Vitu Vitano Vinavyotofautisha watu wanaopata mafanikio ya kawaida na mafanikio makubwa


Watu wawili, wanaweza kuzaliwa na wazazi walewale, wakapata elimu ileile, chini ya walimu walewale. Na kwenye mazingira yaleyale. Ila mmoja akatokea kuwa mwenye mafanikio makubwa sana, huku mwingine akiwa na mafanikio ya kawaida sana au hata pengine kuishia kwenye umasikini. Unajua kwa nini kitu kama hiki kinatokea.

Kwenye makala hii ya siku yaleo ninaenda kukuonesha kwa nini hili huwa linatokea na kitu gani hasa ambacho unaweza kufanya ili uweze kuwa na mafanikio makubwa. Au mafanikio ambayo wengine wanaona kama vile siyo mafanikio ya kawaida.

Lakini kabla sijakwambia kitu kama hiki ningependa ufahamu stori moja ambayo kiuhalisia ipo kwenye maisha ya kila siku. Vijana wawili walizaliwa na baba mmoja ambaye alikuwa mlevi. Kipindi chote wanakua watoto wale, kitu kikubwa sana walichokuwa wanaona kwa mzazi wao, yaani, baba yao, kilikuwa ni kulewa. Kwa hiyo, hiki kitu kiliwafanya wawe na mtazamo tofauti kuhusu maisha.

Kijana mmoja alipokua. Alianza kulewa.

Huku kijana mwingine alipokua alikuwa mfanyabiashara.

Wandishi wa habari siku moja walikuwa na shauku ya kutaka kujua kwa nini mapacha wawili wawe na maisha ya tofauti kiasi hicho.

Mwandishi wa habari alimfuata kijana wa kwanza ambaye alikuwa ni mlevi na kutaka kujua kwa nini alikuwa mlevi. na kwa nini alilewa kila siku.

Yule mlevi alijibu kwa kusema kwamba nilijifunza kwa baba yangu.

Mwandishi wa habari alimfuata kijana mwingine ambaye alikuwa ni mfanyabiashara na kumwuliza kwa nini alikuwa mfanyabiashara, na yule alijibu kwa kusema kwamba nilijifunza kwa baba yangu,

Yaani, vijana wote wawili walijifunza kwa baba yao. Yule mlevi alichoona kwa baba yake ulikuwa ulevi, hivyo, aliishia kulewa.

Yule mfanyabiahsara aliona namna ambavyo baba yale alikuw anatumia fedha zake hovyo hovyo kwenye mambo ambayo hayakuwa ya msingi. Aliona jinsi ambavyo wafanyabishara walikuwa wanakusanya pesa kutoka kwa baba yake na walevi wengine kila siku katika vinywaji, mishikaki na vinginevyo vingi. Hivyo, akaona kwamba ukiwa mfanyabiashara basi unakuwa unakusanya pesa kutoka kwa watu.

Alijiambia kwamba, kuna watu wanapenda kutumia hela zao na kuwapa wengine. Ila hawawezi kukupa hiyo pesa kama wewe mwenyewe huna cha kuwapa. Na utapata cha kuwapa kupitia biashara, hivyo, kwa namna hiyo, akawa ameamua kuwa na biashara.

Hiki kitu kilimsukuma kufanya makubwa na kujituma zaidi kwenye kazi zake na hivyo kuwa mfanyabishara mkubwa wa nyakati zake.

Kitu kama hiki pia unawez akukiona kwa watu wengi ambao unakutana nao kila siku. Kuna watu wengi wanaiga maisha na kuishi maisha ambayo siyo ya kwao kwa lengo la kutaka kuonekana au kuwa na maisha ya aina fulani. Wengine wanaiga kwa kujua hukau wengine wakiwa wanaiga kwa kutokujua.

Na hivyo kitu cha kwanza kabisa kinachofanya watu wafanikiwe na kuwa na maisha bora ni watu ambao wanawatazama. Kwa kiingereza hawa watu wanajulikana kama mentors au role models.

Hwa ni watu ambao unakuwa unawatazama na kujifunz kutoka kwao.

Kama unataka kufanikiwa na kufanya makubwa zaidi. hakikisha kwamba unatafuta mentors au role models ambao utajifunza mazuri kutoka kwako. Hkauna role model hata mmoja ambaye anaweza kuwa amekamilika kwa asilimia 100. Ila kwa kila mtu hata kama hafanyi vizuri, bado unaweza kujifunza kitu ambacho kinaweza kukusaidia wewe kupiga hatu akwenye safari yako ya mafanikio.

Mfano kwa mtu ambaye hajafanikiwa, unaweza kujifunza vitu ambavyo vimemfanya kutofanikiwa na kuvipeuka ili ufanikiwe.

Kwa mtu ambaye hana akiba, unaweza kujifunza namna ya kuweka akiba na kuiweka ili ufanikiwe.

Kwa mtu ambaye hana mahusiano mazuri unaweza kujifunza vitu ambavyo anakosea ili uboreshe mahusiano yako.

Hivyo hivyo kwa watu ambao wamefanikiwa. Kwa hawa watu unaweza kujifunza vitu ambavyo vinawafanya wafanikiwe mpaka kufikia walipo na hivyo kukuwezesha wewe kupiga hatu akubwa sana.

Kitu cha pili kinachowatofautisha wale wanaofanikiwa sana na wale wenye mafanikio ya kawaida ni kwenye kuchapa kazi. Ujue nguvu ambazo mtu unaweka kwenye kazi ni zilezile. bila kujali kwamba unapata mafanikio kidogo au unapata mafanikio makubwa. Sasa kama nguvu ni zilezile kwa nini usiweke nguvu kubwa kuhakikisha kwamba unapata matokeo makubwa mara zote.

Mtu ambaye ana lengo la kawaida atapata matokeo ya kawaida kwa kutumia nguvu ileile ambayo mtu mwenye lengo kubwa analo. na mwenye lengo kubwa atapata matokeo makubwa kulingana na lengo lake.

Na hiki kitu kinanileta kwenye kitu cha tatu kinachowatofautisha watu wa kawaida na wale ambao wanakuwa na amfanikio makubwa. Kitu hiki ni kuwa na malengo. Na watu wanaopata mafanikio ya kawaida siyo tu kwamba wanakuwa na malengo, bali wanakuwa na malengo ambayo wanayafanyia kazi na kuhakikisha kwamba hayo malengo yamekuja kwenye uhalisia.

Sasa wewe unayo malengo rafiki yangu?

Kama hauna malengo, hakikisha kwamba siku ya leo unakaa chini na kuandika malengo yako. kabisa, yaandike malengo yako rafiki yangu ili yaweze kuja kwenye uhalisia.

Malengo ambayo hayajaandikwa rafiki yangu ni kazi bure. Yaandike malengo yako, na kila siku yarudie malengo yako kwa kujikumbusha.

Hiki kitu ndicho kinaleta kwenye jambo letu la nne kwa siku ya leo ambalo ni kujikumbusha malengo yako. Utafiti ambao ulifanyika, ulionesha kwamba mabilionea wanajikumbusha malengo yao, siyo chni ya mara 29 kila siku. Yaani, hawa hawamezwi na kitu kingine chochote kile isipokuwa tu malengo yao.

Vitu vingine vyote wameweka chini, wanachopambana nacho ni malengo yao. Hawajikumbushi kwamba kuna msanii katoa wimbo mpya. hawajikumbushi kwamba kuna watu wanapendana na siku ya vlentine wametokaje. wanajikumbusha malengo yao rafiki yangu.

Na siyo tu kijikumbusha malengo yao kwa maneno bila kutimiza wajibu, bali kwa vitendo pia. hiki kitu kinanileta kwenye pointi ya tano na ya mwisho kwa siku ya leo ambayo ni vitendo. Yaani, kufanyia kazi vile vitu ambavyo unapaswa kufanyia kwa vitendo. Haitoshi tu kuwa role model mzuri, haitoshi tu kuwa na malengo, haitoshi u kujikumbusha malengo yako hata mara 100 kila siku. Vitendo rafiki yangu. Yaani, kufanyia kazi kile ambacho unajifunza na kuhakikisha kwamba kimekuja kwenye uhalisia. hiki ni kitu muhimu kwako na unapaswa kuwa unakifanyia kazi kila siku.

Panga, ila fanyia kazi pia kile ulichopanga.

mipango bila vitendo ni kazi bure.

Kwa hiyo rfiki yangu, kafanyie kazi haya uliyojifunza hapa kwa vitendo.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X