana uchapakazi na kufanya kazi kwa bidii na kujituma zaidi ya unavyolipwa kunalipa zaidi ya kitu kinginecho chochote.

Sikiliza, kama wewe kwenye maisha yako, unafanya kazi kwa kusukumwa. Yaani, kama ni mpaka usukumwe na kufuatiliwa ili uweze kufanya kazi. basi achana na hiyo tabia kuanzia siku ya leo. Badala yake anza kujituma na kufanya kazi hata kama hakuna mtu yeyote yule wa kukusukuma nyuma ya pazia. Kwanza sifa ya kufanya kazi bila ya kusukumwa wala kufuatliliw na mtu yeyote ndiyo sifa ya pekee ambayo watu wanaoingiza kipato kkubwa wanayo, wewe pia unapaswa kuwa nayo.

Tena anza kuwa nayo kuanzia leo hii.

Nakukmbuka kuna kipindi nilikuwa nafanya kazi na kijana mmoja hivi ambaye alikuwa anafanya kazi kwa bidii na kujituma sana. kiukweli nilikuwa napenda kazi zake ambazo alikuwa anafanya na siku zote hakuwahi kuniangusha. Mara nyingi sana nilipokuwa nikimpa kazi ya kufanya kwa siku husika, yeye alikuwa anaweza kuifanya ndani ya saa tatu mpaka nne, na kuimaliza kisha kuendelea na mambo mengine. Hivi union hicho kitu ee. Yaano, kwake kazi ya siku nzima anaifanya ndani ya masaa matatu na kuimalizaa.a

Alikuwa haitaji usimamizi wangu muda wote.

Alikuwa anajongeza snaa kwenye kazi yake na kufanya zida.

Mara zote nilikuwa nikiona juhudi zake, nilizipenda kweli.

Lakini kumbe kuna watu wengine ambao walikuwa wakiona juhudi zake pia. Siku moja, niliona ananifuata na kuniambia kwamba anaachan kazi kwangu. Kitu hiki kwangu kilikuw akama mwiba maana nilikuwa nikipenda kuwa na kijana kama yule anayechapa kazi na kujituma badala ya kijana anayesimamiwa na kufuatiliwa nyuma muda wote.

Nilijaribu kumwongezea mshahara mara mbili ii tuendelee kufanya kazi kwa pamoja, lakini alikuwa ameshafikia uamuzi wa kuondoka. Mpkaka leo hii huwa anakutana naye mara kwa mara, ana furaha muda wote na anapenda kazi anayofanya huku akiendeleza juhudi zake za kuchapa kazi zaidi ya anavyolipwa.

Hiki kitu kimenifunza sana, mbali na kwamba kufanya kazi kwa bidii kunakufanya unalipwa zaidi. lakini pia naona kwamba wanaofanya kazi kwa bidii wana furaha kuliko ambao wanzembe.

Wanaozembea ndio wenye majungu muda mwingi, maneno mengi ambayo hayana tija, ndio wanalalamika, ndio ambao wanapenda kuonewa huruma, wanapenda kuongezwa mishahara huku wakiwa hawaweki juhudi. Naomba unisikilize kwa kitu kimoja. Weka juhudi kwenye kazi zako unafanya. Juhudi zako unawezoweka zitakufikisha mbali zaidi ya ulipo sasa hivi.

Penda sana kufanya kazi zaidi ya unavyolipwa

SOMA ZAIDI: JITUME KWA FAIDA YAKO

FANYA KAZI KWA BIDII

NJIA YA PILI NI KUSOMA VITABU

Kusoma vitabu kuna uwezo wa kukufanya ulipwe mara mbili mpaka mara tatu au hata mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa hivi. kama kuna kitu ambacho unapaswa kukipa kipaumbele kwenye maisha yako nbasi ni kusoma vitabu na kupenda kujifunza mara kwa mara.

Unaweza kuwa unajuliza, kwani kusoma vitabu kunawezaje kunifanya mimi  niongeze kipato changu mara mbili mpaka mara tatu zaidi ya ninavyoingiza sasa hivi.

Kwanza ni kwamba kusoma vitabu na kupenda kujifunza kunakufanya unakuwa na maarifa ambayo wengine wanakuwa hawana. Hivyo, hayo maarifa yanakuwezesha wewe kufanya uamuzi ambao wengine wanakuwa hawana.

Ebu tuchukulie mfano, umesoma na kujifunza kuhusu uwekezaji kwenye hisa. Umeuelewa vizuri na na kutumia maarifa haya mauzri uliyoyapata ukaanza kuwekeza kwenye hisa, hatifungani pamoja na vipande. Baada ya siku kadhaa, utaanza kupata gawio linatokana na uwekzaji wako kwenye hisa. Hicho ni kipato zaidi rafiki yangu ambacho ulikuwa huingizi mwanzoni rafiki yangu.  Na tena unakipata bila kuweka juhudi zaidi.

Au tuseme unasoma kitabu kama JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEBVU. Baaada ya siku chache unajifunza ujuzi wa uandishi, ujuzi ambao unalipa na ujuzi mzuri kwenye zama hizi tunazoishi. Baada ya siku si nyingi utakuwa umeweza kuwa mwandishi mzuri ambaye anaweza kuandika andiko linaloeleweka. Unaweza kukuta unapata tenda z kuandika maeneo mbalimbali ambayo hata hukutegemea kama magazetini, hicho ni kipato cha ziada rafiki yangu hapo kinakuwa kinagonga mlango.

Lakini pia kusoma na kujifunza kunakusaidia wewe kuweza kupangilia ratiba yako na hivyo, kujua majukumu yapi uyafanye lini na majukumu yapi usiyafanye kwa wakati gani. wakati hali ni tofauti kwa mtu ambaye hasomi.

Kusoma vitabu na kupenda kujifunza kunakufanya unakuwa mmbunifu. Kitu hikitu kinaweza kukufanya wewe ulipwe mpaka mara tano au mara kumi zaidi.

Nakumbuka kuna mzee mmoja ambaye alikuwa anapenda sana kujifunza kupitia semina na mafunzo mbalimbali. HUYU MZEE alikuwa daktari. Kuna siku alihudhuria semina inayohusiana na upasuaji wa macho. Semina hii ilikuwa ya gharama kubwa, ila mzee huyu alilipia. Kwenye semina hii alijifunza ujuzi ambao ulikuja kumtofautisha yeye na madajtari wengine maisha yake yote.

Kumbe, kitu kimoja ambacho unasoma kwenye kitabu kinaweza kubadili maisha yako na kukufanya kuwa mtu wa tofauti kabisa.

NJIA YA TATU NI KUWAFIKIA WATU WENGI ZAIDI

Kama unamhudumia mteja mmoja, unachopaswa kufahamu ni kuwa siku huyo mteja akiacha kununua kwako basi wewe utakuwa huna kipato tena. Kama umeajiriwa maana yake unamhudumia mteja mmoja ambaye ni mwajiri wako. Kwa hiyo kipato chako kitakuwa na ukomo kwa sababu mteja unayemhudumia ni mmoja.

Sasa ebu fikiria mtu menye ujuzi kama wewe, elimu kama wewe na kila kitu kingine chochote kama wewe akiwahudumia wateja watano, unadhani atalipwa kiasi gani? maana yake atalipwa mara tano zaidi ya unavyolipwa wewe.

Kumbe basi, mara zote angalia ni kwa namna gani ambavyo unaweza kuwahudumia wateja zaidi na kupanua masoko yako.

Kama umeajiriwa, unaweza kuanza kuagalia namna ya kutumia ujuzi wako nje ya ajira, ili ule muda baada ya kutoka kazini uweze kuuwekeza kwenye biashara au kuwahudumia wengine zaidi. Kwa jinsi hii utakuwa untengeneza mifereji ya kulipwa zaidi hapo baadaye.

NJIA YA NNE NI UAMINIFU

Katika uliwngu tunaoishi sasa hivi, uaminifu ni kitu kimoja muhimu sna ambacho unahitaji. Bila uaminifu rafiki yangu takwama sana. Iwe umeajiriw au unafanya kazi kwa kujiajiri, unahitaji uaminifu  wa hali ya juu sana.

Watu wanapenda kufanya kazi na waaminifu.

SOMA ZAIDI: UAMINIFU NI MTAJI

NJIA YA TANO NI KUONGEZA THMANI KWENYE BIDHAA UNAZOTOA

Watu wanapenda kupata vitu vyenye thamani nzuri. Hakikisha kwamba kazi yoyote ile ambayo mkono wako unagusa, unaifanya kwa viwango vya juu. Kwa jinsi hii nakuhakikishia kwamba muda si mrefu, watu watamiminika ili wapate kazi zako zaidi.

NJIA YA SITA NI KUWA NA BIDHAA ZAIDI YA MOJA.

Ukiwa na bidhaa moja maana yake mteja akija kununua wako hiyo akiondoka ndiyo ameondoka. Yaani, hatarudi tena kununua tena. Ebu tuchukulie unauza redio tu. Mtu akinunnua kwako hawezi tena kuna kununua kwako redio maana tayari anayo.

Ukiwa na bidhaa zaidi ya moja maana yake mteja mmoja anaweza kununua kwako zaidi ya mara moja. na hata akinunua mara moja maana yake atanunua vitu vingi kwa wakati mmoja. Mfano ni simu, earphone, chaja, memory card, n.k

Lakini pia unamfanya mteja aweze kurudi kununua kwako mara kwa mara.

Endapo ukiwa na bidhaa moja walau iwe ni bidhaa ambayo wateja watakuwa wanakuja kununua mar kwa mara. Mfano chumvi au sukari. Hizi ni bidhaa ambazo wateja lazima watakuja kunua mara kwa mara hata baada ya kuwa wamenunua mara ya kwanza. Kwa jinsi hii kadiri watakavyokuwa wanaunua zaidi ndivyo na kipato chako kitaongezeka. Na siyo wanunue tu wenyewe kwa kurudi. Bali warudi na wateja wengine zaidi.

NJIA YA SABA NI KULIPWA KWA KAMISHENI

Kama unachapa kazi kwa bidii, badala ya kukubaliana na bosi wako akulipe kwa mshahara mwisho wa mwezi, amua kwamba unaenda kulipwa kwa kamisheni. Unajiuliza hivi kulipwa kwa kamisheni ndio nini?  Kulipwa kwa kamisheni maana yake unalipwa kulingana na matokeo unayozalisha. Yaani, kwa mfano kama unafanya kazi mgahawani. Ukiuza sahani 10 na kila sahani unalipwa elfu moja maana yake siku hiyo, utalipwa elfu kumi. Lakini, ukijisukuma zaidi ukauza sahani thelathini maana yake siku hiyo utalipwa elfu thelathini. Huku ndiyo kulipwa kwa kamisheni.

Yaani, juhudi zako zinakuwa ziaendana na bidii unavyoweka. Kadiri unavyoweka bidii zaidi kwenye kazi ndivyo ambavyo unalipwa zaidi.

Mbinu hii unaweza kuitumia kama umeajiriwa au umejiajiri.

Kwa mfano, kama unaona unaweza kuajiriwa kwenye biashara fulani na kumsaidia bosi wako kupata matokeo makubwa zaidi ya anavyopata sasa hivi. unaweza kuongea naye, mwambie kwamba  wewe unaweza kuwa na mbinu ya kusamsaidia kuongeza kipato kwenye biashara yako, lakini sharti akulipe kwa kamisheni. Hii ni nzuri sana maana hakuna anayepujwa. Unalipwa kwa jasho lako. Kadiri unavyoweka juhudi zaidi, ndivyo ambavyo unalipwa zaidi.

Kama umeajirajiri unaweza kujiwekea lengo. Labda lengo la kufanya mauzo na laki tano kila siku. Na ukajiambia kwamba nikifikisha mauzo laki tano kwa siku basi mimi mmweywe nitajilipa asilimia labda kumi. Kwa hiyo, siku ambayo unakuwa hujafikisha hiyo laki tano, utajilipa kulingana na kiwango ulichoingiza

Kama umeingiza laki moja basi utajilipa elfu kumi tu.

Hii ni njia nzuri, japo watu wengi hawaipendi kwa sababu haijazoeleka kwenye mazingira mengi. Lakini pia siyo njia rafiki kwa watu ambao hawapendi kufanya kazi kwa bidii na kujituma zaidi.

SOMA ZAIDI: Njia Tano Za Kuingiza Fedha Mtaani Kwako Kuanzia Leo

Je, Kuna Namna Na Kutengeneza Fedha Kupitia Affiliate Marketing Ukiwa Nchini Tanzania?

 

NJIA YA NANE, ACHANA NA ANASA

Unaweza kuwa unajiuliza, kwani anasa zangu zina uhusiano  gani na kulipwa zaidi. Tena, unaweza kuhitimisha kwa kusema kwamba, mimi nitaendelea na starehe zangu ila nitafania kazi hayo mengine ambayo umeeleza hapo juu.

Ninachotaka ni nikwambie ni kwamba, anasa zinapoteza muda wako mwingi ambao ungutumia kwa ajili ya kufanya kazi ya kukuongezea kipato. Anasa zitakufanya upoteze muda kwa wingi. Na muda ni mali.

Kwa hiyo, achana na kupambana na mambo ya anasa kuanzia leo hii. badala yake pambana na ndoto pamoja na malengo yako. Kila siku hakikisha kwamba unafanya kitu na unakfanyia kazi kila siku. Siku siyo nyingi wa

Lakini pia ni muhmu cha kufahamu ni kuwa kwanza anasa zinachukua fedha zako.

pili, anasa zinakupunguzia ufanisi

Na tatu unapokuwa unapambana na anasa, maana yake unakuwa na pambana na lengo ambalo siyo sahihi. Na hivyo, lengo la kuongeza kipato chako zaidi litakushinda.

Rafiki yangu, hizo ndizo njia nane za kulipwa mara nane mpaka mara kumi zaidi ya unavyolipwa sasa.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X