Unafanyaje ili kupata mbia sahihi wa biashara


Leo nataka tuongeelee kuhusu ubia wa biashara. Ikiwa ni moja ya kitu muhimu sana kwenye biashara ambacho unakihitaji hasa kama umelenga kufika mbali. Ubia kwenye biashara unakutanisha watu wenye ujuzi, elimu na hata fedha ambapo wanaungana kutengeneza kitu kimoja. Kwenye biashara ubia ni muhimu sana hasa kama unataka kufika mbali.

Kitu kikubwa unachohitaji kujua kuhusu biashara ni kwamba biashara ni mchezo. Na kama mchezo, una kanuni na taratibu zake, hivyo unapaswa kuzifuata hizi kanuni na taratibu za biashara au kwa manufaa yako, au la unapaswa kuzivunja kwa hasara yako pia.

Sasa vifuatavyo ni vitu muhimu unavyohitaji kujua kuhusu mbia wako.

Kwanza unahitaji kumjua mbia wako vizuri.  Hiki kitu ni muhimu sana kwenye biashara kutokana na ukweli kuwa huyu mtu unaenda kufanya naye kazi kwa muda mrefu.Ni mtu ambaye ambaye mnaenda kujenga kitu kikubwa, hivyo, unahitaji kumjua vizuri huyu mtu wako

Pili fahamu kuwa mbia wako siyo lazima awe mtu mwenye fedha nyingi sana, siyo mtu mwenye ushawishi mkubwa, siyo mwanasiasa, mwenye jina kubwa au mtu wa aina hiyo. Mbia wako ni mtu kama wewe ambaye mnaweza kuendana kwenye kufanyia kazi kile unachofanya. Kikubwa awe ni mtu ambaye mnaweza kuendana kwenye biashara yenu.

Tatu, Mbia wako awe na ujuzi ambao unaweza kujazilia kwenye kile ulichonacho wewe na yupoo tayari kufanya kazi kwa bidii, naam bidii sana.

Nne, Usivunje makubaliano uliyowekeana na mbia wako hata kama utagudua kuwa ule ubia mlioweka, kuna hila fulani zilifanyiaka wakati mnaweka huo ubia. Badala ya kwenda kinyume na makubaliano, utapaswa kumwita ili mkae chini na kuweka sawa kile ambacho unaona kwamba hakijakaa sawa.

Kwa leo nimeona nikushirikishe hayo mambo machache kuhusu ubia na namna ambavyo unaweza kuutumia ubia kwa manufaa.

NB. Tumeanza kusambaza vitabu vya jinsi ya kufikia ndoto zako. nakala ngumu (hardcopy). Kitabu hiki kinatumwa popote pale ulipo Afrika Mashariki. Hakikisha unapata nakala yako leo hii kwa bei ya punguzo. Yaani badala ya 20,000/- unapata nakala yako kwa 15,000/- tu. Mwisho wa kupata kitabu kwa bei ya oda ni tarehe 20. Jionee mwenyewe chini hapa muda uliobaki kupata nakala kwa bei hiyo hapo chini

[wpcdt-countdown id=”5798″]


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X