Kazi Yako Ya Kwanza



Rafiki yangu mpendwa salaam. Najua kuwa unapambana sana kwenye shughuli zako za kila siku. Hongera sana Kwa hilo.

Siku ya Leo ningependa kukwambia kitu kimoja kikubwa sana. Kitu hiki ni kuwa kama unataka kufanikiwa kwenye maisha basi fahamu kuwa KAZI yako ya kwanza kabisa ni kuhakikisha haufi.
Hakikisha unaendelea kuishi.

Hilo, ukishalifanikisha kinachofuata ni wewe kuendelea kupambania ndoto na malengo yako makubwa. Kama kweli utayapambania Kwa ustadi wa hali ya juu. Ni wazi tu kuwa Kuna siku, lazima tu utafanikiwa.

Kwa sababu kanuni ya asili ilivyo ni kuwa hakuna juhudi ambazo Huwa zinapotea Bure. Kwa hiyo, hiki unachofanta Sasa hivi na vingine ambavyo umewahi kufanya, vitaunganisha nguvu na kukuletea wewe mfanikio makubwa.

Hivyo, hakikisha unaendelea kuishi
Jilinde
Ilinde afya yako
Kisha pambania malengo yako


2 responses to “Kazi Yako Ya Kwanza”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X