Aina tano za uwekezaji ambazo kila kila kijana anapaswa kufanya


Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

Habari ya siku hii ya kipekee rafiki yangu. Bila shaka unaendelea vyema kabisa,
Siku ya leo ningependa nikwambie Aina Tano za uwekezaji ambao unapaswa kuhakikisha umezifanya.

Huu ni uwekezaji ambao ukiufanya sasa hivi ukiwa kijana. Kadiri siku zinavyoenda wewe utavuna matokeo yake tu. Hakikisha unazitumia aina zote hizi za uwekezaji ukiwa bado kijana, maana ujana ni muda mzuri wa wewe kutumia kwa vitendo haya unayojifunza hapa ili umri ukisogea uanze kufurahia matunda ya haya tunayojifunza.

Kwanza ni uwekezaji kwako mwenyewe.
Yaani, hapa wekeza kwenye kujifunza na kupata maarifa sahihi ambayo yatakusaidia kusonga mbele.

Kuna vyanzo vingi ambavyo Kama kijana unaweza kutumia kupata haya maarifa, ila Mimi nakushauri sana uweze kutumia vifuatavyo.
Kwanza tumia VITABU. Penda kusoma VITABU maana humu kuna mengi utakayonugaika nayo.
Pili, jifunzee kupitia kozi mbalimbali za mitandaoni, ana kwa ana au vyuoni.
Jifunze kwa waliokutangulia na wazee. Mazuri yao yafanye zaidi. Majuto Yao yaepuke.

chagua mwalimu mmoja kwenye mtandao wa youtube kisha endelea kukjifunza kutoka kwa huyu mwalimu kila mara. Siku hizi kuna walimu wengi kwenye mtandao huu kiasi kwamba huwezi walau kukosa mwalimu mmoja ambaye unaweza kujifunza kwake.

Pili, wekeza kwenye kuanzisha na kukuza iashara Yako.
Hiki Ni kitu KINGINE muhimu ambacho kama kijana unapaswa kuhakikisha umekifanya.
Tunaishi kwenye ulimwengu wa pekee Sana tofauti na miaka mingine mingi ya nyuma. Leo hii Ni rahisi Sana kuanzisha Biashara tofauti na vile ilivyokuwa hapo zamani za kale.

Na hii fursa ambayo kila kijana anapaswa kuhakikisha kwamba anaitumia vizuri. Hata Kama umeajiriwa Sasa hivi, Anza kufikiria NAMNA ya kuanzisha na kuendesha Biashara yako.

Biashara itakupa kipato ambacho hakina ukomo. Maeneo mengine Yana ukomo wa kipato. Ongezeko la mshahara linategemea kudra za bosi, na hata haliongezeki kila mara. ila kwenye biashara kuna uwezekano wa wewe kutengeneza kipato chako bila ukomo. maana kadiri utakavyokuwa unaongeza mauzo kwenye biashara yako ndivyo ambavyo utakuwa unaongeza mauzo zaidi. kwa hiyo basi, nashauri uhakikishe unaanzisha biashara yako ambayo utaanza kuisimamia hata kama umeajiriwa rafiki yangu.

tatu, wekeza kwenye vipande vya utt

Mtu yeyote ambaye huwa ananitafuta na kuniambia kuwa ana hela na angependa kuanza kufanya uwekezaji, basi eneo la kwanza kabisa ambalo huwa namwambia wekeza hela yako ni Utt.. hii ni kutokana ukweli kuwa ni rahisi sana kuwekeza UTT kuliko lilivyo eneo jingine.

Ni rahisi pia kufuatilia mwenenedo wa mifuko ya UTT kuliko ilivyo rahisi kufuatilia mwenendo wa uwekezaji mwingine. Kwa hiyo, basi kama kuna uwekezaji ambao unapaswa kuufanya rafiki yangu, basi ni kuhakikisha kwamba unaanza kuwekeza UTT.

Nne, wekeza kwenye hisa

hili ni eneo moja la muhimu sana ambalo watu wengi wamekuwa hawaelewi. Soko la hisa kwa Tanzania limekuwa kwa miaka zaidi ya 20 sasa. lakini cha kushangza ni kwamba watu wengi wamekuwa hawalielewi na hivyo, kila mara kujikuta kwaba wanajiingiza kwenye uwekezaji ambao siyo sawa huku wakishindwa kufanya uwekezaji mzuri kama huu wa hisa.

Kama wewe huelewi uwekezaji wa aina hii, basi nashauri uweze kupata kitabu changu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. hiki ni kitabu cha kipekee sana ambacho kitakusaidia wewe kuanza kufanya uwekezaji kwenye soko la hisa. lakini siyo tu kwamba utalijua soko la hisa, bali utajifunza pia kwa kina suala zima la vipande na hatifungani.

Nakala ngumu ni 20,000/- tu. karibu sana uweze kujipatia nakala yako sasa hivi.

Tano, wekeza kwenye kuandaa kizazi kijacho

Moja ya kosa kubwa ambalo watu wengi wamekuwa wanafanya ni kupambana kwa nguvu zao zote kutafuta mafanikio ila huwa hawaweki nguvu kwenye kuandaa kizazi kijacho. hiki ni kitu ambacho rafiki yangu unapaswa kukifanyia kazi pia.

wakati unapambana kutafuta fedha na kuwekeza. unapaswa kuwafundisha wanao pia ili wajue kila kitu unachofanya. kwa jinsi hii utakuwa umefanya uamuzi mzuri sana wa kuandaa kizazi kijacho.

Rafiki yangu, anza kuandaa kizazi kijacho sasa.

Hakikisha umepata nakala ya kitabu cha MAAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Nakala ngumu ni 20,000/. Nakala laini 10,000/- tu. Karibu sana.

Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X