Hii Ni Sanaa Unayopaswa Kuitumia Kila Siku Kwenye Maisha Yako


Rafiki yangu, nipe dakika moja tu nikufundishe Sanaa unayopaswa kuitumia kwenye maisha Yako kuanzia leo hii.

Wakati tunasoma Sekondari tulikuwa tunasikia stori kuwa masomo ya sayansi yanalipa sana. Hivyo, NGUVU kubwa tukaiweka huko

Nilipoingia chuoni, ni kozi ya horticulture. Hapa kitu Cha kwanza kabisa unachofundishwa, unaambiwa kuwa horticulture is an art and sayansi. Halafu kumbe siyo sayansi ni science kwa kiingereza. Hahaha.

Hii maana yake ni kwamba horticulture Ni Sanaa, lakini pia ni sayansi. Hapa ndipo nilianza kuuona umuhimu wa sanaa kwenye maisha. Maisha yanahitahi vyote viwili. Maisha yanahitaji sayansi na sanaa. Na vyote viwili tunavitumia kila siku bila kujali chuo ulisoma nini nala hukusoma Nini. Iwe ulikuwa mkali Sana kwenye fizikia kama Einstein, au ilikuwa MTU wa kawaida. Bado utaihitaji Sanaa. Na hata Kama ilikuwa hupendi sayansi kiasi ulikuwa unailaani, kwenye maisha ya kila siku, unaihitaji. Hivyo, vyote viwili tunavihitaji. Na kwa Leo nataka nikufundishe Sanaa moja Itakayokusaidia wewe Kufanikisha mengi

Na Sanaa hii siyo nyingine, bali Ni kusikiliza.

kusikiliza ni sanaa ambayo itakufikisha mbali Sana.

Watu wanapenda kusikilizwa aisee. Naomba kwanza nieleweke kwamba Kuna TOFAUTI kubwa Kati ya kusikia na kusikiliza.

Unaweza kumsikia MTU  ila ukawa hujamsikiliza. Kama MTU amewahi kuongea Jambo na ukawa umemwambia arudie japo alikuwa ameongea kwa sauti. Hapo jua wazi kuwa hukumsikiliza.

Kumsikiliza MTU kunahitaji uweke umakini wake wote kwake

Kuna watu unakuta kwamba hawana shida Wala tatizo lolote, wao wanachohitaji kwako ni kuwasikiliza na kuwapa umakini wako. Hivyo basi rafiki yangu, ninaomba kitu kimoja kwako kuwa msikilizaji.

Yaani, unapokuwa unaongea na MTU, NGUVU zako na Akili Yako yote iweke kwake badala ya kutawanya nguvu zako.

Inalipa sana kusikiliza.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X