Home


  • Hiki Ndicho Kitu Unachopaswa Kuwa Na Wasiwasi Nacho Kwenye Maisha Yako

    Rafiki yangu mpendwa, salaam

    Bila shaka unaendelea vizuri kabbisa. Hongera kabisa kwa siku hii nyingine ya kipekee. Leo ni Jumamosi ya tarehe 16, mwezi wa tisa mwaka 2023. Ni siku bora kabisa ambayo naamini umeweza kuitimia kwa viwango vikubwa.

    Siku ya leo kuna kitu kimoja tu ambacho ningependa kukwambia na kitu hiki syo kingine bali ni kitu ambacho unapaswa kuwa na wasiwasi nacho. Najua sana kwenye maisha yako kwamba unakuwa na wasiwasi na vitu vingi sana kwenya maisha yako. Unaweza kuwa ni wasiwasi kwamba ukianzisha biashara inaweza kufa. Au wasiwasi kwamba ukiongea na mtu fulani kuhusiana na jambo lako anaweza kukukatalia.

    Imethibitishwa mara kwa mara kwamba vitu vingia ambavyo watu huwa wanaogopa, huwa havitokei kwenye uhalisia. Karibia asilimia 90 na zaidi uya vitu unavyoogopa havitakuja kutokea na vingine unavyoogopa havipo kabisa.

    Hivyo, linapokuja suuala zima la kuogopa linakuwa halina maana. Kitu pekee unachopaswa kuogopa ni kile ambacho kinakuwekea wewe ukomo wa kutumia uwezo wako.

    Kulinganisha na vile tunavyopoapswa kuwa, alisema Dr. James Wiliiam, watu bado wameamka nusu.

    Hii ndiyo kusema mimi na wewe tuna uwezo mkubwa sana ambao hata hatuutumii. Unapaswa kuanza kujisukuma mara moja kuutumia uwezo wako uliolala ndani yako.

    Kama watu waliofanya makubwa mpaka sasa hivi wametumia asilimia chini ya kumi. Watu kama akina Steve Jobs ambao wamegudua vifaa vya kompyuta na simu janja ambazo tunazitumia leo hii. Au watu kama albert Einstein ambao ni maarufu kwenye ulimwengu wa fizikia. Kama hawawa tu wametumia uwezo chini ya asilimia kumi tu na siyo zaidi ya hapo, je, unadhani wewe umetumia uwezo kwa viwango gani. Ukweli ni kwamba unaweza ukawa haujatumia uwezo wako zaidi ya asilimia kumi.

    Kwa hiyo basi, kama hujatumia uwezo wako kwa zaidi ya asilimia kumi halafu hapa njiani kinatokea kitu ambacho kinazuia uwezo wako, maana yake, unaenda kukwama zaidi ya hapo. Unachopaswa kufanya sasa hivi ni kuhakikisha kwamba  umeondoa kikwazo chochote kile ambacho kinakuzuia wewe kuweza kutumia uwezo wako kwa viwango viikubwa. Badala yake unapaswa kuweka mazingira ambayo yanakuruhusu wewe kuweza kutumia uwezo wako kwa viwago vya hali ya juu kabisa, hivyo, basi ni jukumu lako kuanzia leo hii kuhakikisha kwamba upo kwenye mazingira ambayo yanakuruhusu wewe kuweza kutumia uwezo wako kwa viwango vya hali ya juu kabisa.

    Swali muhimu unalopaswa kujiuliza siku ya leo ni je, nipo kwenye mazingira mazuri ya kutumia uwezo wangu kwa viwango vya hali ya juu. Je, mazingira haya yanaruhusu mimi kuweza kutumia uwezo wangu kwa viwango vya hali ya juu. Kama mazingira yako hayaruhusu wewe kuweza kutumia uwezo wako kwa viwango vya hali ya juu basi ni muda sasa wa kubadili hayo mazingira, na kama huwezi kubadili hayo mazingira basi unachopaswa kufanya ni kuhama kwenye hayo mazingira ili uweze kukaa kwenye mazingira ambayo yanakusapoti wewe kuweza kutumia uwezo wako kwa viwango vya hali ya juu.

    Rafiki yangu labda tu nikwambie kitu. Utakaopokuwa umefikia umri wa uzee. Utakachojutia siyo wewe kutumia uwezo wako kwa viwangao vya hali ya juu. Bali utajutia kwamba hukuweza kutumia uwezo wako kwa viwango vya hali ya juu. Ndiyo maana leo hii ni kazi yako ni kuhakikisha kwamba umeutumia uwezo wako.

    Sitaki siku moja ujutie kwamba hukuweza kutumia uwezo wako kwa viwango vya hali ya juu. M uda mzuri wa kutumia uwezo wako kwa viwango vya hali ya juu ulikuwa ni pale ulipopata akili. Ila muda mwingine mzuri zaidi ni sasa. Kwa hiyo, kama ulikuw abado huijaanz akutujia uwezo wako kwa viwango vikubwa, muda ni sasa. Anza kuutumia huwezo wqako huu kwa viwango vikubwa.

    Na ukweli ni kwamba unapotumia uwezo wako siyo kwamba unakuwa unawanufaisha watu wengine tu. Bali wewe pia unakuwa unazidi kunufaika zaidi.

    Uwezo tulionao ni kama misuli, kadiri unavyokuwa unautumia  uwezo wako ndivyo unakuwa unazidi kuimarika zaidi na zaidi na kuongezeka. Kama ilivyo kwa misuli, kadiri unavyofanya mazoezi, ndivyo misuli yako inavyozidi kuimarika na kuwa bora zaidi. Kwa hiyo, kazi yako kubwa kwa sasa ni kuhakikisha kwamba unautumia uwezo wako.

    Lakini pia kutumia uwezo wako kunakupa ridhiko la moyo. Yaani, unakuwa unafanya kitu roho inapenda, wakati huohuo unakuwa na utulivu wa moyo na akili,. Hivi kwa mfano utajisikiaje kama wewe utakuwa mmoa wa watu ambao wameutumia uwezo wao  vizuri na wana ridhiko kuuubwa la motyo na akili? Ni wazi kuw autajisikia vizuri sana. Kwa hiyo basi rafiki yangu, hakikisha kwamba unaanza kuutumia uwezo wako mara rmoja.

    Kitu kingine kuhusu kuutumia uwezo wako ni kwamba unakuwa mbunifu. Kadiri unavyoutumia uwezo wako ndiyo unavyozidi kuwa mbunifu zaidi na zaidi.

    Na kitu kingine muhimu sana kuhusu kuutumia uwezo wako ni kwamba, inakupa nafasi ya kuwasaidia wengine kutumia uwezo wao pia. Maaana kuna wau wataona namna unavyotumia uwezo kwako, na watu hao watakuywa tayari kujifunza na kutaka kujua ni kwa namna gani ambavyo wanaweza kutumia uwezo wao pia. Sasa kwa jinsi hiyo, utaweza kuwasaidia  kwa kuwaabia kwamba mnaweza kutumia uwezo mlionao kwa viwango vikubwa kwa kufanyamambo yafuatayo.

    Kish utawaorodheshea mambo yote ambayo wanapaswa kufanya ili kuweza kutumia uwezo wao.lakini pia kwa uwa umeshafanyia uwezo wako kwa viwango vikubwa, utakuw unajua kila kitu ambacho wanapaswa kufanyia kazi ili kuweza kuutumia uwezo wao kwa viwango vya hali ya juu sana.

    Hivyo rafiki yangu, kazi yako ni moja tu. Ni kuhakikisha kwamba umeutumia uwezo wako. Kwa sababu utakuwa mtu mwenye faida pale tu ambapo utaaamua kuuutmia uwezo wako kuliko pale ambapo utakuwa hujaweza kutumia uwezo wako.

    Hayo ndiyoambayo nilitaka kukushirikisha siku ya leo rafiki yangu wa  ukweli. Naamini sana leo umewezaakundondooka na kitu kikubwa sana kwenye makaal hii.

    Nikutakie wikendi njema kabisa.

    kabla hujamalizia kusoma makala hii nakuomba kitu kimoja tu. Na kitu hiki ni kwamba uwashirikishe wenzako makala hii ili nao waweze kuisoma na kunufaika nayo.

    Asante sana.

    Makala hii imeandikwa name rafiki yako

    Godius Rweyongeza

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwangu kwa kupatanakala za vitabu vyangu. Na vitabu vyangu unawezakuvipata mtandaoni kupitia hapa

    Au unaweza kuwasiliana na 0684408755 sasa ili uweze kupata nakala zako

    Asante sana na uwe na siku njema.

  • Cha kufanya kama unaanzia chini kweye maisha

    Rafiki mpendwa salaam, bila shaka unaendele vizuri kabisa. Hongera kwa kazi. Mimi naendelea vizuri nikiwa hapa Morogoro mji kasoro bahari.

    Siku ya leo nataka nikwambie kitu kimoja ambacho unapaswa kufanya kama unaanzia chini kwenye maisha. Unajua ni kitu gani hiki.

    Kwanza ni kuchagua kitu ambacho utafanya. Hiki ni muhimu sana, watu wengi huwa hawapati nafasi ya kufanya kitu kama hiki. Huwa wanajikuta kwamba wanafanya kila kitu kwenye maisha yao. Wewe haupaswi kuwa mtu wa aina hiyo. Chagua kitu kimoja ambacho utaamua kukifanya kwa viwango tena vya juu  sana bila kujali nini kinatokea kwenywe maisha yako.

    Baada ya kuchagua hikl kitu kimoja, weka nguvu zako zote kwenye hiki kitu.

    Jifunze kuhusu hiki kitu. Ni kweli unaweza kufanya mambo mengi, lakini jipe nafasi ya kukua na kufanya jambo moja kwa undani na kwa uwezo wa hali ya juu sana. Kwa hiyo, usihangaike na kila kitu.

    Hili jambo ninalokwambia hapa unaweza kulichukulia poa sana. Lakini jambo hilihili ndilo litakalokuwezesha kulipwa zaidi kwa hapo baadaye. Maana kama utachagua jambo moja, na jambo hili ukaamua kujifunza na kuliewa kwa undani na kuhakikisha kwamba umelielewa kuliko mtu mwingine yoyote. Lakini pia ukaenda mbali zaidi na kuhakikisha kwamba hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kulifanya zaidi ya wewe maana yake utaweza kulipwa zaidi ya mtu mwingine yeoyote Yule ambaye amekuzunguka kwenye jamii yako.

    kinachoponza wengi ni kwamba huwa wanahangaika na mamb mengi kwenye maisha yao, kiasi kwamba huwa wanashindwa kufanikisha jambo moja kwa viwango vikubwa sana. Wewe haupaswi kuwa mtu wa aina hiyo, badala yake unapaswa kuwa mtu ambaye unaweka nguvu zako kwenye jambo moja na unahakikisha kwamba hilo jambo llinafanikiwa kwa viwango vikubwa sana.

    Kitu kingine cha muhimu ambacho unapaswa kufahamu ni kuwa ili uweze kufanikisha jambo la aina hii unapaswa kuhakikisha kwamba unafanya jambo ambalo umechagua kila siku bila kuacha. Kama siyo kila siku basi ufanye hilo jambo mara kwa mara

    Kwa mfano kama umechagua kuandika makala kama hizi unapaswa kuwa unafanya hivyo kila siku bila ya kujali n ikitu gani amabcho kinatokea kwenye maisha yako. Kitu hiki kitakuwezesha kujenga nidhamu kwenye uandishi lakini pia kitakupa nidhamu ya kuwa unajifunza kila siku ili uweze kupata kitu cha kuandika. Maana huwezi tu kulala na kuamka na kuandika bila ya maandalizi.

    Lakini pia kitu kama hiki kitakufanya ubobee kwenye uandishi kuliko mtu mwingine yeyote ambaye amekuzunguka. Kwa hiyo anza kulifanyia kazi hilo.

    Kama umechagua kuweka akiba, inaweza kuwa kila siku kama kipato chako kinaingia kila siku. Lakini kama kipato chako kinaingia kila wiki, basi unaweza weka akiba kila wiiki bila ya kucha.

    Na endapo kipato chako kinaingia kila mwezi basi unaweza kuweka akiba kila mwezi bila ya kcuaha. Kitu hiki kitakufanya urudie kufanya kitu kile kile kila mara na mwisho wa siku utajikuta kwamba umebobea na kufanya jambo hilo liwe tabia yako.

    Kama umechagua kuwekeza, mfano kwenye soko la hisa, unaweza kuwa unawekeza kila wiki, au kila mwezi. Kuwekeza kwenye soko la hisa ni vigumu kufanya hivyo kila siku, lakini unaweza kufanya hivyo kila siku za wiki, yaani jumatatu mpaka ijumaa, maana soko la hisa huwa halifunguliwi jumamosi na jumapili.

    Lakini kama unanunua vipande kwenye mifuko ya vipande kama utt na faida fund ya whi basi unaweza kuwa unanunua kila siku, bila ya kuacha.

    Kama ni mazoezi unaweza kufanya kila siku kwa dakika kadhaa.

    Ni muhimu sana kurudia kufanya jambo na kulifanya kila mara bila ya kuacha.

    Hiki kitu kitakufanya uweze kubobea kwenye hilo jambo na uweze kulifanya kwa weredi wa halil ya juu sana.

    Kwa hiyo kama unaanzia chini kumbuka kufanya yafutayo.

    Kwanza kuchagua jambo moja la kufanya

    Pili lifanye jambo hilo kila mara au kila siku na kwa kurudia rudia bila kuacha na kwa nidhamu kali sana

    Mwisho wa siku vitu hivi vidogovidogo unavyofanya utakuta kwamba vimekua na kuwa vikubwa. Ni jukumu lako sasa kuhakikisha kwamba umefanya hivyo.

    Mwanzoni matokeo yanaweza yasionekane, lakini kadiri unavyoendelea kufanya bila ya kucha kwa muda mrefu utajikuta kwamba umeweza kufanya jambo hilo kwa viwango vikubwa sana.

    Unapokuwa unaanzia chini, unakuwa hauna kitu. Ni nidhamu yako ndiyo itakayokuweka kwenye ramani, bila ya nidhamu utaishia kubaki hukohuko ulipo chini.

    Ndiyo maana tangu mwanzoni nimekwambia kwamba kama unachagua kufanya jambo unapaswa kulifanya kwa kulirudia rudia mara kwa mara, bila ya kuchooka na bila yakurudi njyuma. Nadhani hapo umenielewa vizuri sana rafiki yangu.

    KAMA MAMBO NI RAHISI HIVI KWA NINI WATUWENGI HUWA HAWAFANYI.

    Vitu vya kujirudiarudia huwa havipendwi sana na watu. Watu huwa wanapenda vitu vipya. Na akili zetu ziko  hivyo, zinapenda kuona kitu kipya kila mara, hivyo vinapofanya kitu mara ya kwanza na mara ya pili zinaanza kuzoea kitu hicho. Na mwisho wa siku kitu hichocho kinaanza kuchukuliwa poa.

    Kwa mfano, mtu anaanza kuweka akiba mwanzoni. Lakini anakosa uendelevu, kumbe ule mwendelezo wa kile kitu ndiyo utakaokusabibishia wewe uweze kufiikia mafanakio makubwa na siyo kufanya mambo mengi ya tofautitofauti kwa nyakati tofauti tofauti. Hivyo, kazi yako kubwa na jukumu lako kubwa ni kuhakikisha kwamba ukishajua vitu sahihi vya kufanya, basi vitu hivyo unavifanya kwa msimamo bila ya kuacha kwa muda mrefu.

    Kwa mfano leo umejua kwamba ni muhimus ana kwako kuweka akiba akiba. Hili jambo usilifanye tu kwa siku moja kwa sababu unataka ulifanye kwa siku hiyo, badala yake lifanye kwa mwendezo na siku nyingi zinazo bila ya kuacha. Ni mwendelezo tu ndiyo utakaokupa matokeo. Kumbe badala ya kufanya hilo jambo na kuacha na kutafuta jingine. Lifanye hilohillo moja kwa mwenzelezo na kwa muda mrefu bila ya kuacha. Hiki kitu kitakupa matokeo makubwa sana rafiki yangu ambayo hata hapo mwanzoni wewe mwenyewe ulikuwa hutarajiii.

    Ningependa kusikia kutoka kwako siku ya leo ni kitu gani aambacho umechagua kufanya kwa msimamo na kwa muda mrefu bila ya kuacha.

    Naksuahauri, zaidi usome kitabu cha NGUVU YAKUCHUKUA HATUA YA KWANZA: Na Kwa Nini Unapaswa Kumaliza Kile Ulichoanza. KWENYE HIKI kitabu nimeelza kwa undani kwa namna gani uanapaswa kuanza kufanyia kazi vitu ambavyo unapenda kufanyia kazi bila ya kucha , lakini pia niemeelza kwa undani ni kwa namna gani unapaswa kuendeleza kile ambacho tayari umeanza kukifanyia kazi.

    Kitabu hiki unaweza kukipata mtandao ni hapa

    Hardcopy ni 25,000 unaweza kuipata kwa kulipia 25,000/-. Lipia kwenda namba ya simu 0684408755. Ukishalipia tuma taarifa zako ili utumiwe kitabu popote pale ulipo. NB: Gharama za kusafirisha ni juu yako.

    Ukishalipia utanitumia jina lako ili niweze kukutumia kitabu jhiki.

    Kila la kheri

    Makala hii imeandikwa nami rafiki yako wa ukweli

    GODIUS RWEYONGEZA, unaweza kuwasiliana nami kwa namba ya simu ambayo ni 0755848391

    barua pepe ni godiusrweyongeza1@gmail.com

    Kupata vitabu vyangu vyote wasiliana na 0684408755 sasa au BONYEZA HAPA kuvipata kwa njia ya mtandao.

    Asante sana na karibu sana.

  • Vyanzo Vingi vya KIPATO ni kama miguu ya Meza.

    Vyanzo Vingi vya KIPATO ni kama miguu ya Meza. Meza iliwa na mguu mmoja na mguu huo ukavunjika. Maana yake Meza hiyo kwishney!!

    Ila Meza iliwa na miguu minne, Mmoja ukivunjika. Itatetereka kidogo, ila Bado itakuwa imesimama.

    Kama ambavyo nimekuwa nakwambia, kama hauna vyanzo vingi vya vipato. Basi utakuwa na Vyanzo Vingi vya mahangaiko. Kuwa na Vyanzo Vingi vinavyokuingizia maokoto.

    Nina kitabu KIZURI Kwa ajili yako.Unaweza kukipata Kwa 10,000/- tu

    Kitabu kinaitwa VYANZO VINGI VYA KIPATO

    Kipate hiki Leo Hii. UTANISHUKURU Kwa hatua utakayokuwa umechukua.

    Gharama ya kitabu ni 10,000/-. Ni softcocpy. Hardcopy ni 15,000/-

    Kukipata ni rahisi tu. Unalipia Kwa 0684408755 Jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    CHANGAMKA SASA

  • Tabia za kimasikini unazopaswa kuachana nazo sasa hivi.

    Rafiki yangu mpendwa salaam, leo ningependa kukwambia tabia za kimasikini ambazo unapaswa kuachana nazo. Achana na tabia hizi kwa manufaa yako.

    Kwanza ni vitu ambavyo vinapoteza nguvu zako. Hivi ni vitu vyote ambavyo vinapoteza nguvu zako vitu kama pombe, sigara, ulevi wa aina yoyote, kula vyakula vya hovyo na mambo mengine kama hayo.

    Pili, ni tabia ya kutumia kiasi kikubwa kuliko unavyoingiza. Hii ni tabi anyingine ambayo inaenda kukuanya wewe kuwa maskini maisha yako yote. Ibadili tabia hii kwa kujiwekea tabia ya kuwekeza, kuanzia leo hii.

    Tatu, tabia ya kuwa tagemezi. Kumbuka kwamba maisha ni wajibu wako. Ukishinda ni juu yako na ukishindwa ni juu yako. Hivyo, beba jukumu la maisha yako.

    Nne,  ni tabia ya kuzembea kazi. Achana kabisa na tabia ya kuzembea kazi yako, anzak uchapa kazi yako kwa bidii kubwa. na

    Tano, ni tabia ya kutojiongeza. Maskini wengi wanasubiri waambiwe cha kufanya ndiyo wafanye. na hata baada ya kuambiwa hawafanyi kama wanavyopaswa kufanya, ni mpaka wasimamiwe ndiyo wanafanya. Akitoka msimamizi, basi wao wanaanza kuzembea. wewe usiwe mmoja wao, penda kuchapa kazi tena kwa bidii hata kama hakuna mtu wa kukusimamia.

    Kwenye kitabu cha MAAJABU YA KUWEKA AKIBA nimeeleza tofauti 50 kati ya matajiri na masikini. Hakikisha unapata kitabu hiki kwa manufaa yako. softcopy ni 10,000 tu. kukipata wasiliana na 0684408755

    Karibu sana

  • Ukiuza vitabu vyako vyote ambavyo umewahi kununua utapata shilingi ngapi?

    Leo kuna mtu nilikuwa naongea naye, akaniambia vitabu ambavyo nimewahi kununua, nikiviuza vyote naweza kujenga nyumba kubwa ya kifahari.

    Hiki kitu kikawa kinanitafakarisha kuhusu wewe …

    Hivi wewe ukiuza VITABU vyote ambavyo umewahi kununua unaweza kufanya nini?

    Vitabu vinakufanya uone mbali hata wewe ni mfupi?

    Kila mwezi jiwekee utaratibu wa kununua walau kitabu kimoja tu. Kisha kisome hicho kitabu, ninakuhakikishia baada ya mwaka utakuwa umeweza kufanya makubwa sana.

    Vitabu unavyosoma vitatuonesha aina ya mtu wa siku zijazo. Ndiyo maana, Charles Tremendous Jones alisema kwamba miaka mitano ijayo utakuwa jinsi ulivyo, isipokuwa kwa vitu viwili tu. Vitabu unavyosoma na watu unaokutana nao.

    Jiwekee utaratibu wa kununua na kusoma vitabu vizuri.
    Ukikutana na kitabu kizuri kirudie kukisoma mara kwa mara bila kuchoka.

    Kisha kitumie kitabu kwa kufanyia kazi kile unachojifunza.

  • Siri ya mafanikio ya kweli ni hii hapa

    Usiache kufanya jambo lako kwa sababu huoni matokeo ya muda mfupi. Badala yake kaza. Endelea kupambana kwa muda mrefu

    Kuna watu wengi hawafanikiwi kwenye maisha kwa sababu ya kujaribu vitu vingi kwa muda mfupi na kuacha.

    Sikiliza chagua kitu kimoja
    Kifanye kwa uhakika
    Kifanye kwa muda mrefu bila kuacha.
    Bobea kwenye hicho kiasi kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kufanya kitu hicho kwa ubora kama wewe

    Kinyume chake kitakufanya ufeli.
    Kama
    Utafanya kila kitu.
    Ukakifanya kwa mguu mmoja ndani na mwingine nje.
    Ukafanya kwa muda mfupi na kuacha na kwenda kufanya mengine na yenyewe ukayafanya kwa muda mfupi mfupi huku ukiacha.
    Ukayafanya bila ufanisi.

    Mwisho wa siku utaishia kuwa na maisha ya kawaida. Na haya ndiyo maisha ya watu wengi.

    Nakwambia ufanye kitu kimoja kwa muda mrefu nikiwa na sababu za msingi kabisa.
    Moja ya sababu hizo ni kwamba kuna watu ambao mwanzoni wanakuwa wanakufuatilua, japo kwenye kukufuatilia kwao hawachukui hatua.

    Ni kama wanakuwa wanaangalia kama unabeep au unafanya kweli. Na pale unapothubitisha bila shaka kuwa umedhamiria kufanya ulichochagua, basi huwa wanaanza kukufuatilia kwa ukaribu na hata kuwa wateja wako

    Mtu anaweza kukupuuza mara ya kwanza.
    Mtu anaweza kukupuuza mara mbili ila hawezi kukupuuza mara zote.

    Huvyo, kuendelea kwako ndiyo njia pekee itakayokufikisha kule unapotaka

  • Kauli Yenye Nguvu: Ni bora Ufe Ukiwa unafanya unachopenda…

    Rafiki yangu mpedwa salaam, hongera sana kwa siku hiii ya leo. Siku ya leo ningependa tu kukushirikisha kauli moja ambayo unapaswa kuwa unajiambia kila siku kwenye biashara na kwenye kitu chochote kile unachofanya.

    Mara nyingi ukianza kufanya kazi au kitu chochote huwa wanatokea watu ambao wanakuwa na maoni ya kukushauri juu ya nini cha kufanya au nini ambacho haupaswi kufanya. Sasa kitu hiki kitakufanya usikilize miluzi mingi ambayo mwisho wa siku hiyo miluzi itakupoteza. Sasa ili kwenda vizuri nashauri kitu kimoja kwako

    Na kitu hiki ni kwamba ni bora nife nikiwa nafanya kile ambacho ninapenda kuliko kufanya kile ambacho ninapangiwa na watu wengine. Hivyo, basi fanya kile ambacho wewe wenyewe unapenda na siyo kile ambacho watu wengine wanakupangia kufanya.

    Ni bora ufe ukiwa unafanya kile ambacho wewe mwenyewe unapenda kuliko kufanya kile ambacho watu wengine wamekupangia kufanya.

    Nakutakia siku njema sana

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Unaweza kuwasiliana na mwandishi wa makala hii kwa simu 0755848391

    Kupata vitabu vyake, unaweza kuwasiliana naye kwa 0684408755

    Karibu sana

  • Kheri ya MWEZI WA SEPTEMBA

    Siku zinaenda balaa, ni kama jana tu nakumbuka watu walivyokesha wakiusubiri mwaka mpya. Watu walivyokuwa na mbwembwe za mwaka mpya na mambo mapya, hivi kwenu haya mambo yapo, au ni ushamba wa huku nilipo tu!

    Tafiti nyingi zinaonesha kwamba watu wengi ambao huwa wanaweka malengo. Huwa wanayasahau malengo yao kufikia januari 19, je, wewe malengo yako bado unayakumbuka?

    Katika ujumbe wangu wa kukutakia  kheri ya mwezi mpya siku ya leo,. Napenda pia kukumbusha kuwa tumebaki na siku 120 mwaka huu uishe.

    Hizi siku 120 usizichukulie poa na wala usianze kusema kwamba, ngoja mwaka huu uishe najipanga kwa ajili ya mwakani. Ukweli ni kwamba mwaka huu bado unapaswa kufanya makubwa. Siku 120 zilizobaki ni nyingi sana. Anza kujituma ndani ya hizi siku 120 kuhakikisha kwamba kila siku unafanya kitu cha tofauti.  Chagua kitu kimoja, kisha jisukume kufanya hiki kitu kwa siku 120 zijazo bila ya kurudi nyuma. Ukiweza kufanya kitu kimoja kwa siku 120 zijazo ni wazi kuwa kwanza utajijengea nidhamu, lakini pia kuna kitu ambacho utaweza kufanikisha ndani ya huu mwaka ambacho miakamingi ijayo utajivunia sana.

    Siku 120 ni sawa na mhura mmoja wa chuo kikuu. Ndani ya mhura mmoja mwanachuo anatarajiwa kuwa ameelewa mada ambazo zinafundishwa kwa undani.

    Na mhula mmoja ni kipimo kinachotumika kumpima mwanachuo kuona uelewa wake.

    Wewe pia jipe huu mhula mmoja wa chuo kupambana.

    Mhura wa kufanyia kazi malengo yako hata kama ulikuwa uliyaweka pembeni au ulitulia. Unataka kuandika kitabu, una mhura huu mmoja wa kufanya hivyo.

    Unataka kuongeza kipato chako, una mhura huu mmoja wa kufanya hivyo.

    Unataka kuweka akiba, utumie mhura huu kuweka akiba bila yakuacha

    Unataka kujiondoa kwenye dimbwi la mawazo na sonona inayokusumbnua, una siku 120 za kufanya hivyo.

    Ndani y a hii miezi minne zima kila kitu ambacho hakiendani na lengo lako kuu, kisha juhudi zako zote ziwekeze kwenye lango lako kuu. Kamwe rafiki yangu usikubali kurudi nyuma wala kuyumbandani ya hiki kipindi, huu ni muda wako wa kung’aa. Hakikisha unautumia kung’aa kweli.

    Kama unataka usimamizi wa karibu ndani ya hiki kipindi cha siku 120 zijazo, njoo kikashani nitakusaidia kukushika mkono ili ufanyie kazi lengo lakompaka lifanikiwe. Namba ya kuwasilialina nami ni 0755848391

  • Kazi inayolipa kuliko zote duniani. Jifunze kazi hii utaishi kama mfalme

    Rafiki yangu wa ukweli, bila shaka unaendele vizuri, siku ya leo ningependa kuleta kwako kazi ambayo inalipa kuliko zote hapa duniani. Na kazi hii siyo nyingine bali ni kazi ya kuuza.

    Ni kazi ambayo mtu yeyote ambaye yuko tayari kujifunza anaweza kujifunza. Haina ukomo wa kipato. Unaweza kupata zaidi kadiri unavyouza. Ukiuza zaidi unalipwa zaidi.

    Kitu kikubwa unachohitajhi ni kuwa na bidhaa sahihi na kuiuza kwa watu sahihi. Ni hilo tu. Hakuna zaidi ya hapo.

    Hata kama hauna bidhaa unaweza kuungana na watu wenye bidhaa na kuanza kuuza moja kwa moja. Je, na wewe ungependa kuwa supasta kwenye maisha yako. Basi anza kujifunza mauzo.

    Vitabu viwili unavyoweza kuanza navyo kwenye kujifunza mauzo ni

    Kitabu cha Pschology of selling cha Brian Tracy na

    How I raised myself from failure to success in selling.

    Vitabu hivi vyote viwili unaweza kuvipata kwa njia ya mtandao na kuanza kujifunza kuhusu mauzo mara moja

    Makala hii imeandikwa na Godius Rwqeyongeza. Kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza

    Tafadhali Wasiliana naye kwa songambele.smb@gmail.com

    0755848391

    Morogoro-tz

  • AKILI YA MKULIMA: mambo 12 ya kujifunza kutoka kwa mkulima unayopaswa kuyatumia kwenye maisha yako ya kila siku

    Hata kama wewe siyo mkulima, hakikisha unasoma vizuri makala ya leo.

    MARA KWA MARA UTASIKIA watu mbalimbali wakisema kwamba ,mimi nimezaliwa kwenye familia ya wakulima. Mimi ni mtoto wa mkulima. Ila wanavyokuwa wanaishi maisha yao inakuwa ni kinyume na masomo ambayo tunajifunza kwa wakulima. Kama wewe ni mtoto wa mkulima, ni wazi kuwa kuna mengi ambayo unaweza kujifunza kutoka kwenye familia ya kikulima ambayo unaweza kuyatumia kwenye maisha ya kila siku.

    Kitu cha kwanza kabisa cha kujifunza kutoka kwa mkulima ni akili ya kutunza mbegu. Hakuna mkulima yeyote ambaye huwa anakula mbegu yote baada ya mavuno. Mkulima makini, baada ya mavuno, hata kama amepata mavuno ambayo hayatoshelezi, bado atatoa mbegu za kupanda mwakani. Anajua wazi kuwa akila mpaka mbegu, mwakani hatakuwa na kitu cha kupanda na kama hataweza kupanda basi maana yake kutakuwa hakuna mavuno.

    Hii ni akili makini sana ambayo na wewe mwenyewe unapaswa kuwa nayo na unapaswa kuitumia kwenye maisha yako.

    Inawezekana wewe siyo mkulima. Na inawezekana chanzo chako cha kipato hakitoki kwenye kilimo kama ilivyo kwa wakulima wengine, ila hii akili ya mkulima haupaswi kuiacha. Unapaswa kuambatana nayo popote pale utakapokuwa.

    Kwa kila kiasi cha fedha ambacho utapokea mkononi mwako, kitu cha kwanza kabisa ambacho unapaswa kufanyia kazi ni kutoa mbegu. Fedha yoyote ile ambayo unatoa na kuweka akiba ni mbegu ambayo unaiandaa kwa ajill ya kuja kuipanda mwaka unaofuata.

    Mkulima huwa anajua wazi kuwa mbegu hata kama ni kidogo, akiipanda mwisho wa siku atapata mavuno ambayo ni zaidi ya zile mbegu. Kama ameweka mbegu debe moja, akipanda hilo debe moja, hatapata tena tena debe moja. Badala yake atapata atapata magunia!

    Na wewe linapokuja kwenye suala la fedha yako, haupaswi kula mbegu, badala yake unapaswa kupanda mbegu, ili uweze kula mavuno yanayotokana na mbegu.kwenye kitabu cha tajiri wa babeli kuna somo moja kubwa sana ambalo binafsi niliondoka nalo. Ni baada ya jamaa mmoja kwenye kitabu ambaye anafahamika kama Bansir kuomba ushauri kwa tajiri aliyekuja Babeli kutoka mji mwingine. Tajiri alimwambia kitu kimoja tu, kuwa kwa kila kipato ambacho unaingiza kwenye mfuko wako, kitu cha kwanza kabisa ambacho unapaswa kufanya ni kuweka akiba.

    Bansir aliufuata huu ushauri, baaada ya mwaka mmoja alikuwa amepata kiasi cha kutosha kiasi kwamba litumia kiasi hicho kwenye kununua  punda. Tajiri alipokuja alimwambia kwamba, umekosea. Kitu cha kwanza kwako kufanya hakikupaswa kuwa kununua punda, maana kwa kufanya hivyo, maana yake unakuwa unakula mbegu za matunda yako. Wewe unachopaswa kufanya ni kutunza akiba yako na kuiwekeza ili uwekezaji huu uweze kukuletea mpaka wajukuu na vitukuu. Ni kutokea hapo sasa ndipo utakuwa unaruhusiwa kula wajukuu na vitukuu vyako. hii ni sawa na mkulima ambaye kwake

    Mbegu ya kupandwa kwa mkulima huwa ni kipaumbele na tena huwa inatolewa ikiwa ya kwanza kabla ya matumizi mengine. Tena huwa inatolewa mbegu ambayo ni bora kabisa kuliko nyingine zote. Hakuna mkulima ambaye huwa anatunza mbegu iliyoharibika. Mbegu ambayo huwa inatunzwa ni ile ambayo ni bora kabisa. Hili pia litufundishe kuwa AKIBA, inapaswa kuwa ni kipaumbele cha kwanza. Siyo upate fedha na utumie yote mpaka iishe halafu ndiyo uje ukumbuke kuweka akiba, badala yake ni kwamba unapaswa kuweka akiba kwanza  halafu mambo mengine yatafuata baadaye.

    uwe na siku njema.

X