Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Hiki kitu Kimoja Tu, Kitakufanya Utumie Kipaji Chako Kwa Viwango Vikubwa - SONGA MBELE

Hiki kitu Kimoja Tu, Kitakufanya Utumie Kipaji Chako Kwa Viwango Vikubwa


KIPAJI NI DHAHABU
Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

Leo asubuhi nimeamka na kuangalia video moja ambayo Kobe Braynat alikuwa akihojiwa na Patrick Bet-David. Moja ya swali ambalo Kobe Brayant aliulizwa ni kuwa ni msukumo gani ambao umekuwa ukimsukuma kujituma na kuhakikisha anakuwa jinsi anakuwa mchezaji bora. Kati ya mengi ambayo ameongea, kitu kikubwa amesema sitaki siku moja nije nianze kujuta kuwa ningeweza kuwa zaidi ya hapo. nataka nihakikishe kamba natumia uwezo wangu kwa viwango vya juu  kiasi kwamba hakuna siku hata moja ambayo nitakaa na kuanza kujuta kwa nini sikuweza kukamilisha jambo fulani ambao nilipaswa kuwa niweza kufanikisha.

Kobe Brayant

Rafiki yangu, sijui wewe upo kwenye hali gani kwenye maisha, na wala hata siui kipaji wala uwezo wako ni upi. Ila kitu kimoja cha kuhakika ni kuwa kama na wewe utayatumia haya maneno ya kobe Brayant kwenye maisha yako ni wazi kuwa unaenda kufika mbali na kufanya makubwa. Hii ndio kusema kwamba utajituma zaidi ya unavyofanya sasa hivi, siyo ilimradi tu umejituma, bali ukiwa unajua kuwa sitaki hata siku moja kuja kujutia.

Rafiki yangu, kama una nafasi ya kufanya makubwa leo hii, usiwe mzembe. Yafanye haoyo  makubwa.

Kama unaweza kufanya mazoezi leo, fanya hivyo.

Kama kuna wateja ambao unaweza kuwapigia simu leo hii ili waje kununua kwako, wapigie simu.

Kama kuna kitu unaweza kufanya, kifanye. Kwa vyovyote vile rafiki yangu, hakikisha kwamba, mara zote unajisukuma kuwa bora zaidi ya vile ulivyo sasa hivi.

Rafiki yangu kama kila mtu kwenye hii dunia akifanya kile anachopaswa kufanya kwa namna anavyopaswa kukifanya, ni wazi kuwa hii dunia itakuwa sehemu nzuri sana.

Nzuri kwelikweli!

Lakini ukweli ni kuwa hatuwezi kusubiri kila mtu afanye ndio na sisi tuanze…

Mimi na wewe tuanze. Tufanye kile tunachopaswa kufanya, wengine wataona na wataiga kutoka kwetu…

Timiza wajibu wako kama unavyopaswa kuutimiza.

Kama wajibu wako ni kupika chakula…kipike vizuri sana.

Kama wajibu wako ni kucheza..cheza

Kama wajibu wako ni kufundisha fanya hivyo

Fanya hivyo kiasi kwamba hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kufanya kazi unayofanya kwa viwanvgo unavyofanya. Kwa jinsi hiyo utakuwa umejitofautisha…


One response to “Hiki kitu Kimoja Tu, Kitakufanya Utumie Kipaji Chako Kwa Viwango Vikubwa”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X