Jinsi Teknolojia Kidogo Inavyoweza Kuleta Mabadiliko Makubwa Kwenye Biashara


Siyo kwamba mara zote utahitaji kuwa wa kwanza kufanya kitu fulani ili ufanikiwe.

Ukweli ni kwamba muda mwingine utahitaji ubunifu kidogo. Au utahitaji kuweka teknolojia kidogo tu na kubadili kila kitu.

Mfano Amazon, ujue wazo lao la kuuza vitabu halikuwaa jipya au hata bidhaa nyingine walizokuja kuuza baadaye.
Watu walikuwa wananua na kuuza vitabu kabla yao. Kampuni ya WARMART ulikuwa unafanya hiyo biashara.

Wenyewe walichofanya ilikuwa ni kuongeza teknolojia kidogo tu kwenye kitu kilichokuwepo.

Waliona kweli watu wanahitaki kusoma vitabu, ngoja niongeze teknolojia kidogo tu niwasaidie watu kupata vitabu mtandaoni.

Kitu kilichokuwepo kikapewa teknolojia na watu wakakipenda sana.

Wewe pia huhitaji kuwa wa kwanza ili ufanye makubwa. Kwanza ukiwa wa kwanza kabisa watu wanaweza hata wasinunue bidhaa ZAKO.

Matatizo ya watu ni yaleyale unachohitaji wewe Ni

Kuongeza teknolojia kidogo kwenye kitu ambacho watu wamekizoea.
Watu wamezoea kusoma vitabu, unawawekea mtandaoni. GETVALUE, AMAZON.

Watu wamezoea kutafuta taarifa, warahisishie upatikanaji. GOOGLE, BING

Watu wanapenda kuwasiliana wape nAmna ya kuwasiliana. APPLE, SAMSUNG, AMAZON, TECHNO

Watu wanapenda kuwatumia ndugu zao fedha, Ila sasa utumaji siyo wa kuamininika. Hivyo, watengenezee teknolojia nzuri ya kutuma na kupokea fedha. M-PESA

Watu wanapenda kuangalia tamthiliya, ongeza teknolojia kidogo, Kisha wape movie za kutosha. NETFLIX.

Watu wanasafiri, na teksi ni kitu muhimu kwenye usafiri. Wasaidie kupata teksi kwa haraka popote walipo. UBER

Kwa hiyo nisikilize. Huhitaji hata kuwa wa kwanza kufanya kitu cha kipekee ambacho hakijawahi kifanyika. Angalia Vitu vilivyopo Sasa hivi. Kisha jiulize ni teknolojia gani kidogo naweza kuongeza hapa ikaleta matokeo ya tofauti.

Na kwenye biashara yako hiyohiyo. Jiulize ni teknolojia gani unaweza kuongeza sasa hivi ikarahisisha upatikanaji wa huduma na kuongeza mauzo?

Kama ipo, itumie.


One response to “Jinsi Teknolojia Kidogo Inavyoweza Kuleta Mabadiliko Makubwa Kwenye Biashara”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X