Njia Bora Ya Kukusaidia Kuishi Maisha Yako Kikamilifu


Unaendeleaje upande wa huko.  Mimi naendelea vyema kabisa.
Leo ni jumapili ya tarehe 10.  Siku 100 za kwanza za mwaka huu zimeisha. Na Sasa zimebaki siku 265.

Najua tangu mwaka huu umeanza lazima Kuna kitu uliazimia kuwa utakifanyia kazi. Sasa swali langu kwako, ni je, bado hiki kitu unakifanyia kazi, au ndio tayari umekata tamaa?

Ninachotaka kukwambia ni kwamba, bado nafasi ya wewe kufanya makubwa ipo. Siku 265 zilizobaki ukizitumia vizuri, una nafasi ya kufanya makubwa.

Ndio maana leo nimeona nikushirikishe wewe mbinu ya kukusaidia  kuishi maisha yako kikamilifu

Njia hii ni wewe kuhakikisha kwamba unaweka nguvu zako kwenye malengo uliyonayo. Malengo yako uyape kipaumbele.

Achana na kufuatilia maisha ya watu wengine Kama vile ndiyi kazi uliyozaliwa kufanya. Badala yake malengo yako yawe ndio kipaumbele.

Malengo yako yakiwa kipaumbele haya hapa ndio yatatokea.

Kwanza, utakuwa bize na maisha yako.
Pili, utajisukuma kuweza kwenda mbali na kufanya makubwa kuliko ulivyozoea
Tatu, utajifunza  zaidi na zaidi kuhusiana na malengo yako.

Vitu hivi tu, vitakusaidia kuendelea kuyafanyia kazi malengo yako kwa ufanisi zaidi.

Sasa rafiki yangu, kazi yako ya leo. Angalia vitu vyote vilivyokuzunguka na ambavyo vinakunyima wewe nafasi ya kufanikisha malengo yako. Viweke pembeni, Kisha weka juhudi na bidii zaidi kwenye kufanyia kazi malengo yako


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X