Mjasiriamali ni nani


Siku hizi kumekuwepo na wimbi kubwa la vijana wanaojiajiri. Hiki ni kitu kizuri, hata hivyo wengi wamekuwa wanadhani kujiajiri tu kunakufanya uwe mjasiriamali.

Kwa wengine ujasiriamali umekuwa unahusishwa na kutengeneza bidhaa kama vile sabuni, vitenge, viatu vya kimasai…..

Ukiwa unatengeneza hivyo vitu, wewe ni mjasiriamali. Kama hutengenezi hivyo vitu wewe siyo mjasiriamali. Kitu ambacho siyo kweli?

Ujasiriamali unaanza kwa kutatua tatizo lililopo kwenye jamii. Lakini haushii hapo…
Kutengeneza bidhaa ni sehemu moja. Unaweza kutengeneza bidhaa Ila bidhaa hizo kuuzwa unakuwa bado hujafaulu.

Wengi wamekuwa wanategeneza bidhaa Ila sasa wanashindwa kuziuza. Ujasiriamali wa kweli upo kwenye vitu viwili.

Kutengeneza bidhaa ya kweli au kutoa thamani kubwa na
Kuuza.

Unaweza kutengeneza bidhaa Ila kama hujui kuiuza utabaki unaijua mwenyewe.

Kwa hiyo kama wewe unatengeneza vitenge, viatu vya kimasai au sabuni, usiishie tu kujiita mjasiriamali kwa sababu umejua kutengeneza hizo bidhaa. Nenda kaziuze kwa watu

Ukienda kuuza bidhaa zako ndio utagundua kuwa kazi kubwa haipo kwenye kutengeneza bidhaa bali kuuza.

Kwa hiyo mjasiriamali Ni mtu AMBAYE anatatua changamoto za watu na kuwauzia watu suluhisho.


2 responses to “Mjasiriamali ni nani”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X