Kitu kingine kimoja cha ziada kuhusu Masoud Kipanya


Au wewe hukupenda….

Nashukuru wengi waliipokea vizuri mkala ya Jana, hata hivyo leo nimeona nitaongeza kitu kimoja.

Unachopaswa kufahamu ni kuwa sijalipwa na mtu yeyote kuandika ninayoandika. Ninaamdika mwenyewe tu kwa mapenzi yangu. Ni hivyo tu….

Kitu chenyewe ninachotaka ujue ni kuedesha BIASHARA kitalaam tangu siku ya ya kwanza (day one)

Umeelewa hapo au nirudie.

Ukiangalia hapo utagundua kwamba japo ndio kwanza kampuni yake inaanza, ila tayari ana timu ya mauzo, ana timu ya uzalishaji, mkurugenzi msaidizi,
Logo n.k.

Hapo unagundua kitu kikubwa ambacho BIASHARA nyingi zinakosa. Mfumo sahihi wa kuendesha Biashara.

Ebu niambie, wewe kwenye BIASHARA yako una mkurugenzi wa uzalishaji.
Mkurugenzi wa masoko na mauzo
Mkurugenzi mkuu na msaidizi wake
Biashara yako ina logo?

Najua unaweza kujitetea kwa kusema kuwa biashara yako ni ndogo, ila unachopaswa kufahamu ni kuwa kama una ndoto na mpango wa kuipeleka mbali biashara yako, utapaswa kuipangilia kihivyo.
Utapaswa kuwa na meneja wa uzalishaji hata kama unafanya biashara ya rejareja.
Utapaswa kuwa na meneja wa masoko hata kama uko peke yako kwenye biashara!

Unaona eeh!

Najua utaanza kuniambia, ooh unajua BIASHARA yangu siyo kama ya Masoud. Shauri yako…

BIASHARA yotote unahitaji hivyo vitu.

Tatizo lalo wewe unafanya vitu kienyeji halafu ukiambiwa, unakuwa mhishi kweli….

Ka uko peke yako utapaswa kugawa majukumu yako na kila Mara ujue ni lini unafanya majukumu kwenye idara gani.
Ukienda kununua bidhaa, ujue kabisa kwamba hapo upo kwenye uzalishaji kwa biashara za rejareja na jumla.

Ukiwashawishi wateja waje kwenye biashara yako, hayo ni masoko.

Ukiuza hayo ni mauzo

Fahamu hivi vitu, vitakusaidia weww kuendesha biashara yako kitalaamu.


2 responses to “Kitu kingine kimoja cha ziada kuhusu Masoud Kipanya”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X