Jinsi ya kuwa mtu mwenye msaada kwa wengine


Huwa inatokea kwamba mtu anasoma makala yangu ambayo niliandika siku nyingi za nyuma, kisha mtu huyo anasema kwamba hiyo makala imemsaidia sana.

Mfano leo hii wakati naandika makala hii nimeagalia maoni kwenye blogu kwenye makala za nyuma nimeona kwamba, maoni ya jana yaliwekwa kwenye makala ya ambayo mimi niliandika mwaka jana mwezi wa 11.

kwangu hiki siyo kitu cha kushangaza kwa sababu wakati mwingine unaweza kukuta mtu kaweka maoni kwenye makala ambayo niliandika hata miaka mitano iliyopita.

wakati mwingine mimi nakuwa nimeshaandika na kusahau kuwa niliandika hiyo makala.
lakini andikko hilo linakuwa lenye msaada kwa mwingine.

KITU HIKI ndicho kinanileta kwenye ujumbe wa leo ambao ningependa kukwambia. NA UJUMBE huu ni kwamba, kamwe usipitishe siku bila ya kufanya kitu ambacho utaona kwamba kinaongeza thamani kwa watu wengine. Kila siku fanya kitu ambacho kitaongeza thamani kwenye maisha ya mtu mwingine. Hiki kitu kinaweza kisisaidie mtu uliyemlenga leoleo. lakini kwa sababu umekifanya, kinaweza kumfikia huyo mtu hata baada ya miaka kadhaa.

sasa swali langu kwako siku ya leo ni kuwa ni kitu gani ambacho unaenda kufanya ambacho kitakuwa chenye msaada kwako na kwa wengine hata kwa siku zijazo.

USIWE mbinafsi kwa kutaka kufanya vitu ambavyo vitakunufaisha wewe tu.
Asante sana na kila kheri


One response to “Jinsi ya kuwa mtu mwenye msaada kwa wengine”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X