Kama unafikiri elimu Ni ghali, jaribu ujinga


Siku Kama mbili zilizopita hivi, nilikuwa naongea na mama mmoja ambaye anamiliki salooon kubwa mkoani Mwanza. Katika kuongea aliniambia kitu ambacho nilikidaka vizuri. Alisema, Mimi nimetumia gharama kubwa kujifunza mambo ya saloon. Gharama ambayo nimewekeza Ni kubwa sana.

Hiki kitu kilikumbusha Ile stori ya kwamba Kama unafikiri elimu Ni ghali jaribu ujinga.

Na kitu ambacho kinaonekana kwa mtu yeyote ambaye amebobea. Hakuna MBOBEVU yeyote ambaye amebobea ndani ya siku moja. Wote wamewekeza gharama tena kwa muda mrefu, kabla ya kufikia hapo unapowaona sasa hivi.

Katika ulimwengu wa leo wengi wanapenda matokeo ya haraka bila kulipa gharama. Unaweza kuyapata ila fahamu kuwa hayatakuwa ya kudumu.

Kuna watu wengi ambao wanapenda wapate elimu nzuri bila kulipia, rafiki yangu mpendwa, elimu ni gharama. Tena siyo gharama kidogo, gharama kubwa.

Wakati mwingine unakuta gharama unayilipia haiendani na thamani kubwa utakayoipata kwenye kitu husika. Huwa napenda kutokea mfano wa vitabu vyangu. Labda kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO au KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI. Hivi vitabu thamani yake ni kubwa kuliko unacholipia.

Kama na wewe upo tayari kulipia kidogo, rusha elfu ishirini nikutumie vyote viwili. Kila kimoja ni elfu elfu kumi. Hizo Ni soft copy.

Kila hardcocopy ni elfu 20.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X