Kozi gani nzuri ya Kusoma chuo inayolipa


Sikumbuki ni mara ngapi watu wamekuwa wakinitafuta kwa ajili tu kuniuliza kozi gani ambayo mtu akisoma itamlipa. Nimejitajidi kujibu swali hili kadiri ninavyoweza kwa kila mtu, Sasa leo nataka nijibu swali hili mwanzo na mwisho.

ujumbe niliopokea kutoka kwa mmoja wa wafuatiliaji wa kazi zangu

Jibu la swali hili halina exception. Haijalishi umehitimu kidato Cha nne na unataka kwenda chuo au umehitimu kidato Cha sita na unatakiwa kwenda chuo. Kama swali lako unajiuliza ni kozi gani inayolipa basi soma hapa uone.

Zamani ulikuwa hivi, ulitakiwa kwenda shuleni, kusoma kwa bidii ili baadaye yje uajiriwe serikalini! Serikalini ndipo kulikuwa na uhakika wa ajira maana ulipoajiriwa huko kulikuwa na uhakika kuwa utafanya kazi mpaka unastaafu na hatimaye ungepata kiiunua mgongo na kwenda zako kifurahia maisha. Siku hizi Mambo YAMEBADILIKA.

Kuna kipindi udkaktari ulikuwa dili sana. Hivyo, kusoma tu udkatari kulikufanya wewe uwe kwenye nafasi nzuri ya kutoboa.
Wanafunzi wengi walikimbizana na kusoma udkaktari na masomo yanayohausiana na udaktari, hata kama hawakuwa na ule moyo wa kutibu.  Nadhani ndio maana kulitokea madkatari waliokuwa wanapasua kichwa badala ya mguu…Natania tu!!
Lakini siku hizi madkatari nao wapo mtaani wanasugua benchi.

chanzo: Jamii Forums

Baadaye uanasheria ulivuma. Kama ulitaka kuajiriwa ulipaswa kuwa mwanasheria. Siku hizi wanasheria nao wanasugua benchi mtaani, hawana ajira.

Ualimu nao kuna kipindi ulitamba sana. Kama ulitaka kuajiriwa ulipaswa kusoma ualimu. Juzi kuna mtu nilikuwa naongea naye akaniambia amesomea ualimu Ila sasa ajira ameamua kwebda kusomea umeme…..

Sasa sijui huko kwenye umeme atapata AJIRA….

Ebu kwanza niache ninywe maji….au niagize soda utalipia wewe 😂😂.

Sasa Kwa nini Ushauri Huu Haufanyi Tena Kazi?

Jibu Ni moja tu. Zama Zimebadilika…

Kabisa. Ushauri wa nenda shuleni, kasome kwa bidii utaajiriwa serikalini umepitwa na wakati. Ulikuwa Ni ushauri wa Zama za viwanda. Mtu yeyote ambaye aliutumia ushauri huu kipindi hicho alitoboa Ila kwa ukiutumia ushauri huohuo, unatoboka mwenyewe…

Nifanyeje Sasa? Nisome kozi gani itakayonipa ajira. Ukweli ni kwamba kozi inayolipa kwa sasa ipo moja tu ila yenyewe haupaswi kuisoma kwa mkumbo wa kuajiriwa.  Nakuomba sasa uangalie video hii hapa chini ambapo nimeeleza kwa kina kozi inayolipa zaidi kwenye zama hizi


One response to “Kozi gani nzuri ya Kusoma chuo inayolipa”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X