Uwezo mkubwa ulio ndani yako


Leo nimeikumbuka sana siku nilipoenda kumtembelea rafiki  yangu. Kama ulivyo utaratibu wetu waafrika. Alinikaribisha kwa kuleta vinywaji pale mezani.

Lilikuwa Jambo la furaha sana kukutana na hiyo rafiki yangu na stori zilianza bila kuchelewa, huku tukikumbushana baadhi ya mambo yaliyowahi kutokea siku za nyuma na hata kutaniana.

Wakati stori zinazidi kukolea, glasi mojawapo pale mezani ilidondoka chini na kupasuka.

Hili hambo lilinifanya nitafakari sana, ukizingatia zile glasi zilikuwa bado mpya kabisa.

Nilibaki najisemea kimoyomoyo kwamba hii glasi imeharibika ikiwa bado na uwezo makubwa ndani yake ambao ulikuwa haujatumika.

Hiki kitu kunatokea kwa watu wengi pia..
Kuna watu wengi wenye uwezo mkubwa ila huwa hawautumii hata kidogo. Uwezo huu wa kipekee ungeweza kuinufaisha dunia…

Pengine hata wewe uko kwenye hili kundi.

Labda swali la kujiuliza hapa ni kwamba unautumia KWELI uwezo wako? Unautumia?

Kama hautumii uwezo wako ipasavyo, unadhani kitu gani kinakuzuia wewe kuweza kufanya hivyo?

Amua kuanzia leo hii kuwa nitakutumia uwezo wangu.
Nitakutumia kipaji changu, nitatumia ubunifu wangu au chochote kile nilichonacho.

Kitumie tafadhali, manufaa siyo kwa ajili yako tu. Bali yanakuwa kwa watu wote

Mpaka hapo umenielewa?

Kama umenielewa, weka email yako hapa chini, ili niendelee kukuelewesha zaidi kupitia jumbe zangu za kipekee nikazotuma kwa njia ya email kila siku.

Jaza taarifa zako hapa👇🏿👇🏿


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X