Sehemu sahihi ya kuweka akiba yako


Jana kwa nyakati tofauti watu watatu walinipigia na kuniuliza swali ambalo kwangu lilikuwa ni kama swali moja tu. japo kila mtu alikuwa na namna yake ya kulitoa hilo swali, ila kilichonishangaza ni kuwa hilo swali lilikuwa  na vipande vitatu muhimu ambavyo vinafanana.

  • Kwanza kila mtu alitaka kuweka akiba sehemu nzuri
  • Sehemu ambayo haina makato
  • Sehemu ambapo ataweka kwa muda mrefu
  • Sehemu ambapo atapata fedha yake ikiwa imeongezeka zaidi ya alivyoiweka mwanzoni

Sasa watu hawa watatu wamenifumbua macho na kunionesha kuwa pengine na wewe ungependa kuijua sehemu ya aina hii. Ndio maana siku ya leo nimeona, siyo vibaya, wacha nikuandalie makala ya kina inayoeleza hili suala ili na wewe uweze kuliewa.

Kwanza unaweza kuwa unajiuliza, hivi kweli sehemu ya aina hiyo ipo kweli?

Yaani, kwamba ipo sehemu ambapo unaweza unaweza ukaweka akiba yako kwa usalama, haina makato kwa kipindi chote ambacho umeweka akiba, na baadaye ukataka kuitoa, ukaitoa ikiwa imeongezeka zaidi ya vile ulivyokuwa umeiweka? Sehemu ya aina hii ipo kweli?

Jibu ni ndio sehemu ya aina hii ipo ila haiwezi kuwa benki. Kwa sababu benki mara zote kwenye akaunti yako huwa kuna makato pale unapoweka fedha yako, benki huwa wanakukata kukutunzia fedha yako. Kwa hiyo sehemu ya aina hii haiwezi kuwa benki.

Lakini kabla hujazilaani benki, naomba unielewe kwa kitu kimoja kwanza na cha msingi sana. Mimi nina akaunti ya NMB, kama sijakosea akaunti hii inaitwa akaunti ya mwanachuo au akaunti ya mwanafunzi. Kwenye akaunti hii huwa hawakati fedha pale unapoweka fedha  yako huku. Fedha yako huwa inaendelea kubaki kama ilivyo hata kama ikikaa kwa muda mrefu, labda makato ni pale tu ambapo huwa natoa fedha. Labda kama sera za uendeshaji wa akaunti hii zimebadilika. Ila kama hazijabadilika, basi hii inaweza kuwa akaunti nzuri kwako. ubora ni kwamba NMB wanaruhusu ufungue akaunti hii hata kama wewe siyo mwanafunzi.

Lengo lao ni kusaidia watu kujijengea utaratibu wa kujiwekea akiba. Na mimi nawaunga mkono. Kwa nini? kwa sababu tafiti nyingi zimeonesha kuwa watu wenye akaunti ya benki, walau huwa wanajiwekea akiba ukilinganisha na watu ambao hawana akaunti ya benki. Sasa kama wewe hauna akaunti ya benki, nadhani unaweza usiwe na akiba yoyote ile mfukoni, au uongo?

Enewei, tuachane na hilo, maana tangu mwanzo niliahidi kukwambia eneo unapwoeza kuweka akiba na baadaye ukaitoa ikiwa imeongezeka ila siyo benki. Halafu eti bado naendelea kuongelea masuala ya benki…

Sasa baada ya kusema hayo, naomba tuone eneo ambapo

  • unaweza kuweka fedha yako,
  • Sehemu ambapo hakuna makato
  • Sehemu ambapo utaweka kwa muda mrefu
  • Sehemu ambapo utapata fedha yake ikiwa imeongezeka zaidi ya ulivyoiweka mwanzoni

Hiki ni kitabu kizuri sana ambacho unapaswa kusoma. Gharama yake ni elfu tano tu.

Walau sehemu hii siyo benki.

Sehemu yenyewe ni kwenye akaunti za uwekezaji wa pamoja za UTT

UTT ni taasisi ya kiserikali iliyochini ya wizara ya fedha ambayo inawakutanisha wawekezaji wote wenye mitaji midogo na mikubwa na kuwasaidia kuikusanya hiyo mitaji, kisha kuiwekeza sehemu salama.

UTT imekuwa inafanya kazi hapa nchini karibia mwaka 20 sasa, ila cha kushangaza watanzania wengi hawana uelewa juu ya UTT na hata wengine hawajawahi kusikia habari za UTT.

Ukiweka fedha yako UTT inakuwa sehemu salama, maana fedha yako zinakuwa chini ya taasisi ya kiserikali, lakini sambamba na hilo fedha yako inakuwa chini ya watalaamu ambao wataiwekeza sehemu salama ambazo wao wanajua. Kitu hiki kinafanya uwekezaji wako unakuwa salama na hata baadaye uwekezaji unakuja ukiwa na mrejesho mzuri.

UTT AMIS kama inavyofahamika, ina mifuko sita ya uwekezaji ndani yake. Mifuko hii imeanzishwa kwa dhana na malengo tofauti kulingana na aina ya mfuko.

Mfano mfuko wa umoja ambao pia ni mfuko mkongwe kwenye mifuko yote ya UTT, Ebu angalia picha hiyo  hapo chini

Mfuko mwingine ni mfuko wa ukwasi ambao maelezo yake ya mafupi haya hapa

Kwa kuwa hii makala lengo lake siyo kueleza mifuko yote ya utt kwa undani, nimedokeza hiyo mifuko mwili tu kwa kuwa ndiyo nataka kuiongelea zaidi kwenye makala ya leo.

Kwa hiyo, kama una fedha zako na ungependa kuiwekekeza basi nashauri uweze kuiweka kwenye mfuko mmojawapo hapoo juu. Aidha mfuko wa umoja au mfuko wa ukwasi.

Ukiweka fedha yako kwenye mfuko mmojawapo hapo juu, ni uhakika kuwa baada ya muda fedha yako itakuwa imeongezeka, maana mifuko hii imekuwa na mrejesho mzuri kila mwaka. Ambapo kwa wastani tangu kila mfuko umeanzishwa umekuwa na mrejesho wa asilimia 13.5. Hii maana yake kwamba ukiweka fedha yako huku, kwa kila kiasi ambacho utaweka huku, unapata ongezeko la silimia 13.5.

Ikumbukwe kwamba huo ni wastani. Hii ndio kusema kwamba kuna miaka ambapo uwekezaji huo unaweza kuwa juu kama ulivyoona hapo juu. Na kuna miaka ambapo mrejesho huu unaweza kuwa chini.

Kwa hiyo rafiki yangu, kwa kuwa leo nilitaka kukwambia sehemu nzuri ya kuwekeza fedha yako, basi naona lengo lengu kama nimeweza kulifikia.

Kazi yako ya fuanya siku ya leo.

Nenda kafungue akaunti ya Utt, ubora ni kuwa unaweza kufungua akaunti hata kwa simu yako.

Bonyeza *150*82# uanze kufanya hivyo.

Au unaweza kufungua akaunti kupitia aplikesheni yao iliyo kwenye playstore. Inaitwa UTT AMIS

Kwa maelezo zaidi ya ndani kabisa, nashauri uweze kupata ebook yangu inayoitwa MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE pamoja na ebook nyingine inayoitwa MAAJABU YA KUWEKA AKIBA. Hizi ebooks hizi zitakufaa sana rafiki yangu.

Kila ebook gharama yake ni 5,000/- tu. Ona huyu mwenzako aliyekisoma hapa anavyosema


One response to “Sehemu sahihi ya kuweka akiba yako”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X