Anza Na Moja


Habari za leo rafiki na ndugu msomaji wa SONGA MBELE BLOG . Imani yangu unaendelea vyema katika hatua ya kutafuta na kuelekea mafanikio.Karibu sana katika makala yetu ya leo ambapo tunaenda kujifunza kitu kipya ambacho kitabadili mwelekeo wa maisha yetu
anza na moja
Anza na moja


Moja ni kianzio kukubwa sana cha kila kitu. Hatuwezi kuzungumzia mafanikio katika sekta yoyote ambayo hayakuanza na moja.

Profesa mkubwa sana wa hesabu ukimuuliza siku ya kwanza alipoenda shuleni alijifunza nini? Atakwambia alianza kufundishwa moja. Au ukimuuliza profesa wa kiswahili amabaye anajua karbia robo tatu ya maneno ya kiswahili  na ukimuuliza alianza kuyafahamu maneno mangapi? Atakwambia nilianza kulifahamu neno moja.
ANZA NA MOJA

Ukiongea na mhandisi ambaye ambaye amejenga nyumba ya ghorofa 17 na kumuuliza kwamba aliwezaje kujenga nyumba yenye ghorofa 17 atakwambia alianza na kuweka tofali moja.
ANZA NA MOJA

Ukiongea na Bide mwanzilishi na mwendeshaji wa blogu ya BIDEISM na kumuuliza unawezaje kuandika makala nzuri kwenye blogu yako atakwambia huwa naanza na neno moja
ANZA NA MOJA.

Soma zaidi hapa; kama hawa wameweza kwa nini wewe usiweze

Kumbe kila hatua katikamaisha huanza na moja. Kila kitu kizuri ambacho tunakiona au mafanikio mazuri ambayo tunaona yamefikiwa na watu maarufu sana wote walianza na moja.
Usiogope kuanza kuanza na moja hata katika michezo wanariadha huanza na moja.
Kumbe mpaka hapo tunaweza kusema kwamba kila kitu kilichofikia mafanikio huanza na moja.

Wakati tunaanza na moja tukumbuke kwamba vitu vyote hapa duniani vinaendana na sheria ya asili ya kichocheo na matokeo. Ambapo kanuni hii inasema kwamba nguvu unayoiwekeza ndiyo itakayoleta matokeo fulani

Kichocheo kizuri huleta matokeo mazuri na kichocheo kibaya huleta matokeo mabaya.
Nguvu tutakayoiweka italeta mayokeo sawa kagika maisha.

Kama tutakuwa wenye furaha basi wagu watakuja kwetu wakiwa wenye furaha (kichocheo kizuri huleta matokeo mazuri)
Kama tutakuwa watu wa kulalamika watu watakuja kwetu wakilalamika. (Kichocheo kibaya huleta matokeo mabaya)

Soma zaidi hapa; niambie rafiki zako nikwambie tabia zako.

Upandea wa pili wa sheria hii unaitwa utavuna ulichopanda. 

Kwa hiyo ni muhimu kuweka kichocheo ili uweze kipata matokeo bora ili uweze kuanza na moja iliyo bora na ambayo itakuleta kwenye matokeo yaliyobora

Hakuna kitu kitakuzuia kufikia mafanikio kamautaweka kichocheo kilicho bora

Badilika sasa
Anza na moja
Anza sasa
Muda ni sasa

Endelea kusoma makala za kuelimisha kutoka kwenye blogu hii

Ili upate makala maalumu kutoka songambele blogu BONYEZA HAPA ILI KUJIUNGA

Kujiunga na kikundi cha wasapu cha SONGA MBELE BONYEZA HAPA

Kujipatia kitabu cha BIASHARA NDANI YA AJIRA  BONYEZA HAPA
Ni mimi rafiki na ndugu yako
Godius Rweyongeza
Tuwasiliane
godiusrweyongeza1@gmail.com
Asante.

BIDEISM BLOG


One response to “Anza Na Moja”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X