Kitu hiki kimoja kitakutofautisha wewe na watu wengine wenye kipaji kama cha kwako


KIPAJI NI DHAHABU
Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

Kama kuna kitu ambacho kinaweza kukutofautisha wewe na watu wengine wenye kipaji kama cha kwako basi kitu hiki siyo kingine bali ni kujifunza na kulielewa eneo ambalo unafanyia kazi kwa undani zaidi kuliko mtu mweingine yeyote. Yaani, unahakikisha kuwa taarifa zote za  muhimu kuhusana na kipaji chako unakuwa nazo na unazitumia kwa manufaa kuhakikisha kwamba unaweza kufika kule uhnaptaka kufika kwenye maisha yako.

Ukiwa na taarifa sahihi ni rahisi pia kufanya maamuzi bora (sound choice). Kwa hiyo, jitahidi kuhakikisha kwaba unalifanyia kazi. na njia ya wewe kulifanyia hili kazi ni kuhakikisha kwamba unajifunza kila mara kwa kusoma vitabu na kupitia majarida mbalimbali.

Kamwe usikifikie hatua ambapo utajiona kama vile umefika au umekamilika. Badala yake infanye kila dakika ambayo upo hapa duniani kuwa ni dakika yako ya kujifunza na kukielewa vizuri kipaji chako nje ndani, hili jambo hili rafiki yangu. ukilifanyia kazi baada ya siku nyingi sana ni wazi kuwa hili jambo moja tu litakufikisha mbali.

Kama huamini lijaribu kwa kuliweka kwenye vitendo ili uweze kuona maajabu yake na namna ambavyo litafanya kazi kwako. kumbuka kwamb alinafanya kazi kwa wengine, na litafanya kazi kwako pia.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X