Hivi Ndivyo Unaweza Kufanya Mishale Inayolenga KukuangamizaKuwa Baraka


Maisha hayatakuja kuwa rahisi kwako hata kidogo. Maisha yataendelea kukurushia mawe na mishale. Na kadri utakavyokuwa  na ndoto kubwa sana, ndivyo mishale itakavyokuwa mingi zaidi.

habari njema ni kwamba ukiwa mgumu, mishale hii itakuumiza kwa muda tu lakini bado utaendelea.

Kuna usemi mzuri wa kiingereza ambao unasema kuwa safari inapokuwa ngumu, wagumu ndio huwa wanaendelea na safari yao ( When the going gets tough, the tough get going) Sio wanarudi nyuma.
Sio wanakata tamaa, bali wanaendelea. Mpaka kinaeleweka (mpaka kileleni)

Sasa hapa nataka nikwambie vitu ambavyo vitakufanya wewe uweze kuendelea hata mambo yanapokuwa magumu.

KWANZA HAKIKISHA KUWA UNA MAONO MAKUBWA
Rafiki yangu, bila maono makubwa utapoteza mwelekeo hata ukisukumwa kidogo tu. Yaani utaanza kusema hiki kitu sio kwa ajili yangu (sio type yangu).
Ndio maana, Dale Carnegie anatuasa kwa kusema kwamba, vitu vingi katila dunia hii vimeweza kukamilishwa na watu ambao waliweza kuendelea pale ambapo kulionekana kwamba hakuna matumaini. Kilichowafanya watu waliofikia makubwa  waweze kuendelea ni kuwa na maono makubwa.

Kuna siku nilikuwa nasoma Tawasifu ya Thomas Edison. Niligundua kwamba Thomas Edison alishindwa sana, sana.  Ila alikuwa anaendeleka kila baada ya kushindwa. Kwake kushindwa kukikuwa kama msukumo wake wa kusongambele. Bila shaka lolote Thomas Edison alikuwa anafahamu kwamba Nyuma Ya Ushindi kuna kushindwa, kushindwa, Kushindwa. Aliendelea kusongambele kuelekea maono na ndoto yake kubwa. Hivi wewe nikikuuliza unataka kufika wapi baada ya mwaka mmoja au miaka mitatu ijayo? unataka kuwa umeifikisha wapi biashara yako miaka 10 ijayo. ukiweza kujibu maswali haya, basi nina hakika. Utakuwa na Uwezo wa kuendelea mbele hata mambo yatakapokuwa magumu.

PILI, FAHAMU KUWA VIKWAZO NI KIPIMO SAHIHI CHA BINADAMU
Hatuwezi kujua kama unaweza kufanya makubwa kama hujapitia kwenye vikwazo, changamoto, kurushiwa mawe na mishale. Chuma huwa kinakuwa imara baada ya kupitia kwenye moto.
Matatizo huwa yanaimarisha kitu nankukifanya kiwe ma nguvu zaidi. Nakubaliana na Robin Sharma aliyandika kuwa “ukitoa jasho jingi wakati wa mazoezi, utatoa damu kidogo wakati wa vita”.

Mtu anakuwa shujaa baada ya kuwa amepitia katika vikwazo na kushinda. Kwenye hili Martin Luther King Jr anasisitiza kwa kusema hivi, “kipimo sahihi cha mtu sio pale anapokuwa amesimama wakati wa utulivu, bali pale anapokuwa amesimama baada ya changamoto na vikwazo”

ANGALIA VIDEO HII YOUTUBE: Chuma Hunoa Chuma

TATU, FAHAMU KUWA FURAHA YETU SIO KUTOSHINDWA
Furaha yetu kubwa sana sio kutoshindwa, bali kuamka pale tunapoanguka. kwa hiyo mishale na mawe yanayokujia sio vitu vibaya. Bali vitu ambavyo vitakuongezea furaha pale utakapokuwa umeweza kuvivuka.

leo ili uweze kuvijua. 


SOMA ZAIDI: DO OR DIE: Kitu Kimoja Unachokihitaji Zaidi Kuliko Vitu Vingine

Ni mimi anayejali mafanikio yako,
GODIUS RWEYONGEZA
KUWA MIONGONI MWA WATU AMBAO WANAPOKEA MAKALA MAALUMU KWA WATU MAALUMU KWA KUBONYEZA HAPA
SUBSCRIBE KWENYE CHANNEL YANGU YA YOUTUBE HAPA

JIUNGE NAMI KWENYE NURU ANGAZA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X