Mwongozo kwa wapambanaji (Hustlers Guide)


Leo nataka nitoe mwongozo maalumu kwa mtu yeyote ambaye anapambmana kufikia mafanikio makubwa sana.

Kama unapambana kufikia mafanikio makubwa hakikisha kwamba

1. una malengo na unayafanyia kazi kila siku bila ya kuchoka

2. unajihusisha na watu sahihi, watu chanya na watu ambao wanaendana na wewe. Watu hasi watakuangusha

3. unaangalia namna ya kubadili ndoto yako kuwa huduma. Angalia namna ambavyo unaweza kuwasaidia watu kutatua matatizo yao kwa kujenga huduma nzuri kwenye ndoto yako. Kumbuka usemi wa Zig Ziglar unaosema kuwa “unaweza kupata chochote unachotaka kwa kuwaswaidia watu kupata kitu wanachotaka.”

4. Kila siku piga hatua haka ni hatu ndogo, kuelekea kwenye mafanikio yako.

5. Usiache kusoma kitabu kila iitwayo leo. Tena anza na hiki hapa chaMAAJABU YA KUSOMA VITABU. kinapatikana bure tu.

6. Jifunze kutoka kwenye makosa ambayo umewahi kufanya siku za nyuma. Usirudie makosa yaleyale kila mara.

8. Usitake kujionesha kwamba wewe ni mtu wa aina fulani. Acha vitendo tu vikuoneshe

9. Fanya mazoezi ya kutosha nyuma ya pazia kabala hujatokea kuonekana mbele ya watu. Yes, fanya mazoezi ya kutosha rafiki yangu.

10. Fanya mazoezi kiasi kwamba ukionekana mbele ya watu, watu wafikri kuwa wewe kipaji chako cha asili, kumbe nyuma ya pazia wewe unapiga kazi kwa namna ambavyo hakuna mtu anajua.

Hiki siyo kitu cha ajabu, akina Ronaldo hawa unaowaona wanafanya vizuri uwanjani nyuma ya pazia wanafanya mazoezi ya kufa mtu. Akina Diamond hawa unaowaona wanatoa nyimbo mara kwa mara, nyuma ya pazia wanarekodi nyimbo nyingi kuliko unavyoweza kutazamia. Ila chache unazoziona ni hizo. Wanafanya mazoezi kwelikweli. Na wewe fanya hivyo.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X