Sala Muhimu Unayopaswa Kusali Kila Siku. Inaleta Matokeo Ya Haraka


Kupata vitabu hivi wasiliana na 0755848391

Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweli. Najua umekuwa ukisali sala mbalimbali kwa siku nyingi.

Ila leo ninataka kukwambia sala moja tu ambayo hujawahi kusali, na sala hii siyo nyingine bali kumwomba Mungu akupe usikivu.

Uwe msikilizaji mzuri kuliko kuwa muongeaji mzuri.

Tuna mdomo na masikio mawili. Ikimaanishabkuwa tunapaswa kuwa wasikilizaji wazuri kuliko kuwa waongeaji. Ila kinachotokea Ni kinyume chake. Unakuta MTU Ni muongeaji mzuri halafu hasikilizi.

Sasa kuwa kinyume. Kuwa msikilizaji. Hii itakupa faida nyingi sana, maana kwanza watu wanapenda kusikilizwa.
Lakini pia unaposikiliza unampa mtu nafasi ya kujieleza zaidi na hivyo kumfahamu au kufahamu tatizo lake kiundani.

Kuanzia leo, jipe jukumu la kuwa msikilizaji mzuri. Utajua mengi kupitia kusikiliza kuliko kuongea.

Kwa hiyo sala yako iwe hivi: Ee Mungu naomba unifanye niwe msikilizaji mzuri kuliko kuwa muongeaji. Amina


Kila la kheri
Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli
Godius Rweyongeza
0755848391


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X