Vitabu Vitano Ambavyo Kila Mfanyabiashara Makini Anapaswa Kusoma


Kwanza kabla sijaandika mambo mengi sana siku leo. Ningependa kukwambia kwamba baadhi ya vitabu ambavyo ninaenda kukueleza hapa vinapatikana bure kabisa mtdanoni, hivyo, unaweza kupakua hivi vitabu bure. Labda unajiuliza unawezaje kupakua hivi vitabu bure mtandaoni?

Hakikisha kwamba umeangalia hii video hapa, itakusaidia wewe kupakua vitabu hivi bure. Ila pia kuna vitabu vya kulipia ili uvipate, kwa vitabu ambavyo unapaswa ulipie ili uvipte, basi utatkiwa kutoa kisi kidogo mfukoni li uvipate.

Pili ni kwamba, kuna kitabu cha bure ambacho napenda kila rafiki yangu akisome.

Kupata kitabu hiki, jaza taarifa zako hapa chini, kisha bonyeza nitumie hiki kitabu.

Sasa tuendelee na vitabu vitano ambavyo kila mfanyabiashara makini anapaswa kuhakikisha kwamba amesoma. Ni vitabu ambavyo hupaswi kuchukulia kimzaha badala yake unapaswa kuvisoma na kuviweka kwenye matendo.

Mimi sijui wewe kwa sasa una miaka mingapi. Ila ninataka ujipe changamoto leo. Ebu jiulize umeishi hapa duniani kwa miaka mingapi? Halafu jiulize ni kitu gani cha kipekee umeweza kufanikisha ndani ya hiyo miaka ambayo umekuwa ukifanya kazi bila ya kusoma vitabu au bila kufufuata mwongozo wowote ule kutoka kwenye vitabu? Sasa kwa nini usijipe changamoto ya kuchukua vitabu vichache ambavyo utasoma na kufuata kwa kipindi hata cha miaka mitatu minne ijayo. Yaani, kama umekuwa unafuata mwongozo wako kwa hiyo miaka yote kwani ukitoa miaka mitatu au mitano tu ambayo utafuata mwongozo wa vitabu fulani na kuuishi unadhani utapoteza nini?

Kama kuna mwongozo wa vitabu ambao utapaswa kuufuata basi ni vitabu vifuatavyo.

Kwanza ni kitabu cha THINK AND GROW RICH

Hiki ni kitabu chako cha kwanza ambacho unapaswa kusoma kama unataka kuwa mfanyabiashara makini kwenye maisha yako. Kwenye kitabu hiki unaenda kujifunza mbinu ya kwanza kabisa ya mafanikio kwamba ni kuanza na wazo. Hakuna kitu chochote kile ambacho unaweza kufanikisha bila ya kuwa na wazo kwanza. Na wazo ukilifanyia kazi, na kulileta kwenye uhalisia hilo wazo linawezekana kukamikilika na kuja kwenye uhalisia.

Mwandishi anasema kwamba moja ya kitu ambacho huwa kinawafanya watu wengi wanashindawa kufanikiwa, iwe ni kwenye biashara au kwenye maisha ya kawaida ni kukosa uendelevu kwenye kufanyia kazi wazo ambalo wanakuwa nalo. Unakuta kwamba mtu ana wazo zuri, lakini mtu huyu anaanza kulifanyia kazi wazo lake na baada ya muda mfupi  unakuta amekata tamaa na hivyo anakuwa halifanyii wazo lake kama ambavyo inapaswa na mwisho wa siku anakata tamaa na kuachana nalo.

Tena siku hizi tafiti mbalimbali zinaonesha vizuri. Ambapo zinaonesha kwamba kati ya biashara mia moja ambazo huwa zinaanzishwa kila mwaka karibia biashara kumi zinakufa. Moja ya kitu ambacho huwa kinafanya hizi biashara kufa ni kukosa mwendelezo au mtu wa kuendelea kufanyia kazi wazo la awali la biashara.

Kwenye kitabu hiki utakutana na mwanadishia ambaye atakupa mbinu kumi na tatu, ambazo zitakusaidia wewe kuweza kuinua biashara yako kutoka sifuri mpaka kuifikisha kwenye viwango vikubwa .

Je, upo tayari kwa ajili ya kusoma hiki kitabu na kufuata mwongozo wake.

ANZA KWA KUSOMA UCHAMBUZI WAKE HAPA

PILI NI KITABU CHA THE RICHEST MAN IN IBABYLON

Hiki ni kitabu kingine cha kipekee ambacho haswa kinazungumzia kuhusu fedha. Fedha ni kitu cha muhimu sana kwenye maisha ya kawaida na kwenye biashara. Maisha yetu ya kila siku hayawezi kwenda bila ya kuwa na fedha. Fedha ni kitu muhimu kwenye maisha ya kawaida na kwenye biashara. Ukikosa fedha unaweza kushindwa mpaka kuanzisha biashara na ukiwa na fedha ni wazi kuwa utaweza kuanzisha biashara yako kwa uzuri tu.

Sasa unahitaji kujua misingi ya kutafuta pesa, kuitumia na kuitunza. Na kitabu hiki hapa kimefunza kwa kina hasa namna ambavyo unaweza kufanyia kazi hayo yote matatu bila ya shida yoyote ile.

KITABU CHA TATU NI RICH DADA POOR DAD

Hiki ni kitabu kingine ambacho unaweza kuanza nacho. Hiki kitakusaidia zaidi kwenye utunzaji wa pesa zako. utajua ni wapi kabisa ambapo unaweza kuwekeza pesa zako kwa manufaa ya muda wa sasa na muda ujao. Utajua kwamba kuna baadhi ya vitu ambavyo watu huwa wanaunua kwa kuona kwamba vina thamani kubwa na thamani ambayo inaweza kuwafikisha mbali, ila vitu hivyo kwenye uhalisia siyo kwamba vinapanda thamani na kuwafikisha kwenye utajiri, badala yake ukweli ni kwamba vitu hivyo vinakuwa vinashuka thamani na kuzidi kuwashusha hao watu. kwa hiyo, kwenye hiki kitabu utajifunza mbinu mbalimbali za kifedha ambazo zitakusaidia kuwa NINJA linapokuja suala zima la fedha na hasa uwekezaji.

Sasa baada ya kuwa umesoma hivyo vitabu vyote na umeingia kwenye biashara. Vitabu viwili vya mwisho kwa siku ya leo vina mwongozo ambao unapaswa kuufuata na kuuishi. Ni vitabu ambavyo nashauri usome tu siyo mara moja au mara mbili ni vitabu ambavyo nashauri usome na kusoma tena.

Hivi ni vitabu ambavyo vitakusaidia wewe kuanzia sifuri na mwisho wa siku ukaishia kuwa na kila kitu kwenye maisha yako. Upo tayari kwa ajili ya kuvijua vitabu hivi

4. NI WINNING cha JACK WELCH

Hapa sasa tunaongea biashara. hiki ni kitabu kuhusu usimamizi wa biashara. Yaani, namna ambavtyo unaweza kusimamia biashara yako kitalaam mpaka ikaweza kukua. kama ulikuwa hujui ni kwamba, Jack Welch alikuwa mkurugenzi mkuu wa kampuni ya GM. Aliikuza hii kampuni kwa viwango vikubwa na alikuwa mkurugenzi mkuu kwa miaka zaidi ya 20.

kwa kipindi chote ambacho alikuwa kwenye uongozi wa juu, alijifunza mengi sana alipitia kwenye mambo mengi ambayo ametushirikisha kwenye kitabu chake hiki. Lakini siyo hilo tu, baada ya kuwa amestaafu kazi alikuwa akizunguka maeneo mbalimbali hapa duniani kwa ajili ya kuongea na vijana mbalimbali kuhusiana na masuala ya kibiashara na namna ambavyo wanaweza kukuza biashara zao.

Sasa wakati anafanya hivyo, ndivyo alikutana na maswali mengi ambayo watu walikuwa wakiuliza. Katika kuyaunganisha haya maswali ndipo alikuja kugundua kwamba hayo maswali yote yalikuwa yanatosha kuwa kitabu. Hivyo akawa ameandika maswali kujibu hayo maswali kwa kutumia uzoefu wake. Maswali haya nina uhakika kwamba wewe mwenyewe utakuwa ukijiuliza, haya maswali. Sasa kazi ni kwako siku ya leo kuhakikisha kwamba umepata kitabu hiki na kukisoma.

5. NVUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.

Naam, hiki ni kitabu ambacho nimendika mwenyewe. Ndani yake utajifunza namna ambavyo unaweza kuikuza biashara yako kwa kutumia nguvu ya vitu vidogo mpaka kuifanya hiyo biashara yako iweze kukua.

watu wengi wanashindwa kukua kwa sababu wanataka waaanzishe kitu le hii na kesho yake wawe wameza kufanya makubwa. ila kwenye hiki kitabu unaenda kujifunz kwamba kwa kutumia nguvu ya vitu vidogo unaweza kufanya makubwa kwenye maisha. je, upo tayari kwa ajili ya kuhakikisha kwamba unaitumia nguvu hii ya vitu vidogo kwenye kufanya makubwa?

sasa pata nakala ya kitabu chako kwa shilingi 20,000/-. Kupata kitabu hiki wasiliana nami kwa 0755848391

BONASI KITABU CHA SITA: HOW TO BUILD A MULTI-BILLION DOLLAR BUSINESS IN AFRICA

Hiki kitabu ameandika Strive Masiyiwa. Mmoja wa mabilionea wakubwa hapa barani Afrika. Kwenye kitabu hiki bilionea huyu katushirkisha mbinu halisi ambazo ametumia yeye kwenye kujenga biashara na kampuni zake.

hiki kitabu huwa nakisoma kila mara. Siwezi kusema mengi juu ya hiki kitabu, zaidi ya kusema kwamba kisome.

KUPATA VITABU HIVI YOTE BURE BONYEZA HAPA

Umeshajiunga na kundi letu la THINK BIG FOR AFRIKA? KAMA BADO BONYEZA HAPA

Kama bado hujasoma NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA nashauri sana uweze kusoma kitabu hiki.

Cha kufanya wasiliana nami kupitia 0755848391

Fanya hivyo sasa hivi.

Umekuwa nami

Godius Rweyongeza

0755848391

Morogoro-Tz

Kwa maswali, maoni au booking: songambele.smb@gmail.com


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X