Deprecated: Constant FILTER_SANITIZE_STRING is deprecated in /home/songambele/public_html/wp-content/plugins/blogger-to-wordpress-redirection old/b2w-redirection.php on line 91
Niseme kitu kuhusu Elon Muskย  Kununua Twitter Au Basi!๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ - SONGA MBELE

Niseme kitu kuhusu Elon Muskย  Kununua Twitter Au Basi!๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ


Udhaifu wangu mkubwa Ni kwamba ninapokuwa na kitu kikubwa kinachoweza kukusaidia wewe kufanya makubwa siwezi kukaa nacho!

Nashindwa kabisa  kujizuia,  Ndio maana leo nikaona nikujuze habari za Elon Musk

Habari zilizotawala vyombo mbalimbali vya habari na hasa mtandao wa intaneti siku ya jana ni kuhusu bilionea Elon Musk kuwekeza kwenye kampuni ya Twitter. Ambapo amenunua asilimia 9.18%

Kitu kinachomfanya yeye kuwa mwekezaji mkubwa kwenye hiyo kampuni.

Kama ulikuwa hujui Ni kwamba: ukiwa mwekezaji mkubwaa kwenye kampuni maana yake unakuwa na nafasi ya kufanya maamumizi kwenye kampuni, unakuwa na uwezo wa kupush baadhi ya mambo kwa kutumia wingi wa hisa zako.

Asilimia 9.18 haimfanyi Elon Musk kuwa na maamuzi kamili juu ya kampuni ya Twitter. Maana ili uwe na maamuzi kamili unapaswa kuwa na walau asilimia 51 ya kampuni ila inafanya usemi wake kwenye kampuni kuwa na uzito mkubwa.

Kuna mambo mawili tu nataka ujifunze kutoka kwa Elon Musk siku ya leo kuhusiananna hiki kitu…

1. Ukiamua kuwekeza wekeza
Umeshafuatilia Elon Musk amewekeza kwenye kampuni gani na ana umiliki kiasi gani? Kwenye kampuni yake ya Tesla ana umiliki wa asilimia 17 na SpaceX ana umiliki wa asilimia 54.

Hiki ni kiashiria kuwa huyu jamaa hawekezi kwenye kampuni yoyote kama underdog badala yake anafanya uwekezaji mkubwa haswa.

Hiki kitu kikupe picha na wewe unapofanya uwekezaji. Usiwe mtu wa kufanya uwekezaji wa kudonoa, donoa badala yake amua kufanya uwekezaji mkubwa na wa viwango vya juu bila kuacha.

Hata Kama utakuwa unaanza kidogo, wewe endelea tu kuwekeza kila mara bila ya kurudi nyuma hata kidogo.

2. Ukiamua kufanya kitu kifanye vizuri

Elon Musk amekuwa na historia ya kufanya vizuri kwenye makampuni yake, kitu ambacho kimewapa watu imani alipowekeza  twitter, na hapo watu wanaona kwamba  hata huku anaenda kuleta mabadiliko makubwa.

Imani hiyo tu imefanya hisa za kampuni ya twitter kupanda.


One response to “Niseme kitu kuhusu Elon Muskย  Kununua Twitter Au Basi!๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X