Hivi kaa chini ufikirie kama kila mtu angekuwa ni mzembe kama wewe.
Kama kila mtu angekuwa na visingizio kama wewe
Kama kila mtu angekuwa ni mwoga kama wewe
Kama kila mtu angekuwa ni mlalamikaji kama wewe.
Kama kila mtu angeona aibu kuitumia akili yake?
Kama kila mtu angesema ni acha nile maisha leo kesho itajijua yenyewe
Hivi unadhani nani angethubutu kufanya vitu vya tofauti. Ni nani angethubutu kutengeneza nguo unazovaa? Ni nani angethubutu kuanzisha biashara ambazo zinakusaidia wewe kuweza kufanya kazi zako.
Bila shaka asingekuwepo. Kila unapoona kitu kizuri basi ujue kwamba kuna watu waeamua kuachana na uoga, ulalamikaji, uzembe, kutupia watu lawama na wamekuwa tayari kubeba majukumu ya maisha yao.
Hivyo basi, kitu ambacho unapaswa kufanya kuanzia leo basi ni kuchukua hatua, kuacha kulalamika, uzembe, kutupia watu lawama na uwe tayari kubeba majukumu yanayokuhusu.
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA