KITABU: MAAJABU YA KUSOMA VITABU


Mwezi septemba mwaka 2019 niliandaa kitabu kifupi cha Maajabu Ya Vitabu. Kitabu hiki hapa nilikisambaza bure mtadaoni. Kimetokea kuwa moja ya kitabu cha Kiswahili ambacho kimesomwa na watu wengi sana.

Mwanzoni sikutegemea kama kitabu hiki kingesomwa na watu wengi sana. Ila kilichotokea toleo la kwanza la kitabu hiki hapa kilisomwa na maelfu kwa maelfu ya watu. Asilimia kubwa ya wasomaji wa toleo la kwanza wakawa wananitafuta na kueleza jinsi kitabu hiki kilivyobadili fikra zao kuhusu usomaji wa vitabu. Kuna watu wamejenga tabia ya kusoma vitabu mara baada ya kuwa wamesoma kitabu kile na sasa hivi watu hao ni wasomaji wazuri wa vitabu.

Kwa hiyo, kitabu hiki kikaniunganisha na wahariri, wasomi, wakulima na watu wa kila aina kutoka ndani na nje ya nchi. Wengi wao tumejenga urafiki baada ya kuwa wamesoma hiki kitabu mpaka leo hii. Wapo waliosoma kitabu hiki hapa wakasema kwamba mimi lazima nisome na vitabu vyako vingine. na kweli wakawa wamechukua hivyo vitabu na kuvisoma pia.

Kila aliyesoma kitabu hicho alimtumia na mwenzake ili asome. Hivyo, kwa njia hiyo kikazunguka kila kona ya nchi hii na dunia nzima kiujumla kwa wasomaji wote wa lugha ya Kiswahili.

Hata hivyo, kadiri muda ulivyokuwa unaenda nikaendelea kuboreshakitabu hiki hapa. na hivyo, leo hii napenda kukwambia kwamba lile toleo la kwanza la kitabu cha Maajabu Vitabu halipo tena. Sasa tuna toleo la pili ambalo limeboreshwa mara 30 zaidi ya lile toleo la kwanza. Kama ulisoma toleo la kwanza ukasema, “looo, hiki ni kitabu cha kipekee kweli!”

Sasa ukisoma toleo la pili ni wazi kuwa , hizo looo, zitakuwa mara 30 zaidi. hahah.

Utatumiwa kitabu chako bila kuchelewa.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X