WATU WANASEMAJE KUHUSU KITABU CHA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI?


MIMI NAMFAHAMU GODIUS

Ninamfahamu Godius si tu kwa kupitia maandishi yake bali kwa kupitia maisha yake. Jinsi anavyoishi ni darasa tosha la mtu yeyote mwenye nia ya kufanikiwa.

Nilipoanza kusoma kitabu hiki sikukoma kuacha kwani kimegusa maisha yangu na baadhi ya mambo niliyoyapata humo nimeanza kuyafanyia kazi na nimeanza kuona maajabu makubwa.

Unataka kuwa mbunifu? Soma kitabu hiki. Unataka kuwa kinara kwenye kipaji chako? soma kitabu hiki?

Unataka kuwa kiongozi kwenye maisha yako? Soma kitabu hiki.Unataka maisha yenye furaha na ya kuacha alama? Majibu yote yanapatikana humu kwenye Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni.

Imani yangu ni kwamba unaweza kuanzia hapo ulipo na kufika popote ili mradi akili yako umeipa ruhusa. Kila mtu amezaliwa mshindi, hakuna aliyekuja duniani kuwasindikiza wengine. Wewe ni wa tofauti, kuwa wewe, acha kujilinganisha na wengine, kujilinganisha kunabagua.

Asante sana Godius Rweyongeza kwa kitabu hiki kinachotafakarishi, kinachotia hamasa na kinachotupa dira ya kuishi maisha kwa utimilifu.

Edius Katamugora Mtunzi Yusufu Nina Ndoto


MWANDISHI KATUMIA LUGHA NYEPESI KUONGEA MAMBO MAKUBWA YA KIMAFANIKIO

Kila binadamu ndani kabisa ya moyo wake ana tamanio kubwa la kufanikiwa, yaani ikutoka ngazi ya chini kwenda ngazi ya juu katika Nyanja mbalimbali za Maisha. Kwa lugha nyepesi “Kutoka sifuri mpaka kileleni.

Lakini changamoto kubwa inayowakabili watu wengi ni njia sahihi za kupita au kanuni za kufuata ili kufikia hatima hiyo.

Mwandishi Godius Rweyongeza amejaribu, kwa kadri ya uwezo wake, kutumia lugha nyepesi na mifano halisi ya kumsaidia mtu kuweza kufuatana kutimiza azma ya mafanikio. Amezungumza kiundani jinsi ambavyo binadamu anaweza kutumia uwezo wa utashi aliopewa na Mwenyenzi Mungu katika kujiletea maendeleo binafsi katika Nyanja zote za Maisha.

Ni matumaini yangu kuwau naposoma kitabu hiki utaweka katika matendo yale yote utakayojifunza ili uweze kupata matokeo bora yatakayokuwa chachu chanya kwa wengine pia.

Nakutakia usomaji mwema na utekelezajiwa yale yote utakayojifunza.

Anthony Luvanda

Mjasiriamali na Mhamasishaji.

Anzisha Biashara, Endesha Na Kuza Biashara Yako, Ufikie Ndoto Zako


KAMA HUJUI NAMNA YA KUWEKA MALENGO, MWANDISHI AMEKUSAIDIA KUFANYA HIVYO KWENYE KITABU HIKI.

“Usipowaambia watu kuhusu mafanikio yako bila shaka hakuna atakayekuja kuyajua” Donald Trump

Acha Mimi nikuambie mafanikio yangu ili uyajue kupitia kitabu hiki cha kutoka sifuri hadi kileleni. Ukitaka kujua mafanikio yako anza kusoma kitabu hiki cha kutoka sifuri hadi kileleni. Kwani utagundua uwezo mkubwa wa kufanikiwa ulioko ndani yako, kwanini unajichelewesha kupata ushindi ambao uko ndani yako?

Kama hujui kabisa namna ya kuweka malengo hatua kwa hatua ili yaweze kukusaidia kutoka sifuri hadi kileleni, basi mwandishi na mtaalamu wa kilimo cha bustani (Horticulture) Godius amekusaidia kufanya kazi hiyo kwenye kitabu chake cha kutoka sifuri hadi kileleni.

Ukiona mtu amefanikiwa kutoka sifuri hadi kileleni jua kuna siri kubwa nyuma ya ushindi.

Ninapendekeza kila anayetaka kufanikiwa, na hajawahi kusoma kitabu chochote kile basi kitabu hiki ni cha lazima kusoma kwa mtu makini anayeanzia chini kabisa na kutaka kufikia kileleni. Ni kitabu kinachokuonesha  mchakato wa mafanikio kutoka sifuri hadi kileleni.

Kila la heri rafiki yangu katika usomaji wa kitabu hiki.

Mwl. Deogratius Kessy

Mwalimu, Mwandishi na Mjasiriamali.

http://kessydeo.home.blog


HIKI NI KITABU CHA KARNE YA 21

Kujitoa bila kujibakisha, kusimamia jambo bila ya kurudi nyuma,  pamoja na kugundua uwezo wa ajabu aliouweka Mungu ndani yako, hivi vitakusaidia kufika hapo unapotaka kufika.

Kitabu hiki kimeanza kwa kwanza kwa kumsukuma mwandishi ujiuliza kwa nini wengine wamefika walipokusudiwa na wengine hawafiki, majibu yake yakiwa ndani ya kitabu hiki, yanagusa kuhamasisha na kufundisha, hiki ni kitabu cha karne ya 21,hivyo kila mmoja anapaswa kukisoma.

Mwalimu Adebert Chenche

Mwenyekiti wa taasisi ya VIPAWA LINK ASSOCIATION


NI KITABU CHENYE MAARIFA MENGI SANA.

Ni kitabu chenye maarifa mengi sana. Kwa uhakika atakayekisoma na kuyafanyia kazi ataweza kupiga hatua kubwa katika kutimiza malengo yake

NTANGEKI NSHALA



Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X