Category: TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA

  • Inawezekana Kuinuka Tena Baada Ya Kuanguka

    Kama hujawahi kuanguka maana yake hujawahi hata kujaribu. Ila kama umewahi kufanya au hata kujaribu basi unajua wazi kuwa kuna changamoto na vikwazo ambavyo huwa vipo katika safari yoyote ya kimafanikio. Muda mwingine katika safari kama hii unakuta umeanguka. Hata hivyo, ninachopenda kukwambia ni kuwa unapaswa kuinuka hata baada ya kuanguka. Ukianguka 1. Jiulize kitu…

  • Hatimaye Leo Nimemnasa Aliyesema Hakuna Haraka Barani Afrika

    KWA siku sasa nimekuwa nikijiuliza, hivi ni mtu gani aliyesema kuwa hakuna haraka barani Afrika. Leo hii  tarehe 12.4.2020 ndio nimemgundua huyu mtu aliyesema huu usemi. Najua unajua kuwa usemi huu ndio ule usemi ambao, watu wengi huwa wanautumia kama kisingizio cha kuchelewa. mambo ya maana. Usemi huu ndio umepelekea mpaka watu wengine kuamini kuwa…

  • Huu Ndio Mfumo Bora Utakaokuwezesha Wewe Kutimiza Malengo Yako. mfumo huu haujawahi kufeli hata kidogo

     HIVI IMEWAHI KUKUTOKEA, ukiwa kwenye chumba ambapo kuna  kelele nyingi za watu na unaongea na marafiki ila ghafla ukasikia sehemu mtu anataja jina lako. Yaani watu waliokuwa pembeni kidogo wanaonge mwanzoni na ulikuwa hujawasikia wanachoongea muda wote, ila zamu hii tu mtu kataja jina lako, basi masikio yako yameshanasa kila kitu. Hivi ni kitu gani…

  • Washindi Huwa Wanafanya Hivi Baada Ya Changamoto

    Mara nyingi unapoanza kufanya kitu mwanzoni matokeo mrejesho wake huwa ni mdogo sana. Kwa mfano unaweza kuanzisha biashara ukiwa na timu kubwa ya watu ambao wako nyuma yako na wanakuahidi kununua ila baada ya kuanzisha biashara ukawa huwaoni watu hao kwenye biashara. Au pengine unaweza kuanzisha biashara ukitemgemea kupata mwitikio mkubwa wa wateja kuanzia siku…

  • Kubali Kulipa Gharama Ili Uzifikie Ndoto zako

    LIPA GHARAMA Ili kweza kufikia mafanikio makubwa kwenye kutimiza ndoto zako basi moja ya kitu ambacho utapaswa kufanya ni kulipa gharama. Hii haijalishi kwamba wewe ni ndoto yako ni kuwa baba bora au mama  bora, au iwe ni kufikia viwango vya juu katika mchezo fulani. Kwa vyovyote vile gharama bado haitaepukiki Na hapa ninapozungumzia gharama…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA tatizo unamwibia Petro Kumlipa Paulo

    Kuna misemo mingi sana ya wahenga na kila usemi huwa unakuta umebeba ujumbe fulani. Sasa leo hii tunakutana na usemi unaosema, “unamwibia Petro kumlipa Paulo”.Katika maisha kuna vitu unafanya ambavyo kwa hakika ni vya kumwibia Petro ili Kumlipa Paulo.Mfano umeishiwa na hela na unachokimbilia kufanya ni kukopa. Hapa unakuwa unakimbilia kuzima moto kwa haraka haraka…

  • Makala Maalum Kwa Watu Wenye Mpango Wa Kuomba Kazi Au Wanaoomba Kazi Sasa Hivi

    Moja ya mbinu ambayo imezoeleka kwenye kuomba ni kuandika CV na kuituma kwa mwajiri mtarajiwa huku ukisubiri majibu. Kadri siku zinavyozidi kusogea njia hii inazidi kuwa ya kizamani kidogo na hivyo lazima kuwe na njia bora kabisa ya kuomba kazi tofauti na wengi walivyozoea lakini yenye uhakika. Njia hii mpya ni kuomba kukutana na mwajiri…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-161 Tatizo unajishikiza kwenye kuta za dimbwi la maji.

    Huwezi kuwa mwogeleaji hodari wakati unaendelea kujishikiza kwenye kuta za swimming pool. Ili uwe mwogeleaji mzuri lazima ukubali kuachia kuta za swimming pool na kuingia kati kati ya maji. Kama utaendelea kushikilia kuta za swimming pool, nakuhakakikishia utaendelea kuwasikia waogeleaji hodari kwenye redio. Vivyo kwenye hali kawaida ya maisha, kama ambavyo huwezi kuwa mfungaji hodari…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-154 Tatizo hujau kwamba kila kitu kina msimu wake

    Kila kitu kina wakati wake, wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna, wakati wa kulia na wakacti wa kucheka…. Hakuna kitu ambacho huwa kinatokea tu! Balli  ni majira ya kitu husika tu huwa yanapita Unapokutana na nyakati ngumu sio kwamba ule ndio unauwa mwisho wa safari wala  hicho sio chanzo cha wewe kulia bali ni…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA Tatizo hujaweka ukomo

    Ili kitu kiweze kufanyika vizuri na kwa ufasaha wa hali ya juu sana unahitaji kuhakikisha kwamba umewekiwekea ukomo hasa katika kukitenda na kukikamilisha. Usipokuwa na ukomo  katika kutenda utajikuta kwamba utakuwa unafanya hiki na kufanya kile. Utajikuta kwamba unaanza kufanya kitu fulani ila bado hukimalizi kwa sababu hakina ukomo, Kwani ukomo ni wa nini kwenye…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-153 Tatizo hujajua umuhimu wa mitandao ya kijamii

    Watu wengi sana kwa sasa wameingia katika wimbi la kulalamika kila wakati kwamba mitandao ya kijamii sio mitandao mizuri , badala yake imeharibu jamii. Wanaosema hivyo wanasisitiza kwamba mitandao hii imeleta upotovu mwingi sana kwa vijana kuliko ambavyo dunia imewahi kushuhudia kwenye zama za nyuma.. hata hivyo watu ambao wanasema hivyo wanasahau kwamba mitandao hii…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-137 Tatizo hutaki kujidogosha

    Kuna mwendeshaji mmoja wa baiskeli aliyekuwa anapita mahali na baiskeli yake. Alipofika eneo husika aliona kwamba kulikuwa kuna wanajeshi ambao walikuwa wanajaribu kuondoa kisiki bila mafanikio. Nyuma ya wale wanajeshi alikuwepo mtu mmoja aliyakuwa amesimama tu! Yule mwendesha baiskeli alimwulilza, inakuwaje rafiki yangu, mbona wewe huwasaidii watu hawa wakati unaona kwamba wanahangaika kuondoa kisiki”. Yule…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-136 Tatizo hujajua umuhimu wa soma kitabu

    Kitabu kimoja kina uwezo wa kubadlisha maisha ya mtu na kuyafanya kuwa ya tofati. Ila watu kidogo sana wanaweka juhudi kuhakikisha kwamba wanasoma na kuyatumia maarifa haya yaliyomo kwenye vitabu. Ukiongea na watu walio wengi utawasikia wakisema kwamba wao kusoma vitabu sio hobby yao. Wengine wanajisifia kwamba wao ni magwiji na hivyo hawahitaji kupata maarifa…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOIPOTEA-133 tatizo ni ukosefu wa nidhamu

    Mafanikio yoyote mazuri yanahitaji kuweka kazi kubwa sana kabla ya kuyapata na kuhakikisha kwamba kazi unaifanya kweli. Tatizo la kwa nini watu wengi sana hawapati kile ambacho wanakitaka ni kwamba wanagusa kila kitu na ila hawana kitu ambacho wanafanya. Kuna watu kwa sababu tu za kizembe, hawataki hata kuambiwa ukweli. Na wanaogopa kusikia maneno ambayo…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-132 Tatizo hauna mzigo wa kubeba

    Mara nyingi sana ukimwangalia mtu, anaweza kuwa ni rafiki kaka au ndugu akiwa ambeba mzigo mkubwa sana huwa unamwonea huruma. Unaona kama anajitesa kwa sababu abafanya kazi kubwa sana. anajitesa kwa sababu anabeba mzigo mkubwa sana. ukweli katika maisha sio kwamba aliyebeba  mzigo ndiye anapasa kuonewa huruma. Ila yule ambaye hajabeba mzigo ndiye anapaswa kuonewa…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-131 Tatizo hujaufahamu uwezo wako

    Tukiufahamu uwezo wetu tutakuwa kama ndege, tutaruka bila hofu. Tukiufahamu uwezo wetu tutakuwa kama mbegu, yaani tutaota bila kujizuia na kuzalisha msitu. Tukiufahamu uwezo wetu, tutaamua kufanya na tutafanya bila uoga. Kumbe ndio maana Eckharat Tolle anatuambia kwamba “hauwi mzuri kwa kujaribu kuwa mzuri, lakini kwa kutafuta uzuri ambao tayari umo ndani yako”. kumbe tayari…

  • TATIZO S RASILIMALI ZILIZOPOTEA -130 Tatizo hujataka kukjifunza kutoka kwa watu

    Watu wanaokuzunguka wewe hapo ni watu muhimu sana kuweza kwa kukusuma wewe kwenye mafankio. Watu hawa wanaweza kukusuma wewe hapo kwenye mafanikio kwa njia tofauti tofaut. Wapo wenye uwezo wa kukwambia kwamba kitu fulani ambacho unafanya wala hata hakiendani na kile ambacho unapaswa kuwa unakifanya. Watu hawa n muhimu sana kwako, watu hawa ni muhmu…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-126 tatizo hauna kiu ya kutosha

    Kuna kijana mmoja alimwendea Socrates ili kumuuliza siri ya mafanikio katika maisha. Socrates alimwabia kijana huyo wakutane siku inayofuata kwenye mto uliokuwa karibu yao. Kesho mapema socretes na kijana walikutana kwenye mto. Socretes alimwomba kijana watembee kwa pamoja kwenye mto ule. Walianza kutembea kwa pamoja huku maji yakizidi kuongezeka kina. Maji yalianzia kwenye miguu hatimaye…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA _125 Tatizo unaomba msaada pasipostahili

    Kuna nyakati wakati tuna kuza na kuendeleza vipaji vyetu vilivyo  ndani yetu huwa tunaona kwamba basi hapa ni bora kabisa kuhakikisha kwamba tunatafuta msaada kwa watu  ili waweze kutusaidia. Tunatafuta watu wa kutuwezesha kupiga hatua. Na pengine mtua anatafuta wazazi wake akijua haswa kwamba wao ndio watakaoshughulika na mawazo yake na kuhakikisha kwamba kile ambacho…

  • TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA-124 Tatizo hujajiiuliza maswali haya ya muhimu

    Hivi kwa nini katika jamii moja unakuta kuna mtu kafanikiwa na mwingine anahangaika na hali aliyonayo? Kwa nini baadhi ya watu kila wanachogusa kinageuka kuwa dhahabu wakati wengine kila wanachogusa hugeuka kuwa moto na kuwaunguza? Kwa nini baadhi ya watu wana mahusiano mazuri na wengine wanahangaika? Kwa nini kuna watu kila kitu wanaonekana wanatimiza lengo…

X