Kuwa Imara


Tunaishi katika dunia ambayo haipendi vitu ambavyo siyo imara. Na hili jambo la KUWA imara halijaanza leo. Limekuwepo kwa siku nyingi sana.

Vitu ambavyo vimekuwa imara kwa miaka mingi ya nyuma, ndivyo ambavyo viliendelea kuishi, huku vile ambavyo siyo imara vikidhoofu na kufa.

Watu wanyonge, mimea minyonge, wanyama wanyonge havina nafasi kubwa ya kuishi Kama vile vitu ambavyo ni imara. Hivyo, na wewe unapaswa KUWA imara.

Najua hiki kitu kinaweza kuonekana cha ajabu sana hasa kwa upande wako ukizingatia kwamba umezoea kuambiwa KUWA wewe Ni MNYONGE. Na hivyo kuna watu wanakutetea wewe na unyonge wako.

Ninachotaka kukwambia ni kuwa, usikubali kuwa MNYONGE. Unyonge ni hali ya chini ambayo MTU yeyote hapaswi kuibeba.
Unapaswa KUBEBA ujasiri, uthubutu, na sifa nyingine za aina hii.

Unyonge haukai meza moja na ujasiri. Unyonge hauwezi kukaa meza moja na uthubutu. Unyonge hauwezi kukaa meza moja na utawala.
Ukiwa MNYONGE unanyongwa na haki yako hupewi. Huo ndio ukweli.

Hivyo, nataka ujiondoe kwenye hali ya unyonge kuanzia Leo hii na uanze kuwa jasiri, uwe imara.

Kama kuna rafiki unayemfahamu anayepaswa kuwa imara mtumie ujumbe huu hapa kupitia hapa chini

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE

Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X