Hiki kitu ndicho kinafanya watu wanakuchukulia poa


Umewahi kujiuliza kwa Nini watu wengi wanakuchukulia poa.

Kuna sababu nyingi zinaweza kuwa zinasababisha hiki ila sababu ya kuu unaweza kuwa Ni wewe umewafanya wakuchukulie poa.

Inawezekana kuna kipindi ulitakiwa kutoa huduma fulani kwao ila hiyo huduma hukuitoa vizuri.

Inawezekana ulijishusha viwango kwa kutaka kupata kitu fulani wakati hukupaswa kujishusha

Na pengine inawezekana ni kwa sababu ya mtazamo  wa MTU tu. Yaani, akiaakuangalia anakuchukulia poa.

Unachopaswa kujua ni kuwa siyo kazi yako kuanza kuwaambia watu kuwa msinichukulie poa.

Badala yake nenda kafanye kazi. Acha matendo yako yaongee kiasi kwamba hata wale wanaokuchukulia poa waanze kuona thamani yako.

Anza leo.
Chukua hatua hata Kama ni ndogo kwa ajili ya kuongeza thamani yako.

Kazi utakayofanya, ifanye kwa ubora.
Ongeza kipato chako
Kuwa bize na maisha yako badala ya kufuatilia maisha ya watu wengine.
Acha kutuatilia maneno wanayosema wengine.
Nguvu zako zote ziweke kwenye kazi.

Kwa jinsi hii itakuwa umekataa kuchukuliwa poa kwa vitendo na siyo kwa maneno. Endelea kupambana, watakuona ukivuka ng’ambo.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X