Hii Ndio Gharama Halisi Ya Kufanikiwa. Upo tayari Kuilipa?


Unaweza ukawa unajilinganisha na watu wengine na pengine kuona kama unachelewa  kufanikiwa ukilinganisha na wengine.

Ila sasa usichokijua ni nguvu na juhudi lakini pia miaka ambayo hao watu wamekuwa wakifanya kitu ambacho wanafanya.

Unawajua imewachukua miaka mingapi kufikia walipofikia?

Ebu kwa mfano tuseme wewe ni kijana amayependa utangazaji, na  Salim Kikeke ni mtu unayetamani mafanikio yake!  Unajua miaka mingapi amekuwa kwenye industry ya utangazaji? Unajua?

Ukifuatilia utagundua kuwa amekuwa  akifanya anachofanya kwa miaka mingi.

Sasa swali langu kwako, upo tayari kulipa gharama unayotakiwa ili uweze kufikia kule unapotaka! Upo tayari? Upo tayari kukifanya kwa miaka yote kama ambavyo yeye amefanya

Hapo Sasa ndio ujue kuwa mafanikio makubwa siyo rahisi, yanachukua muda.

Na hili siyo kukuogopesha bali kukuonesha uhalisia wa kile unachotakiwa kufanya mpaka ufike kule unapotaka.

Sasa leo nataka uangalie video hii niliyorekodi miaka Kama kumi iliyopita😂😂. Halafu, ukishaiangalia. Subscribe kwenye channel yangu pia.

Mpaka wakati mwingine, mimini GODIUS RWEYONGEZA
0755848391
Morogoro-Tz

NB: LEO nataka ufanye kitu kimoja tu, uangalie video ya gu yotote YouTube. Kisha usubscribe na kuwashirikisha wengine.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X