Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Ni muda upi mzuri kuanzisha bishara - SONGA MBELE

Ni muda upi mzuri kuanzisha bishara


Rafiki yangu, unaweza kuwa unajiuliza hivi ni muda upi mzuri kwangu kuweza kuanzisha biashara? Rafiki yangu hili swali limekaa kimtego sana.

Kuna watu ambao huwa wanaanza kufanya utafiti kuhusiana na biashara ambayo wanataka kufanya, ila huo utafiti wao huwa haufiki mwisho.

Kuna watu ambao kila mwaka huwa wanajiambia kwamba wataanza biashara ila huwa hawaanzi, mwaka huwa unaisha na tena mwaka mwingine huwa wanasema kwamba nitaanzisha biashara mwakani. Rafiki yangu, pengine tujiulize hivi muda upi ni mzuri kwako kuanzisha biashara?

Wengine huwa wanasema kwamba wanatafuta mtaji. Yaani, kwamba wakishapata mtaji basi moja kwa moja wataweza kuanzisha biashara bila kuchelewa. Na pengine huwa wanaingia kwenye ajira ili waweze kupata mtaji. Ila cha kushangaza ni kwamba miaka huwa inazidi kupita wakiwa bado hawajaanzisha hizo biashara, kumbe, kuajiriwa kwa ajili ya kutafuta mtaji, linaweza kuwa ni wazo zuri sana, na wakati huo huo, linaweza lisiwe wazo zuri sana.

Sasa ni muda gani mzuri wa wewe kuanzisha biashara. Kwa mfano, ukikutana na mimi na kuniuliza swali la aina hii, nitakwambia kwamba anzisha biashara sasa hivi. Ndio sasa hivi. hata kama huna mtaji. Hata kama huna mtaji mkubwa

Hata kama umeajiriwa. Hata kama unasoma. Wewe anzisha biashara sasa hivi, kisha kutokea hapo sasa ndio uendelee kubore

Lakini kitu kikubwa ni kwamba, ukianzisha biashara inakuweka kwenye mwendo. Unakuwa umejinodoa kwenye ile hali ya utulivu. Yaani, ile hali ya kuendelea kusubiri. Mtu ambaye anasubiri kwamba siku moja atakuja kuanzisha bishara, kuna uwekano mkubwa akwamba huyu mtu hatakuja kuanzisha biasharamaisha yake yote.

Unajiuliza kwa nini?

Ngoja nikujibu sasa,

Kadiri ya sheria ya Netwton. Anasema kwamba kitu chochote kile ambacho kimetulia au kimekaa kwenye utulivu, kitaendelea kukaa hivyohivyo mpaka pale nguvu ya ziada itakapotokea. Na kitu kilicho kwenye mwendo kitaendelea kuwa kwenye mwendo mpaka pale nguvu ya ziada itakapotokea kukizuia.

Sasa wewe unapoanzisha bashara, unajiweka kwenye mwendo. Unaanza

Kuna mengi ambayo utajifunza ukiwa kwenye mwendo, kuliko pale ambapo unakuwa haupo kwenye mwendo.

Kuna mengi utajifunza ukiwa na biashara kuliko pale ambapo unakuwa hauna biashara. Ndio maana unahitaji uanzishe biashara yako rafiki yangu. siyo hilo tu, ngoja tuendelee kuona hili

Ukianzisha biashara katika hizo nyakati ambazo pengine kwa upande wako unahisi kwamba haupaswi kuanzisha biashara, na hiyo biashara ukaweza kuisimamisha mpaka ikaweza kuwa biashara bora. Ni ukweli usiopingika kuwa lazima utakuja kuwa shujaa kwenye maisha yako.

Kuna watu watataka kujifunza kutoka kwako kuhusiana na namna ya kuanzisha biashara na kuziendesha katika namna kama hiyo. na wewe utaweza kuwapa ushauri mzuri bila shida yoyote ile.

Rafiki yangu, nadhani siku ya leo uondoke na kitu kimoja tu. KUANZISHA BIASHARA.

Kama umekubaliana na mimi kwenye hili. Njoo whatsap sasa hivi, nitumie ujumbe unaoonesha kwamba biashara utakayoenda kuanzisha ili tuweze kushauriana.

Lakini pia hakikisha umepata mwongozo ambao watu wengi wanaoanzisha biashara wameutumia kwa manufaa makubwa sana. Na mwongozo huu siyo mwingine bali kutoka kwenye kitabu cha MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA B ISHARA. Watu wengi waliosoma hiki kitabu wamethibitisha kuwa hiki ni moja ya kitabu chao bora sana kwao kuwahi kusoma. Ningependa na wewe uweze kupata nakala yako bila ya kuchelewa rafiki yangu.

Hardcopy ya kitabu hiki ni 20,0000/- na SOfrtcopu ni 10,000/- tu karibu sana rafiki yangu.

Ni kitabu kizuri sana, ambacho watu wengi waliokisoma wamekipenda sana. Lipia kitabu hiki sasa kwa 0755848391 jinan i GODIUS RWEYONGEZA

kUMBUKA. Kama unataka kuanzisha biashara ambayo itafika mbali. basi hiki kitbu ndio mwongozo wako ambao unapaswa kuhakikisha umeupata. Gharama ya mwongozo huu ni 20,000 kwa hardcopy na 10,000/- kwa soft copy.

Karibu sana.


2 responses to “Ni muda upi mzuri kuanzisha bishara”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X