MAAJABU YA KUAMKA ASUBUHI NA MAPEMA


Benjamin Franklin ambaye anafahamika kama mwananchi wa kwanza Marekani alikwahi kuandika kwamba kulala mapema na kuamka asubuhi na mapema kunamfanya mtu awe na afya njema, tajiri na mwenye busara. Haya maneno aliyaandika zaidi ya miaka 200 iliyopita kwenye moja ya barua aliyokuwa anaandika kwa mwanae. Pengine Franklin angekuwa anarudi leo hii angeshangaa kwa jinsi maneno hayo machache yalivyopata umaarufu hasa kwenye ulimwengu maendeleo binafsi na hamasa. Maneno yake sasa yanatumika kama sehemu ya kuwahamasisha ili wajenge tabia ya kuamka mapema.

Leo hii ukiingia kwenye mtandao wa Google, na kuandika neno early to bed, early to rise utapata matoke zaidi ya laki mbili na elfu sabini. Hii ndio kusema kwamba huu usemi ni miongoni mwa semi zinazotumika sana.

Kipindi Benjamin Fraklin anasema hivyo hakukuwa na maendeleo makubwa kwenye teknolojia na sayansi kama ilivyo sasa hivi. Tafiti za kisayansi zimethibitisha kwa asilimia 100 kuwa maneno ya Benjamin Franklin ni ya ukweli na uhakika. Hivyo, kulala mapema na kuamka mapema kuna uwezo wa kukufanya uwe na afya njema, uwe tajiri na mwenye busara.

Pengine unaweza kujiuliza nawezaje kuwa na afya njema kwa kulala na kuamka mapema tu? Unaweza kuendelea kujiuliza pia kuwa nawezaje kuwa na utajiri kwa sababu ya kulala na kuamka mapema? Na mwisho unaweza kujiuliza nawezaje kuwa na busara kwa kulala na kuamka mapema?

Sasa hapo naomba uvute kiti chako ili nikuoneshe jinsi kulala mapema kulivyo na nguvu hizo zote na zaidi ya hapo.

JINSI KULALA MAPEMA NA KUAMKA ASUBUHI NA MAPENDA KUNAVYOWEZA KUKUFANYA UWE NA AFYA NJEMA

Imethibitishwa kuwa muda wa kulala kwa mwanadamu yeyote unapaswa kuwa kati ya saa sita mpaka nane. Suala la nani analala masaa sita au saba au nane linategemea na mtu mmoja mmoja. Kuna wale ambao mwili wao unawahitaji kulala saa saba, kuna wale ambao mwili wao unawaruhusu kulala saa nane. Mwili ukiunyima usingizi wa kutosha utakuwa unajichosha na itafikia hatua ambapo wewe mwenyewe utapoteza nguvu na uwezo wako wa kufanya kazi kwa weredi.

Nimewahi kusikia hadithi ya mzee mmoja aliyekuwa bahiri na hakutaka kupanga chumba cha kulala. Hivyo, akawa anajibana na kulala kwenye jiko la kazini kwake. Kadiri siku zilizyokuwa zinasogea mzee huyo akawa kama anaumwa. Ila hospitali walipokuwa wanapima ugonjwa wakawa hawaoni chochote. Ndipo watu walimshauri apange chumba na apate muda wa kutosha wa kulala. Alipopanga chumba ndani ya wiki moja ya kupata usingizi unaoeleweka, afya yake ikawa imerudi kwenye hali ya kawaida.

Kumbe usingizi ni muhimu sana kwa afya yako. Kitu kingine kuhusu kulala mapema ni kwamba, saa moja  unalola kabla ya saa sita usiku ni bora zaidi kuliko masaa matatu unayolala baada ya saa sita za usiku. Yaani,  mwili huwa una mpangilio wake wa kibaiolojia (biological rythm) ambapo katika masaa fulani kuna shughuli zainafanyika. Muda wa kuanzia saa nane mpaka saa 10 ni mida ambayo mwili unakuwa unajitengeneza, hivyo ni muda ambao mtu ananufaika kama ameshalala kwa muda na kuwa kwenye usingizi mzito. Hivyo, kulala mapema kunaufanya mwili kukamilisha zoezi hilo vizuri. Pia mtu anapowahi kulala anapata muda mzuri wa kuwa kwenye usingizi mzito (REM SLEEP) kuliko anayechelewa kulala. Usingizi mzito ndiyo wenye manufaa zaidi kwenye mwili

Kama huamini, toa siku moja ulale saa nne usiku na uamka saa kumi na moja ambayo hayo yatakuwa ni masaa nane kamili. Kisha toa siku nyingine ulale saa saba usiku na uamke saa moja asubuhi. Utagundua kwamba siku uliyolala saa saba usiku na kuamka saa moja asubuhi ni siku ambayo unaamka umechoka huku ukiwa hauna nguvu ila siku uliyoamka saa kumi na moja ni siku ambayo unaamka mwili ukiwa umetulia kwa asilimia zote. Hii ndio maana napenda kukwambia kwamba kulala mapema na kuamka mapena kunamfanya mtu awe mwenye afya njema.

JINSI KULALA MAPEMA NA KUAMKA MAPEMA KUNAVYOWEZA KUKUFANYA UWE TAJIRI


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X