Ukifanya Hiki Kitu Kimoja Tu Utafanikiwa Sana


Rafiki yangu wa ukweli, kuna kitu kimoja ambacho endapo utakifanyia kazi, ni wazi kuwa utafanikiwa, tena siyo kwa viwango vya chini, bali utafanikiwa kwa viwango vya juu sana.Unaweza kuwa unajiuliza hili linawezekanaje maana kila siku najifunza kuhusu mambo mengi ya kufanya ili kufanikiwa.

Kitu kikubwa unachohitaji wewe siyo kufanya mambo mengi ili ufanikiwe, bali unahitaji kujithibiti wewe mwenyewe na kuhakikisha kwamba umekuwa na nidhamu kwenye yale unayotakiwa kuyafanya na kuyafanya bila ya kukosa. Ukiweza kufanya hili, ujue utafika mbali sana/

Hii ni kutokana na ukweli kuwa asilimia kubwa ya vile vitu vya msingi unavyotakiwa kufanya kwa ajili ya mfanikio yako, tayar unavijua.

Najua unajua kwamba unahitaji kuweka akiba. Kwa hiyo wewe unachohitaji sasa hivi siyo kuambiwa kwamba weka akiba. Unajua vizuri tu. unachohitaji ni nidhamu ya kuweka akiba bila ya kuacha.

Tayari unajua kwamba unapaswa kufanya kazi kwa bidii. Unachihitaji wewe siyo kuambiwa tena kwamba fanya kazi kwa bidii. Bali ile nidhamu ya kufanya kazi kwa bidii.

Tayari unajua kwamba mafanikio makubwa hayaji ndani ya siku moja. bali ni matokeo ya vile vitu vodogovidogo unavyokuwa unafanya kila siku na unavifanya kwa mwendelezo bila ya kuacha.

Kwa hiyo, unachihitaji wewe siyo kusubiri uwe na mabilioni ya fedha kwenye akaunti yako ili uwe bilionea, bal unajua wazi kuwa kuweka akiba hata kama ni kidogokidogo kwenye akaunti yako kila siku, kutekupeleka wewe kwenye ubilionea huo

Kumbe basi rafiki yangu, unachohitaji wewe siyo vitu vingi sana ili ufanikiwe. Unahitaji kitu kimoja tu. na kitu hiki ni nidhamu ya kuamua kufanya jambo na ukahakikisha kwamba hilo jambo unalifanya kwelikweli.

Sasa ninachotaka kutoka kwako siku ya leo ni kitu kimoja tu. Nataka uniambie ni kitu gani kimoja ambacho utakuwa unafanya na utakufanya kwa msimamo kila siku bila ya kuacha. Halafu, mimi nikusaidie kukufuatilie kwenye hilo, ukifanye hicho kitu mpaka uifanikishe.

Hilo ndilo jambo kubwa sana ambalo nilitaka kukwambia siku ya leo. Naomba nikutakie kila la kheri.

Kitu kimoja cha ziada, ningependa tu kukumbusha kuwa semina yetu ya ana kwa ana ambayo itafanyika Morogoro mwezi wa sita, ndio hiyo hapooo inakaribia.

Nichukue nafasi hii kukukaribisha kwenye semina hii ya kipekee sana.

Kitu kimoja cha kufanya ni wewe kuhakikisha kwamba unajiandikisha kwa ajili lya kuhudhuria semina hii. Fanya hivi. TUMA UJUMBE unaothibisha kwamba utashiriki kwenye hii semina kwa whatsap Namba 0755848391.

Ada ya semina ni 50,000/-


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X