STRIVE MASIYIWA


STRIVE MASIYIWA

Strive Masiyiwa ni bilionea wa Zimbambwe ambaye alizaliwa mwaka 1961 huko nchini Zimbambwe. Alikulia nchini Zimvambwe na baadaye alienda kusoma masomo ya chuo kikuu nchini Uingereza akisomea uhandisi. Baada ya masomo Strive Masiyiwa kama walivyokuwa watu wengine wazalendo wa kipindi kile alirudi nchini mwake kwa ajili na kuanza kufanya kazi na shirika la mawasiliano, akiajiriwa Kama mhandisi

Masiyiwa anasema kwamba, kila mara  alipokuwa akitoka kazini alikuwacna mazoea ya kukutana na marafiki zake baa ili wapate moja baridi, moja moto.

Siku moja katika maongezi na rafiki zake alipendekeza kuwa watenge kiasi kidogo Cha fedha, yaani na wawe wanaweka kiasi hicho kama akiba kwenye akaunti Yao ya benki. Alipendekeza wazo hili kwa watu 10 Ila waliochukua hatua na kuweka akiba walikuwa wawili tu.

Mpaka hapo tunajifunza kuwa unaweza kuwa na marafiki wengi, Ila kumbe hao marafiki siyo wale wa kushirikiana na wewe katika upambanaji Bali wanakuwa marafiki wa bata tu! Ukiwa na mmarafiki wa Aina hii, mafanikio kwako yanakuwa magumu kwa sababu hawafikirii nje ya boksi, na hata pale wanapokuwa na wazo hawachukui hatua.

Sisi kama mabilionea mafunzoni tuna mengi ya kujifunza kutoka kwake. Kuanzia namna unavyoweza kuanzia chini kabisa, ambapo Masiyiwa anasema kwamba kwake hakuna kilichobadilika, unaanza na kile ulichonacho, unafanya kinachowezekana ili mwisho wa siku uweze kufanya yasiyowezekana.

kuja kwenye kukuza mtaji, kuja kwenye kujenga timu.
Kuja kwenye kwenye kupambania ndoto, kusaidia watu na kutoa na vitu vingine.

Asilimia kubwa ya vitu ambavyo tunafanya Sasa hivi Masiyiwa alivipitia miaka mingi iliyopita.

Kadiri ya Forbes Masiyiwa Ni bilionea namba 1012
Utajiri wake ni Dola bilioni 3
Utajiri wake mkubwa unatoka kwenye mitandao ya simu

Ambapo anamiliki zaidi ya 50% ya kampuni ya Econet Wireless


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X