Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Tofauti Kati ya wale wanaofanya makubwa na wale wanaofanya vitu vya kawaida - SONGA MBELE

Tofauti Kati ya wale wanaofanya makubwa na wale wanaofanya vitu vya kawaida


Kwenye kitabu cha 10X Rule Grant Cardone,  anasema kwamba tofauti pekee Kati ya wale watu wanaofanya makubwa na wale wanaofanya mambo ya kawaida imelala kwwnye  kanuni ya mara kumi zaidi.

Kadiri ya kanuni hii Ni kwamba kama unataka kupata matokeo makubwa zaidi ya unavyopata sasa hivi, sharti uwe tayari kufanya vitu mara kumi zaidi ya unavyofanya sasa hivi.

Unapaswa KUANZA kwa kuweka malengo MAKUBWA mara kumi zaidi.
Unapaswa kuchukua hatua mara kumi zaidi.
Unapaswa kwenda hatua ya ziada mara kumi zaidi.
Kiufupi kwenye maisha yako unapaswa kuwa MTU wa mara kumi zaidi ili uweze kupata Yale unayotaka.

Hivyo ndivyo unapaswa kuishi kwenye maisha yako.

Unaweza usinielewe vizuri sana ninapokwambia kanuni ya mara kumi zaidi. Ila ngoja nikueleweshe kwa undani ZAIDI. Tuchukulie wewe ni mwanachuo. Unasoma chuo AA

Na kuna notsi ambazo profesa alitoa Ila Sasa kwa bahati mbaya hizo notes umezipoteza.
Ila unajua marafiki zako wanazo. Ila kwa bahati mbaya, unazihitaji hizi notes SAA tano usiku na marafiki zako wamelalala tayari. Sasa inafanyaje?

Unaweza kuamua kumtumia Innocent ujumbe ili akutumie hizo notes halafu ukatulia. Japo utakuwa umefanya uamuzi mzuri wa kuomba notsi kwa Innocent. Ila inawezekana Innocent asiingie hewani usiku huo au hata akawa mbali na simu. Au akaona ujumbe wako Ila akaaanza kufanya Mambo mengine mpaka akasahau kukutumia notsi.
Au hata akaona ujumbe wako Ila akawa Hana kifurushi Cha kukutumia hizo notsi.

Hivyo, kama upo makini utatumia kanuni ya Mara kumi zaidi kuomba notsi.
Utatuma kwa ujumbe wa kuomba notsi hizo kwa
Innocent
Janet
Jeni
Said
Abdallah
Joseph
Ashura
……..yaani, kiufupi utatuma kwa watu wasiopungua kumi.

Nakuhakikishia siyo wote watakujibu kwa wakati.
Siyo wote watakutumia hizi notsi
Na wengine wanaweza hata wasiwe nazo Kama wewe.
Wengine watakuwa wanazitafuta Kama wewe
Na wengine wataona Ila watasahau kukutumia.
Ila hatakosa mmoja au wawili au watatu wa kukutumia notsi zako.

Kwa jinsi hiyo, notsi zako utakuwa umezipata.

Sasa huu mfano unafanya kazi kwenye vitu vingine kwenye maisha. Mara zote fikiri Mara kumi zaidi.
Chukua hatua Mara kumi zaidi.
Piga simu kwa wateja mara kumi zaidi
Kutana na wateja Mara kumi zaidi
Weka LENGO la kuuza Mara kumi zaidi.
Soma vitabu Mara kumi zaidi ya wengine
FANYA mazoezi Mara kumi zaidi

Hii inakuweka kwenye eneo zuri Sana kuliko MTU ambaye anakuwa anafanya vitu kwa namna ya kawaida.
Usiwe mtu wa kawaida. FANYA kazi Mara kumi zaidi

Kila la kheri


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X