Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Jinsi Ya Kupata Wazo La Kuandika Kitabu - SONGA MBELE

Jinsi Ya Kupata Wazo La Kuandika Kitabu


Kuna watu huwa wanafikiri labda ili kuandika kitabu basi unapaswa kuwa na wazo la kipekee sana ambalo halijawaji kutokea Hapa duniaani.

Siyo kweli. Unaweza kuwa na wazo la kawaida tu, Ila wazo Hilo ukalikuza na kulifanya kuwa kitabu kizuri sana. Bado huamini!

Mfano kwenye picha ya kawaida tu ambayo watu wanachukulia poa wewe unaweza kupata kitabu kizuri sana.

Nakumbuka juzi nikikushirikisha kuhusu mama aliyenunua kitabu changu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU wakati wa maonesho ya nanenane.

Wakati namtumia kitabu hiki kwa WhatsApp niligundua kitu kimoja. Na kitu hiki ilikuwa Ni picha aliyokuwa ameweka kwenye profile yake. Niliipenda ile picha, kiasi nikamwambia hii picha ina kitabu ndani yake.

Unaweza kuiona picha yenyewe hapa

Akiwa bado haamini amini Kama hiyo picha inaweza kutoa kitabu, nilichukua karatasi na kalamu na kuanza kuandika kichwa Cha kitabu. Nikamwambia kutoka kwenye hii picha kichwa Cha kitabu kinaweza kuwa hiki.

Baada ya hapo nikashuka chini na kuandika UTANGULIZI. Nikakwambia kwenye utangulizi andika hiki na hiki.

Kisha nikaendelea mbele kwenye sura ya kwanza mpaka ya nne.

Kisha nikakwambia sura nyinginezo utatafuta mwenyewe.

Hivyo, ndivyo waandishi huwa tunapata vitu vya kuandikia.

Kwa kitu chochote unachokiona kuna kitu chaa kuandika ndani yake, itategemea tu na mamna unavyokiangalia kitu.

Tukichukulia mfano wa mti.

Daktari akiona mti, anaona dawa ndani yake.

Mwimbaji akiona mti, anaona wimbo ndani yake.

Mpishi akiona mti anaona kuni

Wakati msafiri akiona mti, anaona kivuli na sehemu ya kupumzila

Fundi seremala kwenye mti huohuo ataona kitanda Safi kabisa.

Kumbuka mti ni uleule Ila kile watu wanachoona kwenye ule mti ndio kinatofautiana.

Na kwenye uandishi hivyohivyo, unaweza kuona kitu ukakichukulia kawaida. Mwingine akaona kuna Kuna kitabu ndani yake.

Ukiwa Kama mwandishi jitahidi kupata walau wazo moja la kuandika kwenye kila kitu unachokiona au watu unaokutana nap.

Bado unaona haiwezekani tu. Sikiliza, nenda kasome kitabu changu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU. Hiki kina kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uandishi wa vitabu na Makala.

Halafu kinauzwa elfu tano tu. Na unatumiwa kwa simu au baruapepe yako.

Yule mama wakati anaendelea kukisoma akisema haya

Mambo ndiyo hayo. Lipia elfu tano sasa kwa 0684408755jina Ni GODIUS RWEYONGEZA

Godius Rweyongeza

0755848391

Morogoro-Tz


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X