Kitu kinachowakwamisha wengi ukiwemo wewe


Wengi wanakwama kwenye maisha, siyo kwa sababu nyingine bali kwa sababu tu ya UJUAJI. Yaani, wanajua, na hata hii makala wataipitia juu juu kwa sababu tu wanajua.

Umewahi kuona watu wa aina hiyo ee. Ukianza kuongea naye jambo anakwambia na hilo nalijua.

Mkianza kuongelea mada fulani, anajijua. Yaani, anajua kila kitu, 

Kwenye mahusiano, yeye ndiye nyota.

Mkiongelea michezo anajua kila kitu.

Mkiongelea kuhusu siasa, anajua kila kitu.

Mkiongelea usomaji wa vitabu, anajua kila kitabu,

Mkiongelea wasanii, anajua kila kitu mpaka chakula waichokula leo…..

UJUAJI, UJUAJI, UJUAJI.

Muda mwingine wewe unapaswa kuwa msikivu. Wasikilieze wengine wanasemaje, utapata kujifunza mengi, na utapata mengi ya kufanyia kazi kwenye maisha kuliko ukiwa mjuaji zaidi.

Wengi wanakwama maishani kwa sababu ya ujuaji mwingi. Mtu anasoma makalaunayoandika kwa juu kwa kusema kwamba ANAJUA.

Au mwingine anasoma ila hafanyi kazi, kwa kusema kwamba anajua.

Mwisho wa siku hapati matokeo. Anaendelea kuwa na maisha yaleyale.

Labda nikuulize, ni kwa kiwango gani ujuaji umekukwamisha wewe kufika mbali maishani. TOA MAONI YAKO HAPA CHINI


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X