
Rafiki yangu umewahi kujiuliza kwa nini huwa tunarudia kusoma vitbu ambavyo tulishavisoma siku za nyuma. Nimeanza mwaka huu kwa kurudia kusoma kitabu cha THINK AND GROW RICH. Na mwaka huu kuna vitabu vingi ambavyo nitakuwa narudia kusoma zaidi ya hiki. Unajua kwa nini huwa tunarudia kusoma vitabu.
Huwa tunarudia kusoma vitabu kwa sababu kwenye kusoma hicho kitabu kuna kitu cha ziada ambacho tutapata kutoka kwenye hicho kitabu ambacho pengine mara ya kwanza wakati tunasoma hicho kitabu hatukukipata.
Huwa tunarudia kusoma vitabu kwa sababu mara ya kwanza wakati tunasoma kile kitabu tulikosoma kwa mlengo fulani.
Mfano, kama inawezekana WAKATI nasoma kitabu hicho nilikuwa nataka kujifunza zaidi kuhusu kuweka akiba, kipindi hicho mambo ya kuwekeza yalikuwa hayajaingia kichwani maana hata hela yenyewe ya kuweka akiba ilikuwa ni shida, ila sasa hivi nasoma kitabu ili nijifunze zaidi kuhusu uwekezaji.
Au pengine nilisoma kitabu kwa sababu nilikuwa nataka kujua namna bora ya kuingia kwenye mahusiano. Ila sasa hivi nimeshaingia kwenye mahusiano na sasa nataka kujifunza zaidi kujenga na kuboresha mahusiano.
Au pengine nilisoma kitabu nikiwa najifunza namna ya kuanzisha biashara. Lakini sasa hvii nataka kujenga timu kwenye biasahara yangu.
KWA HIYO RAFIKI YANGU, hivyo ndivyo vitu ambavyo vinatufanya tusome vitabu na turudie kusoma vitabu zaidi na zaidi.
Unaporudia kusoma kitabu ambacho ulishasoma mara ya kwanzpata unajikuta kwamba kuna itu vya ziada ambavyo unakuwa unapata kutoka kwenye kile kitabu ambavyo hapo mwanzoni huku
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
One response to “Kwa nini huwa tunarudia kusoma vitabu”
Asante