Kitu Kimoja Cha Kufanya Kama Hauna Fedha Sasa Hivi



Chukua hatua. 


 Tafuta bidhaa yoyote unayoweza kuuza. Nenda kwa watu uuze. Unachopaswa kujua ni kuwa fedha zako wanazo watu. Ila huwezi kwenda kwa watu na kuwalazimisha wakupe hiyo fedha. Huo utakuwa wizi au unyang’anyi. Njia bora ya wewe kupata fedha kwa watu ni kuwapa hao watu huduma au bidhaa wanayotaka.


Zig Ziglar aliwahi kunukuliwa akisema; unaweza kupata chochote unachotaka kama utawasaidia watu kupata kile wanachotaka.


Huwa napenda kuwaambia watu kuwa matajiri nao wanaomba fedha. Ila hawaombi kama ombaomba wa mtaani, wenyewe wanaomba fedha kwa kukuletea kitu unachotaka. 


Na wewe anza kuomba fedha kitajiri. 
Kumbuka: unaweza kupata chochote unachotaka kama utawasaidia watu kupata kile wanachotaka.
Kila la kheri.

subscribe pia kwenye channel yangu ya YouTube.

Umekuwa nami rafiki yako, Godius Rweyongeza. Tuwasiliane kwa 0755848391

For booking: songambele.smb@gmail.com au songambele@songambele.com


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X