-
Jinsi ya kunufaika na muda wako wa safarini
Kwa namna moja au nyingine KATIKA maisha yetu ya kila siku Kuna kusafiri.
Unaweza kuwa unasafiri umbali mrefu sana kama kutoka mkoa mmoja KWENDA mwingine.Lakini muda mwingine Unaweza kuwa unasafiri eneo fupi tu. Dakika kumi, kumi na tano au SAA moja.
Bila kujali, umbali unakwenda, Bado safari Ni safari na muda huu unapokuwa unatoka eneo moja kwenda jingine Unaweza kuutumia kwa manufaa.
Huu muda wa Kutoka eneo moja kwenda jingine ukiuunganisha kwa siku, kwa wiki na kwa mwaka utajikuta kwamba unapata muda mwingi sana. Brian Tracy anasema kwa mwaka mmoja muda ambao MTU anakuwa safarini ni sawa na mhura mmoja wa chuo.
Kumbe huu muda huu ukiutumia vizuri ni wazi kuwa utajifunza mengi, na pengine hata kitu ambacho umekuwa unatamani kujifunza kwa siku nyingi utakielewa.
Ebu chukulia umekuwa unatamani kujifunza uandishi kwa siku nyingi. Ukaamua tu kuhakikisha unautumia muda ule wa safari kusikiliza vitabu na kozi za uandishi, na Kisha ukawa unatenga dakika chache tu za kuandika kila siku. Ni wazi kuwa baada ya muda utabobea.
Au kama umekuwa unapenda kujifunza mauzo. Unaweza kuutumia muda huu wa ziada kusikiliza mafunzo ya sauti ya mauzo ambayo yatakufanya uweze kubobea kwenye mauzo.
Kumbe basi, wito wangu kwako Ni mmoja TU rafiki yangu, kuanzia Leo hii, hakikisha kwamba unautumia vizuri Sana muda wako wa safari.
Utumie kujifunza na hasa kujifunza kwa kusikiliza mafunzo ya sauti. Yaani, AudiobooksHizi zitakupa maarifa yenye manufaa makubwa.
Rafiki yangu, tunahitaji kuleta mapinduzi kwenye jamii zetu. Na hatuwezi kuleta mapinduzi kwa kuendelea kufanya Mambo Yale Yale ambayo tumekuwa tunafanya kila siku. Badala yake fanya mambo ya TOFAUTI kidogo kabisa. Kama kusikiliza mafunzo ya maana wakati wengine wanapoteza muda huo kwa kuchati, kusikiliza miziki na vinginevyo.
SOMA ZAIDI: Jinsi ya kupata mafunzo yenye hadhi ya chuo
Kila la kheri
Kama ungependa kupata vitabu sauti vya Kiswahili. Basi akuhakikishia kwamba vipi. Tuwasiliane sasa kwa 075584391 ili uweze kuvipata au BONYEZA HAPA
Kisha andika AUDIOBOOKS
-
Unataka kufanya vitu vya tofauti? Siri hii hapa
Watu wanaofanya vitu vya tofauti siyo kwamba ni watu ambao wameshuka kutoka mbinguni. Siyo watu ambao wana vitu vya kipekee kukuzidi wewe. Siyo watu ambao wana elimu kubwa kulliko wewe. Isipokuwa ni kuwa wana sifa moja kubwa ambayo inawatofautisha wao na wewe.
Na sifa hii siyo nyingine, bali ni sifa ya kuamua kufanya jambo na kuhakikisha kwamba wanalifanya bila ya kurudi nyuma.
Hii ni sifa ambayo na wewe unapaswa kuwa nayo pia rafiki yangu.
Kuazia leo hii fahamika kama mtu ambaye akiamua kufanya jambo analifanya kweli.
Na kwa sababu ninataka ufahamike hivyo kuanzia leo hii. Nataka uanze kuchukua hatu akuanzia sasa hivi.
Ebu sasa hivi andika chini jambo ambalo unaamua kufanyia kazi kuanzia leo hii.
Kisha nenda kalifanyie kazi kuanzia leo hii.
Lifanyie kazi kila siku kwa siku zijazo mfululizo bila kuacha.
Jipe walau changamoto ya kufanya hilo jambo kwa siku 100 zijazo bila ya kuacha. Ukiweza kufanya hili jambo kwa siku hizi 100 bila kuacha, ni wazi kuwa utakuwa umeweza kujijengea nidhamu kubwa sana. lakini pia utakuwa umejenga njia nzuri yaw ewe kuweza kulifanya hilo jambo.
Na baada ya hapo utakuwa hauzuiliki wala kurudi nyuma hata kidogo
Chukua hatua leo hii
Kila la kheri
-
Siri itakayokuwezesha wewe kufanya makubwa
Rafiki yangu wa ukweli, sina shaka wiki yako umeianza vizui sana. Hongera sana kwa kazi.
Siku ya leo ningependa tu kukwambia kuwa kama unataka kufanya makubwa kuna vitu muhimu sana ambavyo unapaswa kuzingatia nakuhakikisha kwamba umevifuata. Vitu hivi ni pamoja na na wewe kufanya majukumu makubwa kwanza asubuhi kabla hujafanya kitu kingine.
Kama una majukumu mawili, basi nguvu yako kubwa unapaswa kuilekeza kwenye jukumu ambalo ni kubwa kwa upande wako.. Yaani, lile jukumu ambalo usipolifanya, litakuwa na madhara makubwa aidha ya muda mfupi au ya muda mrefu kwa upande wako. Ni jukumu ambaloendapo likifanyika kwa ukamilifu, litaleta matokeo mazuri. Haya majukmu mengine yanaweza kusubiri lakini hili halipaswi kusubiri.
Mara nyingi watu wengi huwa wanaliogopa na kulikwepa hili jukumu. Kitu ambacho huwa kinawafanya wakimbilie kufanya majukumu madogo madogo ambayo hayana nguvu huku wakiacha majukumu ambayo yana nguvu. Ninachotaka kukwambia siku ya leo ni kwamba, kama uanataka kufanya makubwa. kuwa tayari kufanyia kazi majukumu ambayo muda mwingine yanaonekana ni magumu.
Ni kwa sababu haya majukumu ndiyo ambayo yanaweza kukusogeza wewe kule unapotaka kufika.
Haya majukumu japo yanaogopesha lakini ndiyo ambayo yatachangia kwenye kulipwa kwako kwa asilimia 80, ukilinganisha na majukumu ambayo ni asilimia 20 ambayo siyo ya muhimu sana ambayo unakuwa unafanya.
Kazi yako siku ya leo ni kujua ni kuhakikisha kwamba unayajua majukumu yako ambayo ni ya muhimu sana, kisha kuyafanya hayo kwanza kbla hujafanya majukumu mengine.
Kwenye mambo 10 ambayo unapaswa kufanya leo, siyo yote yana umuhimu na nguvu sawa. Ni baadhi tu, au machache kabisa ambayo yana nguvu kubwa. wekeza kwenye haya machache.
Kila la kheri
-
usipofanyia kazi ndoto zako kuna mtu atakuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake
Rafiki yangu, watoto wadogo huwa wanaongoza kwa kuwa na ndoto kubwa sana. Ukiongea na mtoto yeyote yule mdogo atakwambia ndoto zake kubwa, tena kwa kujiamini.
Ongea na MTU mzima sasa. UNAWEZA kutamani kuzaba baadhi ya watu vibao. Watu walewale ambao walikuwa na ndoto kubwa utotoni, kwa sasa hawana tena hizo ndoto kubwa.
Ndoto ileile waliyokuwa nayo utotoni ukiwakumbushia wataanza kukupa sababu kibao kuonesha kwa Nini HAIWEZEKANI kufanyika.
Watakwambia uchumi mgumu.
Watakwambia vyuma vimekaza.
Watakulerea sababu nyingine kibao.Rafiki yangu, wewe ni mmoja wa hao watu?
Ndoto Yako. Naam ndoto Yako Ni kitu muhimu ambacho haupaswi kupoteza. Na ukiona umepoteza ndoto zako, ujue tu lazima Kuna MTU anaenda kukuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake.
Unajua kwa nini?
Kwa sababu dunia haipendi kukaa na utupu. Popote pale kunapokuwa na utupu dunia inatafuta sababu ya kuhakikisha pamejaa.
Kama sehemu Haina mazao Basi itakuwa na magugu.
Kama sehemu ubongo hauna mawazo chanya, basi utakuwa na mawazo hasi.Kumbe na wewe usipofanyia kazi ndoto zako, lazima tu kutakuwa na mtu ambaye atakuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake. Kama MTU hatakuajiri ufanyie kazi ndoto zake. Basi visingizio vitakumeza, kwenye kufanyia kazi ndoto zake.
Sasa rafiki yangu, kuanzia leo amua kitu kimoja tu. Kufanyia kazi ndoto kwa kufa na kupona. Pambania ndoto zako rafiki yangu hata kwa kuanzia chini Sasa hivi.
Kila la kheri
Sasa kitu kikubwa cha kufanya leo ni wewe kuhakikisha kwamba unaanza kufanyia kazi.
-
Hivi ndivyo unapaswa kugawanya muda wako Kama una ndoto kubwa
Rafiki yangu mpambanaji, bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Hongera sana kwa hilo. Siku ya leo ningependa kuongea na wewe machache rafiki yangu mwenye ndoto kubwa.
Ukweli ni kuwa inachukua muda kufikia mafanikio makubwa: unapaswa kuyapambania mafanikio Yako makubwa Kama vile hakuna Kesho. Muda wako wewe mpambanaji unapaswa kuwa umegawanywa sehemu za muhimu tu.
Muda wa kufanyia kazi ndoto zako. Hapa unafanya kila linalowezekana kuhakikisha umezipambania ndoto na malengo Yako kila wakati. Unafanya kazi kwa bidii na haurudi nyuma
Inachukua Muda kufikia ndoto kubwa Ila inawezekana.PILI ni muda wa familia au watu wako wa KARIBU. Huu Ni muda mwingine ambao unapaswa kuwa KARIBU na familia yako au watu wako wa KARIBU.
Ni hivyo tu. Vingine vilivyo nje ya hapo havipaswi kupata muda wako.
Weka muda wako, NGUVU zako na Akili zako kwenye hivyo vitu viwili tu.Nina vitabu viwili vinavyokufaa sana wewe mpambanaji. Kwanza ni JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
Na pili Ni kitabu Cha mwongozo wa wapambanaji. Hustlers Guide. Hivi vitabu viwili hivi, vina mwongozo na kila kitu unachohitaji kujua kuhusu kufanyia kazi malengo na ndoto zako mpaka vikatimia. Cha kufanya hapa Ni kitu kimoja tu. Wasiliana nami kwa 0755848391 ili uweze kupata Nakala zako mapema.
vitabu vyote viwili Ni 30,000/- kimoja ni hardcocopy (JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO) NA gharama yake Ni 20,000/-
na mwongozo wa wapambanaji ni softcopy. Gharama yake ni 10,000/-. Vipate vyote, utanishukuru baadaye.
Nakutakia kila la kheri.
-
Ufanyeje pale bidii yako inapotumika kama mtaji kwa watu wengine
Siku moja kuna rafiki yangu aliniuliza swali, alitaka kujua kuwa unafanyaje pale ambapo unakuwa na bidii na watu wanajua kuwa una bidii ila wanataka wakutumie.
Leo ningependa kujibu swali hili kwako wewe ambaye unaona kwamba una bidii na watu wanaitumia hovyo. Kwanza ningependa kwa kuanza kusema kwamba unapaswa kuwa na bidii kwenye kazi zako. hakikisha kazi yako yoyote ile unayogusa unaifanya kwa bidii, na siyo tu unaifanya kw abidii, bali unaifanya kwa ubora wa hali ya juu sana.
Kama wewe unaona kwamba lazima bosi wako awepo ili ufanye kazi. HUFAI.
Kama unaona kwamba bosi wako akitoka unapumua kwa nguvu kwa vile ametoke. Jua kwamba hufai.
Kama muda wa kazi unachati, unaongea umbea na unajificha kwenye migongo ya watu wngine. Hufai pia.
Rafiki yangu, wewe unapaswa kuwa mchapakazi wa hali ya juu sana. chapa kazi mara zote na sehemu zote, chapa kazi kwelikweli kiasi kwamba asipo mtu ambaye anapaswa kukuzidi kwenye kuchapa kazi.
Na kwenye hii dunia kuna vitu viwili ambavyo haupaswi kuruhusu mtu yeyote akuzidi kwenye kuvifanya, vitu hivi ni kufanya kazi kwa bidii na kujituma.
Kama kuna watu wanakuzidi kwenye hivyo vitu viwili. Basi funguka sasa hivi.
SASA baada ya kuwa nimesema hayo yote kuhusiana na kuchapa kazi kwa bidii. Inawezekana kuna watu watataka kukutumia wewe kwa manufaa yao zaidi kwa vile wanaona unachapa kazi kw abidii.
Na kama unasema watu wanakutumia, kwa lugha nyingine unamaanisha kwamba unafanya kazi kwa viwango vikubwa ukilinganisha na malipo ambayo unapata. Hivyo, unalipwa kiasi kidogo ukilinganisha na vile anavyopaswa kuwa analipwa.
Laiti ungekuwa unalipwa vizuri usingesema hivyo.
Kwa hiyo, kama unaona kwamba haulipwi kama vile unavyostahili unaweza kufanya yafuatayo.
Kwanza, unaweza kuamua kuacha kazi ili uweze kuweka juhudi zako sehemu nyingine ambayo itakulipa kulingana na kazi yako. Huu ni ukweli ambao pengine hukuutegemea lakini unapaswa kuubeba na kuufanyia kazi bila yakuchelewa.
Pili, kama unaona hiyo ni ngumu, basi unapaswa kuonana na bosi wako na kumwambia kuwa anapaswa kukuongeza malipo ili yaendane na viwango vya kazi unayoweka. Hapa nenda na vielelezo vyote ambavyo utahitaji kuonesha kwa bosi wako ili kuthibitisha hilo
Na tatu na mwisho, ni kwenda kwa bosi mwingine ambaye anaweza kukulipa kiwango unachoona unastahili.
Hayo ndiyo mambo matatu ambayo utahitaji kufanyia kazi rafiki yangu,ili kuhakikisha kwamba u
KITU Kikubwa zaidi ni kwamba haupaswi kuja kuzama kwenye kukazania kulipwa na bosi wako na wakati huohuo thamani na ufanisi wako ukapungua. Muda wote huo, ufanisi wako unapaswa kuwa unaongezeka.
Na hata wachezaji wa mpira huwa wanapandishwa viwango vya malipo kutokana na vile wanavyokuwa wanazidi kuwa bora zaidi kwenye kazi zao. Hivyo, kwa msingi huo basi, unapaswa kuongeza uchapaji wa kazi, ufanisi na ubora wa kazi bila kuacha ili kuendelea kupanda viwango
Kila la kheri
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Karibu Kwenye Semina Ya Kufanya Makubwa Mwaka 2023: Fanikisha Ndani Ya Miezi Sita Kile Ambacho Wengine Huwa Wanafanya Kwa Mwaka Mzima
Rafiki Yangu mpendwa, bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Moja ya jambo la msingi kabisa ambalo unahitaji kuhakikisha kwamba umelifanya kwenye maisha yako ni kujenga utaratibu wakujifunza. Kujifunza kunaweza kuwa kupitia kusoma vitabu, kusikiliza mafunzo ya sauti au mafunzo ya vitendo pamoja na semina.
Kwa kulitambua hili, mwaka huu tutakuwa na semina ya ana kwa ana ambayo itafanyika tarehe 24 juni. Itakuwa ni siku ya jumamosi na itafanyika hapa mkoani Morogoro.
Lakini kabla sijajuelez zaidi kuhusu semina, ebu kwanza tuongee kuhusu uhitaji wa wewe kufanya makubwa.
Eb u pata picha malengo uliyoyaweka ndani ya mwaka huu 2023, je, kuna hatua ambazo unaona unapiga? Je, unaona kwamba unaweza kuwa unapiga hatua zaidi lakini haujui ni kwa namna gani ambavyo unaweza kupiga hizo hatua zaidi?
Je, unajiuliza ni vitu gani ambavyo vinahitajika kwako ili kuhakikisha kwamba unapiga hatua na kuweza kufanya makubwa, naam, makubwa sana.
Nalijua hilo nap engine hilo siyo kwamba linakusumbua wewe peke yako, ni jambo ambalo linawasumbua wengi. mtu anakuwa na malengo, anaweka malengona anaanza kuyafanyia kazi, ila sasa mwisho wa siku mtu huyo anashindwa kuyafanyia kazi malengo yake mpaka kufikia mwisho. Ukifuatilia kwa undani unaweza kugunda kuwa kuna vitu viwili ambavyo vinamzuia mtu.
Msukumo wa ndani wa kufanikisha kile alichopanga au
Kukosa mbinu sahihi za kumwezesha kufanikisha malengo yake.
Kwa kulitambua hilo, nimekuandalia semina ambayo inaenda kuchoche moto wa wa wee kufanya makubwa na kuweza kufanikisha malengo yako ndani ya mwaka 2023.
Semina hii inaitwa SEMINA YA KUFANYA MAKUBWA, siyo kwa bahati mbaya, bali kwa sababu kuna maana yake.
Kwenye hii semina tunaenda kujifunza namna ambavyo unaweza kufanikisha makubwa ndani ya miezi sita, wakati wengine huwa wanafanyia kazi hayo kwa miaka mmoja mpaka miaka miwili. Unaweza kujiuliza hili linawezekanaje. Kiufupi ni kwamba linawezekana maana tumekuwa tukililifanyia kazi kwa muda sasa, kinachofuata ni kuhamishia kile ambacho tumekuwa tukikifanyia kazi kwako ili na wewe uweze kukifanyia kazi kwa muda mfupi kuliko ambavyo umekuwa ukitegemea.
Sambamba na hilo kwenye hii semina tunaenda kujifunza mambo mengine mazuri ambayo yatabadili maisha yako na mwelekeo wa maisha yako kiujumla.
Tunaenda kujifunza juu ya safari ya kuelekea uhuru wa kifedha, kwenye hii semina tutaona namna ya kuianza safari hii hatua kwa hatua, tutaona namna ya kuendedelea na hii safari na hatimaye kuhakikisha kwamba hii safari inakamilika.
Lakini siyo kwamba tutaishia hapo, tutaona namna ya kuamsha uwezo ulioala ndani yako na kuutumia kwa viwango vya juu ili uweze kufanikisha hayo yoooe ambayo tumekuambia.
Kuna watu ambao huwa wanaogopa kwamba hivi vitu, vinaweza visifanye kazi. tutaona namna ya kuondoa hofu ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako na namna ambavyo unaweza kuwa na maisha unayotaka baada ya kuwa umeondoa hiyo hofu.
Hatutaishia hapo tu kwa wale walio kwenye mahusiano, tutaona namna ambavyo mnaweza kufanikiwa kifedha mkiwa kama wenza.
Kiufupi hii semina itakuwa imejaa mengi kwa ajili yako. Na itakuwa ni semina ya siku nzima. Semina hii itaanza saa moja asubuhi na itamalizika jioni saa 12.
Tutakuwa na siku moja nzima ambapo tutjitenge na uliwewengu na kukaa kwenye mazingira ambayo tutajifunza namna ya kupindua mambo mengi kwenye maisha yetu.
Baada ya hii semina, kitakachofuata ni kuchukua hatua na kufanyia kazi yale tutakayokuwa tumejifunza.
Hivyo, sasa naomba rasmi nichukue nafasi kukukaribisha kwenye semina hii ya kipekee.
SEMINA HII ITAFANYIKA hapa morogoro,. Itafanyika siku ya jumamosi, na itakuwa ni semina ya siku nzima kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni. Chakula na bites vyote utapata kwenye hii semina.
Gharama ya semina hii itakuwa ni shilingi 50,000/-
Na mwisho wa kufanya malipo kwa ajili ya semina ni tarehe 15.6.2024
Karibu sana kwenye semina ya kufanya makubwa mwaka 2023. Mwaka 2023 haturembi mwandiko!
Kwa kumalizia ningependa kukumbusha mambo machache tu.
- Semina itafanyika tarehe 24, Juni, 2023.
- Itakuwa ni siku ya jumamosi
- Itafanyika kuanzia saa moja asubuhi mpaka jioni saa 12
- Gharama ya semina ni 50,000/-
- Chakula na bites vitakuwepo.
Cha kufanya ni wewe kuthibitisha malipo yako sasa hivi. zifuatazo ni namba ambazo zitatumika kufanya malipo ya semina.
*NMB: 22110047274 JINA NI GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA*
*Mpesa: 0755848391*
*Airtel money: 0684408755
*JINA NI GODIUS RWEYONGEZA*
Kitu cha kufanya leo.
Siku ya leo fanya kitu kimoja tu rafiki yangu.
Tuma ujumbe wa kuthibitisha ushiriki wako kwenye semina. Tuma ujumbe huu kwenda whatsap
0755848391 au bonyeza hapa
Kisha niambie, utalipia kwa mpango gani.
Utalipa kiasi chote kwa pamoja au takuwa unalipa kila wiki, au kila mwezi na kiasi gani utakuwa utakuwa unalipia?
Tuma ujumbe wako hapa
Mfano:
*Mimi GODIUS RWEYONGEZA nathibitisha kushiriki semina ya mwezi wa sita*
*Nitalipia kiasi chote kwa pamoja tarehe 15 MACHI, 2023.*
*JIUNGE NA KUNDI LA WALIOTHIBITISHA KUHUDHURIA*
Karibu sana
-
Jinsi Ya Kujenga Mafanikio Makubwa Hata Kama Hauna Kitu
Hapo zamani za kale, ili kujenga utajiri ulipaswa kuwa na ardhi kubwa, ng’ombe na vitu vingine vinavyoendana na hivyo. Ulipokuwa na vitu vya aina hiyo, hapo sasa ndipo watu walikuwa wanasema kwamba mtu fulani ni tajiri. Ila leo hii mambo yamebadilika.
Baadaye ilikuwa inaaminika kwamba ili kujenga utajiri unapaswa kuwa walau na konekisheni na ndugu au mtu ambaye ni tajiri au ambaye anafanya kazi kwenye taasisi kubwa. ila leo hii mambo hayo yote yamebadilika, huhitaji kuwa na konekisheni wala ndugu yako ambaye anafanya kazi serikalini, huhitaji kuwa fisadi, huhitaji kuwa mashamba mengi wala ng’ombe elfu. Unahitaji kutumia kile ulinacho. Na kwa sababu hiyo, siku ya leo ninaenda kuandika makala ya kina inayoeleza namna ambavyo unaweza kufanikiwa kwa viwango vikubwa hata kama hauna kitu.
Hatua ya kwanza ya kujenga mafanikio makubwa hata kama hauna kitu ni
1. KUJUA KITU UNACHOPENDA NA KUANZISHA BIASHARA KWENYE KILE UNACHOPENDA
Rafiki yangu, najua kuna vitu kadha wa kadha unapenda hivi kwako vinapaswa kuwa sehemu ya kuanzia. Haitoshi tu wewe kila siku kwenye kuangalia mechi kila siku, huku ukishangilia kwamba Mayele kafunga au hajafunga. Baala yake unapaswa kuangalia fursa iliyojicicha kwenye hicho kitu mbacho unapenda na namna ambavyo unaweza kuitumia hiyo fursa kufanya makubwa.
Ukishajua kitu ambacho unapenda, basi acha kufanya mambo mengine yoyote yale, badala yake wekeza nguvu na muda wako kwenye hicho kitu unapenda.
Jenga biashara kwenye hicho kitu. Jenga hata biashara ya kuanzia chini.
2. ANGALIA RASILIMALI ZILIZO KWENYE MAZINGIRA YAKO UNAZOWEZA KUANZA KUTUMIA SIKU YA LEO
Kuna rasilimali ambazo naamini unazo ambazo unaweza kuanza kutumia.unaweza ukawa unafikiria kufanya makubwa sana ambayo pengine hayajawahi kufanyika kwenye hii dunia, lakini unachopaswa kufahamu ni kwamba, hayo makubwa unaweza kuanza nayo kidogo kidogo na kwenda nayo hatua kwa hatua mpaka ukaweza kuyafanya kuwa makubwa zaidi.
Kuna rasilimali nyingi zimekuzunguka ambazo unahitaji kuhakikisha kwamba umezitumia. Nguvu zako, muda wako, mazingira yaliyokuzunguka na mengine mengi. Tumia hizi rasilimali kuhakikisha kwamba unafanya makubwa. Naam, makubwa sana.
TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA
3. TOA THAMANI KUBWA TENA BURE
Najua u ataka kulipwa tena kwa viwango vya juu. IlA NJIA NZURI YA wewe kuweza kulipwa ni kuanza na kile ulichonacho, ukiweza kufanyia kazi vizuri kile ulichonacho, utaweza kufanya makubwa sana. tumia kile ulichonacho kwanza.
4. JIPE MUDA
Kila kitu hakitaweza kufanyika ndani ya siku moja. unahitaji kujipa muda ili kuweza kujenga mafanikio ambayo unataka. Mafanikio makubwa hayajengwi ndani ya siku moja au wiki moja. badala yake ni kwamba yanachukua muda.
5. JIJUE MWENYEWE
Jijue mwenyewe ni vitu gani unaweza zaidi kuliko vingine. badala ya kupambana kufanya kila kitu, wekeza nguvu na muda wako kwenye vitu vichache ambavyo unaweza kuliko kufanya kila kitu bila mpangilio.
6. PAMBANA KWA BIDII
Rafiki yangu, malengo yako na ndoto zako unapaswa kuzipambania kwelikweli bila ya kurudi nyuma. Na hili hakikisha kwamba unalifanyia kazi bila ya kurudi nyuma. Kiufupi. Hakikisha kwamba kila unapoamka mpaka unapoenda kulala, unakuwa umepambana na kupambana zaidi. ukiona imepita siku bila ya kufanya kitu chochote kwenye ndoto yako. Basi ujue hiyo siku umeipoteza.
Cha kufanya pale wenzako wanapokuzidi elimu, kipaji, ujuzi konekisheni n.k.
7. TUNZA MUDA WAKO VIZURI
Muda ndiyo rasilimali pekee ambayo inaweza unayo bure na ambayo ukiipoteza unakuwa umeipoteza. Kwa hiyo basi, mara zote pambana kuhakikisha kwamba unautumia muda wako kwa uzuri na kwa weredi mkubwa kuhakikisha kwamba muda wako unakuwa wenye manufaa.
Watu wanaofanikiwa sana na wale ambao hawafanikiwi sana wana muda uleule. Tofauti kati ya wale wanaofanikiwa sana na wale ambao wanakuwa na mafanikio ya kawaida ipo kwenye matumizi ya muda. Hivyo basi, ili uweze kufanya makubwa unapaswa kuhakikisha kwamba unautumia vizuri muda wako. Anza na dakika yako moja ya sasa, kisha pangilia saa lako moja la baadaye na kisha siku yako nzima. Muda wako ni rasilimali muhimu sana ambayo unapaswa kuitumia vizuri sana.
8. PENDA MCHAKATO
Mchakato ni muhimu zaidi kuliko lengo. Watu wengi huwa wanaweka malengo mwanzoni mwa mwaka, ila malengo ni kitu kimoja. Kufanyia kazi yale malenngo ndio jambo lenyewe haswa. Na hili ndilo ambalo ningependa ulifahamu siku ya leo
9.ACHA KUJALI SANA KILE AMBACHO WENGINE WANAFIKIRIA
Najua kuna mengi sana ambayo watu wengine wanafikiria. Acha kujali sana mambo ambayo watu wengine wanafikiria. Badala yake wekeza muda wako na nguvu zako kwenye kile unachofanya tu.
soma zaidi: Vitu 21 Ambavyo Ni Lazima Kufanya Hata Kama Una Kipaji Kikubwa
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Kitu muhimu ambacho kila mtu anapswa kukifhamu
Rafiki yangu, najua kuna vitu vingi ambavyo unahitaji kufahamu. Ila siyo kila kitu unachokifahamu kina manufaa chanya kwako. kwa mfano unaweza kufahamu kuwa kuna ajali fulani sehemu fulani, ila siyo kwamba hiyo ajali ina manufaa yoyote kwako. au kwa wewe kufahamu kuwa kuna vita sehemu fulani, hilo kwa kupande wako siyo kwamba linakuwa na matokeo chanya ambayo unaweza kuyatumia.
Ila kwa upande mwingine kuna vitu ambavyo ni muhimu kwako kuvifahamu na baada ya kuvifahamu unapaswa kuhakikisha kwamba umetumia maarifa na kila kitu ulichokipata kwa manufaa zaidi. moja ya kitu ambacho wewe unahitaji kuhakikisha kwamba umekifahamu kwa undani zaidi ni THAMANI YAKO.
Karibu upate kitabu hiki cha kipekee sana. Gharama yake ni 30,000 tu Thamani ni kitu cha muhimu sana ambacho unahitaji kuhaikisha kwamba umekifanyia kazi, tena unahitaji kuhakikish kwamba unakifanyia kazi sasa hivi rafiki yangu
Ukijua thamani yako, utaokoa mengi sana rafiki yangu.
Thamani yako inakusaidia wewe kupangilia muda na kazi zako ambazo unafanya. hii ndiyo kusema kwamba badala ya kufanya vitu hovyohovyo, unakuwa unafanya vitu kwa ustaarabu na kwa utaratibu mzuri ambao umeupangilia. Kitu ambacho hujakipangilia hukifanyi.
Pili kujua thamani yako kunakusaidia kujua vitu vya kukubali kwenye maisha yako na vitu ambavyo unapaswa kukataa. Siyo kila kitu unaweza kukifanya, kuna baadhi ya vitu unaweza kuvikubali na kuamua kuvifanya kwenye maisha yako, ila kuna baadhi ya vitu unapaswa kuacha kuvifanya ili uwekeze nguvu zako na muda wako kwenye kukuza thamani yako zaidi.
Hii inakusaidia kuwekeza muda wako kwenye sehemu zenye nguvu na kuachana na sehemu ambazo hazina nguvu kwa upande wako.
Rafiki yangu kama kuna sehemu ambapo wewe unapaswa kuwekeza muda wako na nguvu zako basi ni kwenye thamani yako. Hakikisha kwamba unaijua thamani yako kw aundani.
Nimeandaa kitabu kizuri kwa ajili yako kitakachokusaidia wewe kwenye hili. Kitabu kinaitwa JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO.
Karibu sana uweze kujipatia nakala yako siku ya leo.
Kupata nakala tuwasiliane kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA
-
Wewe unapenda kitu gani?
Kati ya vitu vyote, nilipenda vitabu zaidi– Nikola Tesla
Wewe unapenda kitu gani? Nadhani hili ni swali ambalo ukiuliza kwa vijana kama sisi wa siku hizi utapata majibu ya ajabu Sana.
Kama unaweza kuvumilia *pressure,* Basi uliza hilo swali. Ila Kama una *pressure* ya haraka basi usiliuze labda Kama umechoka kula ugali. Hahaha
Nakwambia hivyo, kwa sababu majibu utakayopata kutokana na swali Hilo yatakusikitisha sana.
Mimi sitataja majibu utakayopata, hivyo kaulize mwenyewe…..
Utagundua mwanzoni nimeanza na nukuu ya Nikola Tesla ananasema Kati ya vitu vyote, vitabu ndivyo nilipenda zaidi.
Sijajua wewe upande wako vipi.
Leo nimeona nikusisitize zaidi huu ya umuhimu wa vitabu. Vitabu ni vya muhimu Sana kwenye maisha. Nakumbuka siku za nyuma niliwahi KUANDIKA kitabu kizima kinachoeleza NGUVU KUBWA iliyo kwenye Kusoma vitabu na jinsi ya kuitumia hiyo NGUVU kufanya makubwa.
Nashauri na wewe usome hiki kitabu maana kina Mambo mengi mazuri sana ndani yake ambayo yatakunufaisha na wewe. Na ubora ni kwamba unaweza kukipata bure hapa
Kwa kuwa vitabu vina Mambo mengi mazuri. Leo nataka nikwambie kwamba vitabu vina uwezo wa kukutoa kwenye ukilaza kuwa gwiji. Nikola Tesla ambaye nimeanza kwa kutoa nukuu yake hapo mwanzoni, alikuwa gwiji wa Aina yake.
Alifanya Mambo mengi mazuri kwenye ulimwengu wa ugunduzi. Ni mmoja wa watu wanaoaminika kwamba waligundua redio.
Lakini ukifuatilia nyuma yake unakuta kwamba alikuwa anapenda kusoma vitabu. Sijajua Hilo linakuwaje, Ila kila Mara ukifuatilia historia za watu waliofanya MAKUBWA, Kati ya Mambo mengi ambayo najifunza Kutoka kwa hao watu ni kusoma vitabu.
Ninapoandika hapa nipo nasoma historia ya Mkurugenzi maarufu wa kampuni GE. Jack Welch, nadhani ukitafua Google wakurugenzi Bora wa nyakati zote, Ni lazima Jina la huyu jamaa ulikute.
Lakini kinachonishangaza ni kwamba pamoja na mengine mazuri ambayo alifanya ila bado alikuwa anapenda kusoma vitabu.
Hivyo, nadhani usomaji wa vitabu, unabaki kuwa ni moja ya jambo muhimu sana kwenye ulimwengu wa leo. Yaani, unabaki kuwa ni jambo la muhimu mno.
Kati ya vitu vyote ambavyo utafanya, basi hakikisha kwamba unasoma na vitabu pia. Vitabu Ni muhimu Sana.
Tenga muda hata kama Ni kidogo kuhakikisha unasoma vitabu.
Pakua kitabu Cha bure hapa ili uweze kukisoma zaidi
Kila la kheri