THE SIMBA MENTALITY


Karibu sana kwenye makala ya leo. Ni makala ndefu kidogo. Kwa wale wasiopenda kusoma vitu virefu sana hii ya leo inaweza isiwe makala ya aina yako. Ila wale ambao wanapenda kuzama ndani na kujifunza vitu kwa kina vilivyotafitiwa na kutafitika, basi vuta kiti maana unachoenda kujifunza hapa ni kitu kikubwa sana.

Kwa siku nyingi sana nimekuwa nikipanga kuandika makala yenye kichwa hiki cha The Simba Mentality. Nadhani mara ya kwanza kupata wazo la aina hii, ilikuwa kipindi nasoma wasifu wa Kobe Bryant, unaoitwa The Mamba Mentality.

Kwenye wasifu huu, Kobe Brayant ameeleza safari yake kimichezo tokea akiwa shule ya upili (high school) mpaka anastaafu. Ni kitabu kizuri sana. na sote tunajua kwamba Kobe alishatangulia mbele ya haki, tangu mwaka 2020, hivyo, kitabu hiki, ndio kimebaki kama alama ya kumkumbuka na kujifunza kutoka kwake, sambamba na video na mafunzo kadhaa yanayozunguka mtandaoni. Unaweza kutazama video ya uchambuzi wa kitabu chake kwenye channel yangu ya youtube hapa chini. hakikisha umesubscribe pia.

Nakumbuka mwanzoni nilipanga kabisa niandike kitabu kinachoitwa The Simba Mentality, ila sasa leo nimeona kwanza nikudoletee makala hii. Kama utaipenda, unaweza kuniambia niiongezee nyama zaidi, ili pengine nitengeneze kitabu.

Siku siyo nyingi kwenye mtandao wa youtube nilikutana na video iliyokuwa ikiwaonesha simba waliokuwa njiani. Kilikuwa ni kikosi kikubwa cha Simba, ambao walilala katikati mwa barabara na hivyo, kusababisha magari yaliyokuwa yanatokea kila upande kukwama kwa muda, kila mwenye gari alijitahidi kupiga honi kadiri alivyoweza ili labda kuwaongopesha hawa wanyama na kuwafanya wasogee, ila hakuna mnayama hata mmoja ambaye alitoka.

Sote tumewahi walau kisikia stori za simba. maana nikisema, sote tumewahi kumwona simba ana kwa ana, hapa tutaanza kutafutana., labda kumwona kwenye royal tour tu

Simba ni mnyama wa mwituni ambaye pia anajulikana kama mfalme wa nyika. Anafahamika kwa ukali wake na uwezo wake maridadi wake kuwinda. Mpaka tulipokuwa wadogo tulikuwa tumamwimba,

Tulikuwa tunaimba hivi

KIONGOZI: Watoto wanguu ee

WOTE: Ee

Kiongozi: Mimi mama yenu

WOTE: Ee

Kiongozi: Sina nguvu tena

WOTE: Ee

Kiongozi: Za kuua simba

WOTE: Ee

Kiongozi: Simba ni mkali

Wote: Eeh

Kiongozi: Aliua mama,

WOte: Ee

Kiongozi: Akaua mama

Wote: Ee

Kiongozi: Sasa kimbieni

Wote: Makelele ya shangwe……

Naam, nimekurudisha utotoni ee.

Huyu ndiye simba. Nakumbuka nyumbani jina maarufu la mbwa, ni simba. Mbwa wengi wa nyumbani ambao nimewahi kuwaona majina yao wanaitwa simba. Hii yote ni kwa sababu kila mtu anapenda mbwa wake awe na ukali kama simba. Na hata siku hizi kuna watu wanajiita majina ya wanyama.

Kama nilivyokudokeza tangu mwanzo kuhusu kitabu cha Kobe Brayant ambaye pia alikuwa anajiita Black MAMBA. Watu wengine wanajiita majina ya wanyama kama yeye, likiwemo jina la simba, chui,…

Nadhani kila mtu anajaribu kutafuta jina ambalo litamtambulisha vizuri, kulingana na tabia alizonazo. Ila jina SIMBA, nadhani wengi wanalipigania.

Sidhani kama kuna mtu ambaye anapenda aitwe panya, kunguru, au nguchiro. Hii yote ni kuonesha kwamba kila mtu anataka kuonekana kwamba ana ustadi wa hali juu kwenye kile anachofanya.

Sasa simba ana kitu gani cha kipekee ambacho kinamtofautisha na wanyama wengine.

Zifuatazo hapa chini ni sifa muhimu za simba ambazo zinamfanya kuwa mfalme wa nyika.

Fedha ya kupata ebook yenye andiko lote la THE MAMBA MENTALITY utaituma kwa namba 0755848391 Jina ni GODIUS RWEYONGEZA


One response to “THE SIMBA MENTALITY”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X