Endelea Kupambania Ndoto Na Lengo Lako


Kama una lengo na ndoto kubwa ambayo unaifanyia kazi. Endelea kupambania ndoto yako na lengo lako kila siku. Usirudi nyuma kwa kuanza kujilinganisha na watu wengine.

Sikiliza kila siku jiboreshe wewe mwenyewe.
Jifanyie tathimini kila mara kuangalia umatoka wapi, uko waapi unaelekea wapi.

Jisukume kila mara kufanya zaidi. Ila usijilinganishe na MTU mwingine.

Hakuna mtu mwingine mwenye lengo na ndoto Kama zako.

Kabisa….

Kila mtu anapambana na hali yake…

Kitu pekee ambacho unapaswa kuchukua kutoka kwa Watu Ni mbinu na namna ambavyo wanainuka kutoka eneo moja kwenda jingine na kusongambele.

Ila siyo kujilinganisha nao.

Kisa eti fulani kanunua gari Basi na wewe ukimbizane na gari

Kisa eti fulani kajenga NYUMBA Basi na wewe ukajenge.

Sikiliza, tulia na ndoto yako na vipaumbele.
Ukifuata kile ambacho wengine wanafanya Hutakata uishi maisha yako kama wewe. Utaishi maisha ya kuiga tu siku zote na sehemu zote. Hakuna haja ya wewe kuiga maisha.

Ishi maisha yako
Jitathimini kila mara
Fanyia kazi uliyopata kutoka kwenye tathimini yako.
Songambele.
Tukutane kwenye jukwaa la wanamafanikio.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X