App Itakayokusaidia Kutuma SMS baadaye, kupiga simu kwa wakati na kudai hela zako๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚


Katika makala ya leo tunaenda kuona namna ya kuandaa ujumbe leo na ukautuma siku ya krismasi au mwaka mpya. HutahItajika kuuandika tena au kuutuma tena
Tutaona namna ya kupanga kumpigia siku za mbeleni na ukampigia kwa uhakika bila kukosa hata dakika 1
Tutaona namna ya kupangilia watu wa kuwasiliana nao.
Tutaona njia nzuri ya kukukumbusha kufanyia kazi majukumu yako na kuyafanikisha na mengine mengi.

Kwa wale waliojiunga na emali list yangu watakumbuka kuwa huwa nawatumia ujumbe wa kuwapokea ambao huwa
Unawaahidi kuendelelea kuwashirikisha vitu mbalimbali vya kuwasaidia kupitia makala na mafunzo ambayo ninatoa kwa njia ya baruapepe. Na hiki ni kitu ambacho nimekuwa nikikifanyia kazi. Kama wewe hujajiunga na email list yangu, hakikisha unafanya hivyo kwa KUBONYEZA HAPA ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ na kujaza taarifa zako kamili.



Hiki kitu huwa nakifanyia kazi mara kwa mara na leo napenda kukuletea app ambayo inaweza kukusaidia SMS siku za mbeleni.

Mfano tuseme,  nataka nikuandalie ujumbe mzuri wa kheri ya krismasi.

Ila Sasa nataka niuandae ujumbe huu uje kwako siku ya krismasi Ila nataka niuandae Leo hii tarehe 18.12.2022. na ninataka ujumbe huu uje kwako tarehe 25.12.2022 saa moja asubuhi.
Kwa kutumia app hii inawezekana.

Au tuseme kwamba tumeongea leo tarehe 17 na umeniambia nikupigie tarehe 31 Disemba saa kumi na mbili na nusu jioni kabla hujaenda kwenye mkesha wa mwaka mpya.
Halafu nikaongea na mwingine akaniambia nimpigie tarehe 23 asubuhi saa mbili. Nikawa na orodha ya watu ishirini na kila mtu Anataka mimpgie kwa muda wake, saa yake na tarehe yake. Utakumbukaje?

Utaandika kwenye diary si ndio?  Kuandika Kwenye diary ndio suluhisho la Watu wengi Ila tatizo muda mwingine unaweza kusahau, na linapokuja suala la muda Kuna watu wengi ambao utajikuta huwapigii kwa wakati.

Siku ya leo nina app ambayo nimekuwa naitumia na imekuwa inanisaidia kutuma SMS muda, saa na dakika ninapotaka.
Imekuwa pia inanikumbusha kuwapigia watu muda, saa na dakika tulipokubaliana.

Tuseme nataka nikutumie wewe ujumbe Leo saa kumi jioni. Lakini muda huu ninapoandika makala hii ni saa kumi na moja asubuhi. Hapa ninachofanya naandika ujumbe wako kama ifutavyo hapa chini

Habari yako  [JINA LAKO], nakukumbusha kuwa leo jioni saa mbili tutakuwa na kikao cha Cha pamoja kwa njia ya mtandao wa zoom. Nakutakia maandaalizi mema kwa ajili ya kikao, tafadhali hakilisha unawahi.

Halafu usisahau kutuma Ile laki tatu ya kozi tetu inayoendelea. Malipo yote yafanyike kwa namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

Enewei, huu ujumbe ninaweza kuuandaa Sasa na ukaja kwako baadaye leo jioni.  Au siku yoyote ya tukio.

Ninaweza kuandaa ujumbe huu na kuupanga uje kwako kwa kutumia APP inayoitwa DO IT LATER. Lakini Kuna mengine zaidi ya haya ambayo ningependa ujue kutoka kwenye hii APP.

Vifuatavyo Ni vitu Tisa ambavyo app inaweza kukusaidia kufanya

  1. KUKUKUMBUSHA KUPIGA SIMU
    Mfano, tumeongea Sasa hivi na umeaniambia nikupigie tarehe 2.2

Tukimaliza kuongea tu kwenye simu yakokitajitokeza kitu Kama hiki.

App inavyoonekana baada ya kuwa umempigia mteja. Unaweza kuamua kumtumia ujumbe au kuweka reminder kwamba ikukunbushe lini utampigia tena

Hapo nitachagua sehemu ya Call na Kisha nitapanga lini ningependa kuongea na wewe. Ambapo kwa upande wako Ni tarehe 2.2.2023

Hiyo tarehe ikifika , muda na saa tukivyokubaliana. App itanikumbusha nikupigie.

Wakati naendelea kuandika makala hii, app ilinikunbusha nimpigie Godius Rweyongeza. Hahah
kama aPp imekukumbusha umpigie mu, lakini unaona umebanwa huwezi kumpigia kwa wakati huo. Unaweza kubonyeza SNOOZE kisha ukachagua lini utampigia

2. KUTUMA SMS BAADAYE
Nadhani tangu mwanzo nimeliongelea hili. App hii inaweza kunisaidia kuandaa ujumbe wa kuja kwako tarehe, muda, saa na dakika ninayotaka au tulivyokubaliana.

3. KUTUMA SMS kwa mtu kwa kwa kurudia.
Tuseme kwa mfano, birthday yako ni tarehe 1.1. kila mwaka.
Halafu Mimi nataka kila tarehe 1 Januari niwe nakutumia ujumbe wa kukutakia kheri ya siku ya kuzaliwa. Lakini nahisi naweza kusahau, au sitaki niwe naurudia kuandika ujumbe huohuo kila mwaka. Naweza kuandaa ujumbe leo ambao utakuja kwako tarehe 1 Januari na utakuwa unakuja kwako kila mwaka tarehe moja Januari.

Ujumbe unaojirudia kila wiki. Sihitajiki kurudia kuandika ujumbe huu kila wiki. Ikifika jumapili, wenyewe unaenda hewani.

Kama umekuwa unapata changamoto ya ndugu kukwambia kwamba

Ooh unajua huwa hautupigiagi.
Ooh hata hutusalimii, siku hizi unalinga. Ngoja nikwambie kitu, kuanzia leo hawapaswi kukwambia huwasalimii.

Wachukue hao ndugu zako wote. Waweke kwenye grup maalumu, Kisha waandalie ujumbe wa kuwatakia wikendi njema na panga ujumbe huo uwe unaenda kwao kila jumamosi saa nne asubuhi. Umemaliza. Ujumbe huo utakuwa unaenda kwao kila jumamosi asubuhi maisha yako yote, mpaka siku utakapoamua kubadilisha hilo.

App inanikumbusha nimpigie kila alhamisi ya mwisho wa mwezi

Ni hivyo tu.

5. KUANDAA SMS NYINGI ZA KWENDA KWA MTU ILA ZIKAENDA KWA NYAKATI TOFAUTI
Unaweza kuandaa sms nyingi za kwenda mtu na ZIKAENDA kwa NYAKATI tofauti.

Mfano  unaweza kuandaa sms ya kwanza ya kwenda kwa MTU yenye ujumbe huu.

Habari, tunakushuru Sana kwa kununua simu mpya aina ya…. Siku ya leo.
Tumefurahi Sana kukuhudumia siku ya leo na tunakutakia kila kheri. Je, kuna Jambo lolote ungependa kuongea kuhusiana na huduma yetu? Kama unalo tafadhali usisite kutuambia, ahadi yetu Ni kwamba maoni utakayotoa tutayafanyia kazi.

Asante Sana na karibu kwa maoni.

Siku ya pili ukaandaa ujumbe wa kwenda kwa mtu huyuhuyu unaosema hivi

Habari ya tangu jana, Sina shaka umeshaanza kutumia simu yako uliyonunua kwetu sisi….. Unaoionaje?

Unaweza kuandaa jumbe nyingi na za kutosha kwenda kwa mtu yuleyule au kikundi cha watu. Mtu/watu unaweza hata kuwaandalia jumbe za mwaka mzima au hata miezi mitatu au minne ijayo.

Kwa kutumia app hii hutasahau birthday za wateja wako au watu wako wa karibu maisha yako yote.  Wewe unaweza kusahau Ila app haitasahau, itakuwa inawatumia jumbe na wataona unawajali kweli.

5. UNAWEZA KUITUMIA APP KAMA ALARM
Hapa app itakukumbusha majukumu yako ya muhimu ya kufanya

6. APP INAWEZA KUTUMA SMS KWENYE WHATSAP
Mimi nimeijaribu kwa upande wa WhatsApp. App haifanyi kazi vizuri hasa pale unapokuwa unataka kutuma jumbe kwa watu wengi, Ila kitu kimoja Cha uhakika Ni kwamba kama umeandaa ujumbe wa kwenda kwa mtu mmoja, utaenda. Ni uhakika utaenda.

Ila pia unapaswa kuwa mtandaoni.

7. APP INAWEZA KUKUONESHA WATU AMBAO IMEAHAWATUMIA UJUMBE NA AMBAO IMEAHINDWA KUWATUMIA
Kama kuna watu IMESHINDWA KUWATUMIA ujumbe, labda kutokana na kuwa simu yako ilikuwa imezima. App itakuonesha watu wa Aina hiyo. Na utaweza kuwarudia.

Ila pia app itakuonesha watu ambao wamekamilishwa kwa kutumiwa jumbe au kupigiwa.

App ikionesha missed call baada ya mtubkunipigia na kunikosa.

8. APP ITAKUSAIDIA KUWAKUMBUSHA WANAOKUDAI WAKUTUMIE HELA YAKO๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Natania tu japo ni ukweli.

9. APP INA UWEZO WA KUTAJA JINA LA MTU NA KUFANYA MENGINE MENGI.

Kama unatuma ujumbe kwa wengi na ungependa kila mtu atajwe jina lake. App ina huo uwezo.

Na mengine mengi sanaโ€ฆ

Ukitumia hii code wakati unatumia app. Itataja jina la mhusika kwenye ujumbe mfupi hata kama hukuandika jina hilo

Cha kufanya sasa. Ningependa nikushike mkono kwa kukupa maelezo ya kina juu ya namna ya kuitumia app hii. Sitaki upate shida hata kidogo. Nipo hapa kukusaidia.

NB: utapaswa kulipia 50,000/- ambapo utaelekezwa na kufunzwa kila kitu kuhusiana na app hii. Wewe mwenyewe utaipenda. Gharama utakayolipa kufundishwa ni ndogo kulinganisha na mengi utakayopata.

Karibu sana

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE

Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.

Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.

Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X