Vitu vitano ambavyo hupaswi kuvipoteza kwenye safari yako ya mafanikio


Siku ya leo nataka nikwamie vitu viwili vikubwa sana ambavyo hupaswi kupoteza kwenye safari yako ya kufikia ndoto zako.

Kwanza usipoteze ndoto yako kubwa

Hiki ni kitu muhimu sana. ukipoteza ndoto zako maana yake unapoteza ile motisha na ile nguvu ya kukusukuma wewe kuweza kufanya kitu cha tofauti. Mara zote na sehemu zote hakikisha kwamba haupotezi ndoto yako kubwa uliyonayo.

Ndoto kubwa ndiyo inakupa motisha na nguvu ya kusongambele mara zote.

Pili haupaswi kupoteza kitu ambacho umetafuta kwa hela yako

Kama kuna kitu umekinunua kwa hela yako, hela ambayo umeitafuta kwa nguvu zako zote, usikubali kitu hiki ukipoteze kirahisi. Kitunze vizuri kwelikweli.

Tatu, usikubali kupoteza uaminifu ambao watu wanao juu yako

Kama kuna watu wanakuamini, usikubali kupoteza uaminifu huo kwa vizutu vya kijinga.

Nne, usikubali kupoteza mahusiano yako

Mahusiano yako ni muhimu kwa ajili ya mafanikio yako. Hakikisha unayapa kipaumbele mahusiano yako

Tano, usikubali kupoteza afya yako.

Afya yako ni muhimu sana kwako. hakuna hata mtu mmoja ambaye huwa anaweza kufanikiwa kwa viwango vikubwa bila ya afya. Ukifanikiwa huku ukiwa unaumwa, hutaweza kufurahia mafanikio hayo makubwa uliyokutana nayo.

/


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X