Hii ndiyo Siri ya wewe kutengenezea utajiri mkubwa kwenye maisha.


Na siri hii ni kwamba kama unataka kuwa tajiri basi fanya kinyume na watu wengine wanavyofanya.

Mara nyingi watu wengi huwa wanafuata mkumbo kwenye maamuzi yao. Kwa hiyo, maamuzi yao yanakuwa siyo sahihi. Mtu anafanya kitu Kwa sababu na jirani yake anafanya.

Mtu anajiunga na VICOBA Kwa sababu jirani na rafiki zake wote wamejiunga na VICOBA.

Hata hivyo, matajiri siyo watu wa kufuata mkumbo. Wana msimamo kwenye maamuzi yao na mara nyingi maamuzi yao yanakuwa ni ya tofauti na watu wengine. Wewe pia unapaswa kuwa kama wao

Mfano, utakuta watu wa kawaida wanasema kwamba uwekezaji ni hatari na hivyo hawawekezi. Matajiri wanajua kuwa uwekezaji ni hatari ila wanatafuta namna Bora ya kuwekeza huku wakiondoa au kupunguza hatari.

Watu wa kawaida wakiwekeza wanawekeza Kwa mkumbo, labda mfano hisa zinapokuwa zinapanda bei Kwa Kisha wanakuja kuuza Kwa hasara. Matajiri wanawekeza muda kujifunza na hivyo wanapochukua maamuzi ya Kununua hawanunui tu Kwa mihemko inayowaongoza watu wa kawaida Bali Kwa sababu wamefanya utafiti wao wa kina na wamejiridhisha kuwa uwekezaji fulani uko sawa.

Kwenye maisha yako hata kama huna mpango wa kuwa tajiri, jitahidi kuwekeza kama tajiri. Fanya kila kitu kama matajiri wanavyofanya. Utanishukuru sana Kwa hili rafiki yangu.

Kwa kusema hayo basi naomba nikusisitize Tena Kwa mara nyingine kuwa Siri ya wewe kutengeneza utajiri mkubwa kwenye maisha yako ni kufanya KAZI na shughuli zako, kinyuma kabisa na watu wengine wanavyofanya.

Kila la kheri

Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.

Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.

Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X