Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Mwaka Huu Ni Wangu Kufanya Makubwa - SONGA MBELE

Mwaka Huu Ni Wangu Kufanya Makubwa


Kila mwanzoni mwa mwaka watu wengi huwa wanaweka malengo makubwa ya kufanyia kazi. utasikia mtu anasema kwamba mwaka huu ni mwaka wangu wa kufanya makubwa. utasikia mwingine anasema kwamba mwaka huu lazima tu nifanye makubwa. ila sasa cha kushangaza

Unakuta kwamba siku zinakuwa zinazidi kupita kiasi kwamba inafikia hatua huyo mtu anashindwa kufanyia kazi lengo lake la mwaka.

Kinachokwamisha watu wengi ni kwamba wengi wanaweka mipango na malengo makubwa ila wanakuwa hawachukui hatua kuhakikisha kwamba wameweza kufikia malengo na ndoto zao.

Hivi wewe ni miongoni mwa hawa watu rafiki yangu?

Ninachotaka kukwambia ni kwamba mafaniko makubwa huwa hatatokei mara moja tu yaani, mwishoni mwa mwaka. Badala yake ni mchakato wa vitu vidogovidogo unavyokuwa unafanya kila siku.

Hivi vitu vidogo vidogo unavyofanya kila siku, baadaye vinaunganika na kutengeneza kitu kikubwa.

Ebu fikiria kila siku ukiwekea utaratibu wa kufanya kitu hata kama ni kidogo, ni uhakika kuwa mpaka mwisho wa mwaka lengo lako lililokuwa kubwa utakuwa umelisogeza mbali pangine hata kulifikisha na kupita makadirio yako.

Hiki kitu hakiwezi kukushinda.

Kwa siku zilizobaki kumaliza mwaka huu. anza kufanya kitu hata kama ni kidogo tu kila siku kuelekea kwenye lengo lako kuu. Kila siku fanya kitu hata kama ni kimoja tu. uhakika ni kuwa baada ya mwaka utakuwa umeweza kufanya siyo hicho kitu kimoja, badala yake utakuwa umeweza kufanya makubwa.

Haijalishi umeajiriwa

Uko bize sana au

Bosi wako anakubana.

Huwezi kukosa hata dakika kumi na tano tu kwa siku za kufanya kitu cha kwako hata kama ni kidogo. rafiki yangu, endelea kuipambania ndoto yako mpaka kieleweke. Usikubali kurudi nyuma kwa namna yoyote ile.

Bila kuongeza la ziada, naomba niishie hapo……..

Kitu kimoja cha ziada kuhusu kitabu cha nguvu ya vitu vidogo kuelekea mafanikio makubwa.

Najua hapa kwa vile nimeongelea kitabu unaishia hapa na kucha kusoma zaidi. hahahaha

Unaanza kufikiria huyu jamaa hapa anaongelea pesaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Enewei, hiki kitabu ni muhimu kwako rafiki yangu…..

Ni muhimu mno.

Kama kuna kitabu kimoja unachopaswa kusoma mwaka 2022 basi ni hiki. Sikisifii kwa sababu nimekiandika mimi bali kwa sababu waliokisoma wengine wamethibitisha hilo.

Ebu ona maoni haya hapa chini

Umeona ee….

Sasa, kitabu hiki ni 20,000 tu za kitanzania au dola kumi (10) kama upo nje ya nchi.

Utaongeza gharama kidogo za usafiri kulingana na sehemu ulipo nami nitakutumia hiki kitabu. Ninatuma popote pale duniani.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X