Kama Wewe Ni Shabiki Wa Yanga au Simba Hakikisha Umesoma Hapa


Jana ilikuwa ni mechi ya simba na Yanga. Ni moja ya mechi zinagusa watu wengi kwa hapa Tanzania. Kuna watu hawashabikii timu yoyote ile hapa duniani, isipokuwa simba au Yanga.

Sasa leo nilikuwa nikifikiri kuhusu hili nikawakumbuka rafiki zangu ambao wanahangaika kuandika vitabu. Wanahangaika na hawajui kitu gani wanaweza kuandikia. Nikasema ngoja leo niwaambie kitu.

Kama wewe unajiuliza ni shabiki wa yanga au simba na unajiuliza ni aina gani ya kitabu unaweza kuandika. Ebu kuanzia leo hii tuandikie kitabu kuhusu ushabiki wako na timu yako.

Ebu tuambie kwa nini unaipenda Simba au YANGA. Ilikuwaje mpaka ukaipenda simba au Yanga.

Kwa nini mpaka leo hii wewe unaendelea kuishabiki hii timu

Nini mpango wako kwa siku za mbeleni juu ya hii timu?

Je, ushabiki wako nje ya hizi timu ukoje?

Je, huwa unatumia kiasi gani kwa mwaka kwa ajili ya hii timu? Iwe ni kuangalia mechi, kutoa michango n.k

Kuna mambo mengi san asana ya kuandika kuhusu simba na yanga tu, ambayo ni kitabu tosha.

Nadhani kitabu chako unaweza kukiita. MIMI NI YANGA AU SIMBA DAMU.

Au USHABIKI WANGU DHIDI YA SIMBA au YANGA NI MPAKA KIFO

Au hata unaweza kusema NIMEFUNGA NDOA NA SIMBA au NIMEFUNGA NDOA NA YANGA. hahah

Ni mapendekezo tu. lakini hii yote ni kutaka kukuonesha kwamba unaweza kuandika kitabu kuhusiana na hili nab ado tukasoma kitbu chako.

Kwa hiyo kuanzia leo hii usije ukasema kwamba mimi sina cha kuandika na wala sijui nianzie wapi. Aznia hapohapo.

Tukutane siku nyingine

Kwa maswali, maoni au booking: songambele.smb@gmail.com

Umeshapata nakala yako? Wasiliana na 0755848391


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X