Kama Unatumia Nguvu Kubwa Kujitambulisha…


Kama unatumia nguvu kubwa  kujitambulisha jua bado unapaswa kuweka nguvu kubwa kwenye kufanya kazi kwa bidii pia.

Unajua kwa nini? Kwa sababu watu hawakujui.

Pata picha Sasa hivi umepigiwa simu na
Samia Suluhu Hassan
Vile tu akijitambulisha kwako, hutahitaji KUANZA KUMWULIZA maswali mawili au matatu. Utakachofanya utaanza kumsikiliza anataka kusemaje?

Lakinj he, vipi wewe kwa upande wako. Ukimpigia mtu mgeni ambaye hana namba Yako inakuwaje? Atakufahanu? Atasema ndio nakufahamu .. na KUANZA kukusikiliza unasemaje au utaanza kujitambukisha Mara tatu, tatu.

Ukiona unatumia nguvu kubwa kujitambulisha, basi jua kazi unayo.
Bado unapaswa kufanya kazi kwa bidii. Tena kwa bidii sana.

Sasa kazi yako ya leo. Chukua namba kumi ngeni ambazo hujawahi kuzipigia. Watu ambao hawakujui.
Wapigie simu.
Je, unajitambulisha kilaini? Wanaelewa jina lako? Je, ulipowaambia bidhaa yako wameitambua haraka? Unaweza kufanya hivyo kwa watu wengine 100 nao wakakutambua wewe na bidhaa yako mapema.

Kama siyo kaongeze bidii kwenye kazi.

Imeandikwa na
Godius Rweyongeza
www.songambele.co.tz
0755848391
Morogoro-Tz


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X